Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Raphael Masunga Chegeni
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busega
Primary Question
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. JAPHET N. HASUNGA) aliuliza:- Sheria ya Mahusiano Kazini ya mwaka 2004 inawataka wafanyakazi kujiunga na vyama vya wafanyakazi vya kisekta; walimu na wafanyakazi wengine wamekuwa wakiingizwa kwenye vyama hivyo bila ya wao wenyewe kukubali. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaruhusu wafanyakazi kujiunga na vyama vya wafanyakazi wanavyotaka kwa hiari badala ya kuwalazimisha?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini inafahamika kabisa kwamba vyama hivyo vya wafanyakazi vinakuwa vinachukua matakwa na mahitaji ya wafanyakazi wenyewe. Na kwa kuwa Serikali imekuwa ikiwasaidia sana waweze kuingia katika vyama hivi na Serikali hapa imetoa agizo kwamba itawachukulia hatua waajiri ambao wanawazuia kujiunga na vyama hivi.
Je, Serikali inatoa tamko gani kwa sababu baadhi ya wafanyakazi wanakuwa wamefanya kazi lakini wanakuwa na madai yao mbalimbali ambayo hawajalipwa na Serikali. Kwa mfano, Chama cha Walimu Tanzania kina madai mengi sana Serikalini lakini madai hayo bado hayajalipwa. Je, kupitia bajeti hii, Serikali itatoa tamko la kuwalipa walimu madai yao na malimbikizo yao?
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu tamko Serikali itasema nini, naomba nirudie katika majibu yangu ya msingi ya kwamba Serikali kupitia Sheria Namba 6 ya mwaka 2004 imeendelea kutoa msisitizo kuwataka waajiri wote kuruhusu wafanyakazi wajiunge katika vyama vya wafanyakazi. Na jambo hili ni la kisheria na Kikatiba, na vilevile sisi Tanzania tumekubaliana na ile ILO Convention Namba 87 ambayo inazungumza kuhusu uhuru wa wafanyakazi kujiunga katika vyama vyao.
Kwa hiyo, nichukue tu fursa hii pia kuwataka waajiri kwa kutoa tamko tena ya kwamba wahakikishe kwamba wanawaruhusu wafanyakazi wao wote kujiunga na vyama vya wafanyakazi kwa sababu hii ni haki yao ya kimsingi ya kushirikiana kama ambavyo imesemwa kwenye sheria na kwenye Ibara 20 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuongezea katika majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri,katika Ofisi ya Waziri Mkuu. Ni kwamba, katika suala zima la madai ya walimu, tumezungumza kwamba sasa hivi Ofisi ya Rais - TAMISEMI inafanya uhakiki wa madai yote. Lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba walimu wote ambao wanadai, na si walimu peke yake bali katika kada mbalimbali, katika kipindi hiki cha mwaka wa fedha unaokuja basi madai yote tuweze kuya-address; kila mtu afanye kazi kwa morale katika mazingira yake ya kazi.
Name
Mary Pius Chatanda
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Korogwe Mjini
Primary Question
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. JAPHET N. HASUNGA) aliuliza:- Sheria ya Mahusiano Kazini ya mwaka 2004 inawataka wafanyakazi kujiunga na vyama vya wafanyakazi vya kisekta; walimu na wafanyakazi wengine wamekuwa wakiingizwa kwenye vyama hivyo bila ya wao wenyewe kukubali. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaruhusu wafanyakazi kujiunga na vyama vya wafanyakazi wanavyotaka kwa hiari badala ya kuwalazimisha?
Supplementary Question 2
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa walimu wamejiunga na PSPF lakini walimu hawa wanapoomba mikopo watu wa PSPF wanachelewa sana kuwapa majibu na kuwakamilishia haki yao ya msingi ambapo wengine wanakuwa wamekaribia kustaafu wanataka wajiandae. Je, Serikali inawaelezaje walimu hawa ambao wanakaribia kustaafu na wanahitaji wapate huo mkopo wanawacheleweshea kuwapa mkopo huo?
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ni haki ya walimu waliojiunga katika mfuko wa PSPF kupata mkopo pale ambapo wamekidhi yale masharti yanayohitajika, kwa maana umri ule wa kustaafu ambao kwa mujibu wa taratibu za sasa za mfuko ule, tayari wamekwishakuanza kutoa mikopo kwa walimu ambao wamekaribia umri wa kustaaafu kuanzia miaka 55 wakishapeleka maombi yamekuwa yakifanyiwa kazi.
Nichukue tu fursa hii kuwaomba walimu wote ambao watakuwa wamekidhi masharti na vigezo vya kupata mkopo basi wafike katika ofisi zao kwa ajili ya kuweza kupata huduma hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved