Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Makurunge watapatiwa eneo la makazi la Razaba baada ya maeneo yao kuchukuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo inadaiwa viwanja takribani 1,000 na pia hao wananchi wa Makurunge hawana sehemu ya kukaa ambayo ipo sahihi.

Je, ni lini Serikali au Wizara itawapatia Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo mashamba mawili ambayo ni Greenwood na Jeneta ambayo umiliki wake ni wa utata ili kuweza kuwasidia wananchi hawa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mheshimiwa Waziri ni lini anaweza akaja Bagamoyo ili kuja kuyaangalia yale mashamba ya Greenwood na Jeneta ili atoe tamko la Serikali kuhusu umiliki wake yale mashamba? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Muharami Shabani Mkenge, Mbunge wa Bagamoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, juu ya shamba la Greenwood na Jeneta nadhani taratibu za kisheria zinaeleza na wananchi wa Bagamoyo wanatakiwa wafuate hizo taratibu kama kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo ili kama Serikali itajiridhisha juu ya maombi yao na kama ninavyosema kwamba kutakuwa na utata wowote basi tutaangalia kuona jinsi gani tunaweza kuliamua.

Mheshimiwa Spika, juu ya suala la pili, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie tutakamaliza Bunge hili katika kipindi nitakachokuwa kwenye ziara katika Jimbo langu litakuja Bagamoyo ili tuweze kushughulikia kero hiyo. (Makofi)