Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, kuna mpango wowote kubadili mwelekeo wa ujenzi Barabara ya Tanga kupitia Handeni, Kiberashi, Mrijo, Mondo Bicha hadi Kwamtoro?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa wananchi wa Kondoa Mondo, walikuwa wanasubiria ujenzi wa barabara hiyo, sasa hivi inaonekana kwamba imekwepeshwa. Sasa Serikali ina mpango gani juu ya kuijenga barabara hiyo hiyo ambayo imeandikwa kwenye Ilani kutokea Mondo kwenda Kondoa - Bicha – Guseria kwenda kwa Mtoro?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi walikuwa na matumaini, kwamba kilomita hizi 400 zingepita kwenye Daraja la Mto Bubu, je, Serikali sasa ina mpango gani wa kuharakisha ujenzi wa lile daraja ambalo litaunganisha barabara hii iliyokuwa inategemewa ili kuondoa kero na kuokoa maisha ya wananchi na mali zao vinavyopotea kila mwaka?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Barabara ya kuanzia Goima – Mondo - Kondoa – Bicha, ipo kwenye Ilani na nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri ya upatikanaji wa fedha barabara hii pia itajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa daraja katika Mto Bubu, Daraja la Mungui, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Kondoa kwamba tunajua changamoto ambayo ipo, upembuzi yakinifu wa daraja hili umeshakamilika na sasa hivi tutakamilisha usanifu wa kina. Meneja wa Mkoa ameshapewa kibali aandae pia na documents za kutangaza daraja hilo kuanza kujengwa. Kwa hiyo, litaanza kujengwa tu mara baada ya kukamilisha usanifu wa kina.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, kuna mpango wowote kubadili mwelekeo wa ujenzi Barabara ya Tanga kupitia Handeni, Kiberashi, Mrijo, Mondo Bicha hadi Kwamtoro?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA B. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ningependa kujua Barabara ya Bariri – Mgeta, ambayo ahadi yake ilitolewa na Mheshimiwa Rais, mwezi wa pili mwaka huu, ni lini itamaliza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Bunda Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Bunda – Mgeta kama alivyoisema, iliahidiwa na viongozi na sisi kama Wizara pamoja na Serikali tunaendelea kutafuta fedha ili kutimiza hiyo ahadi ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.