Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT.OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa skimu za umwagiliaji Wilayani Muleba?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipatia fursa ya kuuliza maswali mawili madogo nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hizi Skimu za Buhangaza, Kyota na Kyamyorwa ni za muda mrefu, zilijengwa kwa fedha za walipa kodi wa Tanzania lakini hazijakamilika kwa maana hiyo tumezamisha fedha za walipa kodi lakini hakuna tunachokipata.

Je, hizi skimu nataka kupata commitment ya Serikali ni lini zitakamilishwa ili ziweze kutumika kama ilivyokusudiwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Kagera tumebarikiwa kuwa na bonde Mto Ngono, ni bonde kubwa linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji maji. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanza kulitumia hilo Bonde la Mto Ngono kwa kilimo cha umwagiliaji? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika majibu yangu ya msingi nimeeleza mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwanza tumefanya tathmini ya kina ya skimu hizi kufahamu gharama halisi na baadaye utekelezaji wake utaanzia mwaka 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili la kuhusiana na Bonde la Mto Ngono, niliwahi kutoa maelezo hapa naomba niyarudie; ukiangalia katika jedwali la saba katika kitabu cha bajeti cha Wizara ya Kilimo tumeainisha mabonde 22 ambayo Serikali itakwenda kuyapitia kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina likiwemo Bonde la Mto Ngono.

Mheshimiwa Spika, nataka niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge wanaotoka Mkoa wa Kagera nafahamu hili ni eneo ambalo mmekuwa mkilipa kipaumbele kikubwa sana, tumeanza na upembuzi yakinifu tutajenga skimu katika Mto Ngono na umwagiliaji utafanyika na wananchi wa Kagera watanufaika na bonde hilo. (Makofi)