Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kiteto – Chemba hadi Singida utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, binafsi naomba kwanza kuipongeza Serikali kwa kuamua kuanza kujenga hata hizo kilometa 20.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, inaunganisha mikoa minne, kwa maana ya Mkoa wa Tanga, Manyara, Dodoma na Singida. Kama hiyo haitoshi, ni kwamba barabara hii ni barabara ambayo Bomba la Mafuta kutoka Hoima Uganda hadi Chongoleani Tanga ndiko linakopita. Sasa nataka kuuliza swali.

Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa haraka na kuhakikisha kwamba kilometa zote 461 zinakamilika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Mheshimiwa Naibu Waziri alifanya ziara ya kupita barabara hii mwaka 2021; na kipindi hiki mvua zinanyesha.

Je, yuko tayari kumwagiza Meneja Barabara Mkoa wa Tanga aweze kufanya marekebisho katika maeneo ambayo yameharibika?Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Kigua pamoja na Waheshimia wote ambao barabara hii inawagusa ambao wamekuwa wanaifuatilia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wameipitisha barabara hii kama ni barabara ya kipaumbele kutokana na umuhimu wake kwa ajili ya bomba la mafuta. Maana linapopita bomba la mafuta ndiyo barabara hii inakopita. Kwa hiyo, Serikali ina mpango kwa kushirikiana na nchi nyingine kutafuta fedha ili ikiwezekana kilometa zote hizi 461 ziweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, naomba tu kama tulivyotoa agizo kwa wakuu wote wa TANROADS wa Mikoa ahakikishe kwamba anakwenda kwenye madaraja na maeneo yote ambayo yamepata changamoto ya usafiri katika Mkoa wa Tanga; siyo tu kwa Mheshimiwa Kigua, ni pamoja na barabara zake zote ili kuhakikisha kwamba wananchi hawakwami katika kipindi hiki cha mvua. Ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kiteto – Chemba hadi Singida utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri mwaka 2021 alifika kwenye Barabara ya Haydom - Katesh na amejionea hali ya ile barabara ambayo inategemewa na wananchi kwa shughuli za kilimo pamoja na huduma mbalimbali: -

Je, ni lini wananchi wa Jimbo la Hanang na Mbulu watawaona wakandarasi wakiwa kwenye kazi kutengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tutafuatilia na kuona kwamba wakandarasi hawa wanakuwepo site haraka inavyowezekana. Ahsante. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kiteto – Chemba hadi Singida utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kwenye swali la msingi kulikuwa na hiyo barabara ya Kiberashi na imetengewa Kilometa 25 na tender imeshatangazwa; na Mbulu Vijijini, barabara ya Haydom – Mbulu kulikuwa na tender ya namna hiyo hiyo: -

Je, unataumbaje; tenda hiyo imetangazwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ziko nyingi, ikiwepo moja ya Mheshimiwa Flatei Massay ambayo iko kwenye hatua za mwisho za kusainiwa mikataba ili wakandarasi waanze kazi. Ahsante. (Makofi)