Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi wa Kata ya Majengo Tunduma waliovunjiwa nyumba zao?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Pamoja na majibu ya Naibu Waziri lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; baadhi ya wananchi waliovunjiwa nyumba hizi tayari walikuwa na hati ambazo zilikuwa zimetolewa na Serikali. Sasa je, Serikali haioni imefanya maonezi makubwa kwa kuwavunjia wananchi ambao tayari walikuwa na hati zilitolewa na Serikali yenyewe? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili nataka kujua sasa ni lini Serikali itatoa viwanja mbadala kwa wananchi hao ili kutokuwaumiza kama walivyofanya sasa? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la hati miliki pia kuhusiana na suala la pili la viwanja mbadala kwa kuwa jambo au shauri hili liko mahakamani, ningeomba tuwe na subira na tutakapopata mwongozo wa mahakama tutakuja kueleza hatua zinazofuatia.