Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

Watoto wengi nchini wameendelea kudhalilishwa kwa kukosa malezi bora ya wazazi wao hali inayosababisha waishi maisha ya kuombaomba na kwa kuwa baadhi ya wazazi wanaosababisha hali hiyo ni wanaume wanaoharibu maisha ya wasichana kwa kuwapa mimba na kukwepa jukumu la kulea watoto wanapozaliwa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwabaini wanaume hawa na kuwafikisha mahakamani kwa kosa la kuwatelekeza watoto na kuwasababishia mateso na kuwanyima haki zao za msingi? (b) Je, ni lini Serikali italeta Bungeni muswada wa kufanya marekebisho katika sheria husika ili kuwashughulikia wazazi wanaowatelekeza watoto wao kwa kutowahudumia ipasavyo?

Supplementary Question 1

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa tatizo hili ni kubwa sana nchini kwetu na kwa kuwa wahusika Wizarani wanaonekana kutolitambua vizuri ukubwa wake pamoja na kwamba watoto wa mitaani wanaonekana kila siku; je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuanzisha register pale Wizarani kwake ambako itapokea majina ya wanaume pamoja na wanawake wachache ambao wanatelekeza watoto wao ili aweze kuwa na kumbukumbu nzuri? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri atakubali kupokea ushauri binafsi kutoka kwa wadau wanaokerwa na tatizo hili ili ushauri huo aweze kuutumia katika kuleta mapendekezo ya kurekebisha Sheria Namba 21 ya Watoto?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti naanza na la (b), Serikali iko tayari sana kupokea ushauri kutoka kwa mtu yeyote Yule.
Lakini (a) kwamba Serikali kuanzisha registers pale Wizarani namba nijibu kwamba Serikali kupitia Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009 ambayo ilitungwa na Bunge lako Tukufu, kwenye kile kifungu cha 94 inatoa mamlaka kwa Halmashauri yaani Serikali za Mitaa kuwabaini watoto wote wa mitaani na kuwahudumia.
Kwa maana hiyo Waheshimiwa Wabunge tusikwepe jukumu hili kusimamia utekelezaji wa sheria hii kwenye Halmashauri zetu. Lakini kusema jambo hili litashughulikiwa centrally pale Wizarani wakati watoto wako kwenye Serikali za Mitaa ni kujaribu kuweka urasimu ambao hauhitajiki.
Hivyo Waheshimiwa Wabunge wote na Halmashauri zetu tukiwa kama viongozi wajumbe kwenye Halmashauri hizi, tuweke mikakati mahsusi ya kuwahudumia watoto hawa kule kule kwenye Halmashauri zetu.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

Watoto wengi nchini wameendelea kudhalilishwa kwa kukosa malezi bora ya wazazi wao hali inayosababisha waishi maisha ya kuombaomba na kwa kuwa baadhi ya wazazi wanaosababisha hali hiyo ni wanaume wanaoharibu maisha ya wasichana kwa kuwapa mimba na kukwepa jukumu la kulea watoto wanapozaliwa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwabaini wanaume hawa na kuwafikisha mahakamani kwa kosa la kuwatelekeza watoto na kuwasababishia mateso na kuwanyima haki zao za msingi? (b) Je, ni lini Serikali italeta Bungeni muswada wa kufanya marekebisho katika sheria husika ili kuwashughulikia wazazi wanaowatelekeza watoto wao kwa kutowahudumia ipasavyo?

Supplementary Question 2

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Nimesikia majibu ya Serikali kwa upande wa jinsi Serikali zitakavyoshughulika na hawa watu ambao wanaleta matatizo, lakini kuna matatizo ambayo yanasababishwa na Serikali. Kwa mfano kule Moshi Vijijini katika Kata ya TPC
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
17
watoto wa kike wanatembea kilometa kumi, saba kutoka eneo linaitwa Chemchem kwenda kutafuta shule iliko, na haya ni mashamba ya miwa ambapo kuna mambo membo mengi sana yanaweza kutokea hapo katikati, kuomba lift na vitu kama hivyo. Sasa Serikali inaweza kutuambia nini kuhusiana na hali kama hiyo; labda kujenga mabweni kwenye shule za aina hiyo ambazo ziko mbali kiasi hicho?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya mwanza nilizungumzia suala ambalo Mheshimiwa Komu amelisema na hili linanipa faraja kubwa sana, kuona kila Mbunge hapa anasimama katika ajenda ya kumuokoa mtoto wa kike, hili naomba nishukuru sana. Na katika hili naomba niwaambie Wabunge tutaendelea kwa kadiri iwezekanavyo kuhakikisha kwamba tunasimika mabweni maeneo ya jirani, lakini sio mabweni peke yake, tutahakikisha kwamba jinsi gani tunafanya nguvu ya pamoja kwa ajili ya kuleta solidarity hata kwa wazazi; kwa sababu kuna maeneo mengine mabweni yamejengwa lakini watoto wanapenda kukaa uswahilini au kutembea mbali zaidi kwa sababu kuna mambo yao yale ya ku-discuss zaidi wanayoyapenda.
Kwa hiyo, sisi tutahakikisha kwamba tunasimamia na kuhamasisha wazazi wote; lakini kama Ofisi ya TAMISEMI inaliona hilo kwa sababu Wizara ya Afya imejielekeza vya kutosha katika kumuokoa mtoto wa kike na Wabunge wote, mimi naamini jambo hili tutafanikiwa kwa karibu zaidi.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

Watoto wengi nchini wameendelea kudhalilishwa kwa kukosa malezi bora ya wazazi wao hali inayosababisha waishi maisha ya kuombaomba na kwa kuwa baadhi ya wazazi wanaosababisha hali hiyo ni wanaume wanaoharibu maisha ya wasichana kwa kuwapa mimba na kukwepa jukumu la kulea watoto wanapozaliwa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwabaini wanaume hawa na kuwafikisha mahakamani kwa kosa la kuwatelekeza watoto na kuwasababishia mateso na kuwanyima haki zao za msingi? (b) Je, ni lini Serikali italeta Bungeni muswada wa kufanya marekebisho katika sheria husika ili kuwashughulikia wazazi wanaowatelekeza watoto wao kwa kutowahudumia ipasavyo?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Napenda kuuliza swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri. Kumekuwa na ongezeko kubwa la akina mama wanaojifungua kwa operesheni, na suala hili lilikuwa linahusishwa pia na maadili ya madaktari wetu. Je, Serikali ina tamko gani kwamba suala hili ni suala la kitaalam au ni mmomonyoko wa maadili miongoni mwa madaktari? Ahsante.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kujifungua kwa operation ni jambo ambalo haliwezi kuwa la kukiuka maadili, bali ni jambo la kitaalamu. Kuna sababu na vigezo mahususi ambavyo hupelekea daktari akafanya uamuzi wa kumpeleka mama mjamzito kwenda kujifungua kwa njia ya operation (caesarean section) na kitu chema sana kufanya uamuzi huo kwa sababu huokoa maisha ya mama na mtoto kuliko kusubiria kujifungua kwa njia ya kawaida ambapo mama mjamzito anaweza akaingia kwenye hali hatarishi.