Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO aliuliza: - Je, nini hatma ya wananchi wa Ubungo Kisiwani waliofanyiwa tathmini ya kulipwa fidia ili wapishe ujenzi wa mradi wa mabasi yaendayo kasi?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza. Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI alifika katika Mtaa wa Ubungo Kisiwani tarehe 14 Mei, 2022 akafanya mkutano na wananchi pale na kulikuwa na mgogoro wa kiwango. Aliagiza kwamba wataalam wakafanye tena tathmini ili warudi kwa wananchi waelewani kuhusu kiwango ambacho kinastahili. Je, ni lini hiyo ripoti itapatikana?

Mheshimiwa Spika, la pili. Kwa kuwa muda mrefu umepita na wananchi pale hamna kinachofanyika na hata anuani za makazi hazijafanyika pale kwa sababu ya suala hili: Kwanini Serikali kupitia Mheshimiwa Naibu Waziri msitoe tamko kwa sababu fidia hii haijulikani italipwa lini na wananchi wanaendelea na maisha yao kama kawaida? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Kitila Alexander Mkumbo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwezi Aprili, Mthamini Mkuu alishamaliza kazi yake na alishasaini. Kwa hiyo, baada ya hili zoezi kukamilika, kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, ni kutafuta fedha. Kwa hiyo, kikubwa ni kwamba tutarudi kukaa na wananchi na kuwaeleza haya yote ambayo yanaendelea.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwondoe tu hofu Mheshimiwa Waziri kwamba kauli ya Serikali ni kwamba bado tunahitaji kuendelea kulitumia lile eneo, na ndiyo maana tunatafuta fedha ili tuwalipe kwa wakati. Kama muda utakuwa umepita, maana yake kuna options mbili kwenye sheria. Moja, kurudia uthamini; na pili, kunaweza kukawa na interest ili kuhakikisha kwamba wale wananchi wanapata fidia stahili kutokana na kutoa eneo lao. Ahsante sana.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO aliuliza: - Je, nini hatma ya wananchi wa Ubungo Kisiwani waliofanyiwa tathmini ya kulipwa fidia ili wapishe ujenzi wa mradi wa mabasi yaendayo kasi?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa changamoto ya ulipaji wa fidia inawakumba pia wakazi wa Mbagala, maeneo ya Kokoto mpaka Kongowe na Tuangoma, bado wanadai fidia kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya Kilwa Road; na kwa kuwa toka imefanyiwa tathmini mwaka 2019 mpaka leo hii hakuna malipo yoyote yanayofanyika kwao: Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia hiyo kwa wananchi wa Mbagala – Kokoto mpaka Kongowe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi wote ambao wamefanyiwa tathmini yao watalipwa haki zao kwa sababu Serikali haina muda wa kutaka kwenda kumtapeli mwananchi yeyote. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi huo. Kwa sababu Serikali ni moja, barabara ile najua iko upande wa TANROADS, basi tutafanya kazi hiyo kwa pamoja kuhakikisha jambo hili linawafikia. Ahsante sana.