Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Sera Mpya ya Elimu ya mwaka 2014 inatambua upatikanaji wa elimu ya msingi bure; lakini Serikali imeshindwa kupeleka ruzuku ya shilingi 10,000 kwa kila mwanafunzi wa shule za msingi za umma na shilingi 25,000/= kwa kila mwanafunzi wa shule za sekondari za umma:- Je, Serikali inaweza kuweka mchanganuo wa jinsi gani itakavyoweza kutekeleza Sera ya Elimu ya mwaka 2014 kwa kutoa elimu bure bila kuathiri ubora wa elimu?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kutoa masahihisho, Naibu Waziri wakati anajibu aliniita Malopo naitwa Malapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu hayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Serikali iko tayari sasa kuwaambia wananchi kuwa haiko tayari kutekeleza Sera ya Elimu Bure kwa maana halisi ya Kiswahili ya neno bure isipokuwa elimu inayotolewa sasa ni ya kuchangia gharama? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nini wito wa Serikali kwa wananchi kuhusu sera hii ili kuwawezesha walimu kufanya kazi yao bila kero kutoka kwa wazazi wanaofikiri hawawajibiki kulipa pesa yoyote kwa ajili ya elimu hiyo kwa watoto wao? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante. Kwanza naomba radhi kwa kukosea jina la Mheshimiwa Mbunge ni Malapo na nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala kwamba Serikali iseme haina nia ya dhati katika suala zima la elimu bure, ndugu zangu naomba niwaambie, kama sisi ni mashahidi wa kweli vijana wengi waliokuwa wanaenda sekondari walikuwa wanashindwa kulipa hizi gharama za kawaida. Hata wale waliokuwa wanaanza elimu ya msingi mnafahamu wazazi wengi sana wanashindwa kulipa zile gharama za awali ili mtoto wake aweze kujiunga na shule na ninyi wenyewe ni mashahidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi juzi kupitia vyombo vya habari wazazi wanakiri kabisa kwamba suala hili limewasaidia kwa kiwango kikubwa vijana wao kwenda shule. Hata turn over katika shule zetu imekuwaje? Hata madarasa wakati mwingine shule zinahemewa kwa sababu wazazi wote ambao mwanzo walikuwa wanakwazika na gharama hizi sasa wanapata fursa ya kuwapeleka watoto wao shule. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tukiri kwamba Serikali katika hili imefanya juhudi kubwa sana. Naamini jambo lolote lazima lina changamoto zake, hizi changamoto ndogo-ndogo ni kwa ajili ya kuboresha ili mradi mpango uende vizuri lakini dhana ya Serikali imekamilika na inaenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya pili, wito wa Serikali Walimu wasibughudhi wazazi, nadhani tumeshasema wazi na Waziri wangu jana alilisema wazi kwamba jambo kubwa elimu hii ni bure. Hatutarajii mwalimu awazuie watoto kwenda shule kwa kuzusha mchango wake mwenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili tumesema tutakuwa wakali sana kwani lengo kubwa ni mtoto wa Kitanzania aweze kupata elimu ya shule ya msingi na ya sekondari mpaka form four. Lengo ni kwamba kila mwanafunzi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania apate fursa ya uongozi na mikakati ya Serikali ya Awamu ya Tano.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuongezea majibu mazuri yaliyotolewa na Naibu Waziri wa TAMISEMI kutokana na maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Malapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imefanya jitihada kubwa katika suala hili la elimu bure, lakini inasikitishwa kwamba wenzetu walihoji fedha hizi zimetoka wapi kwenye bajeti na leo fedha hii iliyotolewa kwa ajili ya kusaidia jamii maskini watoto wao waende shule wanahoji tena hiyo bure gani, ni mkanganyiko ambao haueleweki. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niseme tu, katika kila shule za msingi za kutwa tutapeleka kila mwezi shilingi 600/= kwa kila mtoto kwa ajili ya uendeshaji. Kwa shule za sekondari za kutwa tunapeleka kwa kila mwezi shilingi 3,540.57/= kwa kila mtoto kwa ajili ya uendeshaji wa shule. Kwa wale wa bweni tunapeleka shilingi 7,243.39/= kwa kila mwezi. Fedha hizi zikijumlishwa uwezekano wa kuendesha elimu upo pamoja na changamoto zilizopo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo ninavyozungumza kutokana na mpango huu wa elimu msingi bila malipo pale ambapo tulitegemea wajiandikishwe watoto 80 kuanza darasa la kwanza wamejiandikisha 240; pale tulipotaka wajiandikishe watoto 180 wamejiandikisha karibu 700 na hiyo ni Dar es Salaam tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, yako baadhi ya maeneo uwezekano tu wa kuwapokea watoto hawa ni mgumu kwa sababu wazazi maskini wameona mpango huu ni muhimu kwao na umewasaidia sana.
Kwa hiyo, kuubezabeza hapa ni kwenda kinyume kabisa na wananchi ambao wanaona mpango huu umewasaidia na kwa hakika kusema kweli unalisaidia Taifa. Tupingane katika mengine lakini kwenye jambo zuri tutiane moyo kama Watanzania. (Makofi)

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Sera Mpya ya Elimu ya mwaka 2014 inatambua upatikanaji wa elimu ya msingi bure; lakini Serikali imeshindwa kupeleka ruzuku ya shilingi 10,000 kwa kila mwanafunzi wa shule za msingi za umma na shilingi 25,000/= kwa kila mwanafunzi wa shule za sekondari za umma:- Je, Serikali inaweza kuweka mchanganuo wa jinsi gani itakavyoweza kutekeleza Sera ya Elimu ya mwaka 2014 kwa kutoa elimu bure bila kuathiri ubora wa elimu?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona, naitwa Mwalimu Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika huu mpango wa Serikali wa kutoa elimu bure, napenda kufahamu Serikali ina mpango gani sasa kuboresha maslahi ya walimu kwa mpango utakaoitwa elimu bure na maslahi bora kwa walimu?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua umuhimu wa ualimu, lakini vilevile tunatambua umuhimu wa watumishi wote wa umma. Lakini kwa kutambua umuhimu huo wa walimu kama Serikali, kwa miaka takribani nane tumeshapandisha takribani asilimia 160 ya mshahara wa walimu. Ukiangalia hivi sasa mwalimu wa chini kabisa anapata shilingi 419,000/=, na wa juu anapata shilingi 719,000/=. Tunatambua bado mazingira ya kuishi gharama ni kubwa na wanahitaji kuongezewa kipato na tutafanya hivyo kwa kadri hali ya uchumi itakavyokuwa ikiruhusu.