Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lushoto – Magamba – Lukozi – Mlalo hadi Umba Junction kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya kutoka Lushoto, Magamba, Lukozi, Mlalo mpaka Umba Junction ni uti wa mgongo wa shughuli za maendeleo na kujenga uchumi wa wananchi wa eneo hilo. Vilevile barabara hii ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya 2015 hadi 2025. Kwa kuwa ipo ahadi ya Serikali ya kuanza kuijenga barabara hii kutoka kilometa moja moja inayofanywa sasa, kwenda katika kuijenga kilometa 10, 10 kila mwaka. Je, ni lini sasa Serikali itaanza utekelezaji wa ahadi hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, imetengwa bajeti kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kutoka mwanzo mpaka kwenye junction ya mwisho ya barabara hii. Je, ni ipi commitment ya Serikali katika kufanya usanifu wa kina na upembuzi yakinifu katika barabara hii ili iweze kuwa mradi kamili?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara iko kwenye ilani na ni ahadi ya viongozi, lakini nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Mheshimiwa Shangazi ambaye najua barabara hii inamhusu sana ameshahakikishiwa na Wizara kwamba katika mwaka huu wa fedha, barabara hii itafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kwa sababu ilikuwa haijafanyika hivyo ndiyo maana ilikuwa ni kusanifu na kujenga. Kwa hiyo tunahakikisha barabara hii itafanyiwa usanifu katika mwaka wa fedha ujao kwa barabara yote. Ahsante.

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lushoto – Magamba – Lukozi – Mlalo hadi Umba Junction kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kulikuwa na mpango wa ujenzi wa barabara ya Tarime kupitia Nyamwaga, Nyamongo mpaka Serengeti lakini kuna taarifa kuwa mpango huo haupo. Je, ni nini tamko la Serikali juu ya barabara hiyo kwa wananchi wale? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ghati Chomete, Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Mara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni swali lingine tena naulizwa, siku mbili zilizopita liliulizwa swali kwenye barabara hii hii. Naomba nimjibu Mheshimiwa Ghati Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mara kwa kumhakikishia tu kwamba, Mheshimiwa Mwita Waitara, Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, jana amekuja ofisini akiwa na madai haya haya, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo na wananchi wa Tarime, mpango huu unaosemwa hakuna mpango uliofutwa. Nataka nimhakikishie kwamba tayari tuko kwenye hatua za kusaini mkataba kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kuanzia Tarime hadi Nyamwaga, kilometa 25 na zabuni inaandaliwa kuanzia Nyamwaga hadi Mugumu kilometa 61. Jumla kilometa hizo 82, kwa hiyo hakuna mpango uliofutwa na iko kwenye mpango.

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lushoto – Magamba – Lukozi – Mlalo hadi Umba Junction kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Spika. Kwa kuwa changamoto iliyopo kwenye barabara ya Lushoto mpaka Mlalo inafanana na changamoto iliyo kwenye barabara ya kutoka Makofia – Mlandizi mpaka Vikumburu.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kipande hiki cha kutoka Makofia – Bagamoyo mpaka Mlandizi kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alice Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara hii iko kwenye ilani na imetengewa bajeti kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami mwaka huu. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ujenzi utaanza mara tu fedha itakapokuwa imepatikana. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Lushoto – Magamba – Lukozi – Mlalo hadi Umba Junction kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukurru kwa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mloo - Kamsamba - Utambalila kupitia Chitete yenye kilometa 145.14 iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020/ 2025 kwenye ukurasa wa 75: -

Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali ilishafanya maandali ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Tayari usanifu wa kina umeshafanyika. Changamoto iliyokuwepo ya Daraja la Momba, imejengwa kwa ajili ya kupokea barabara hiyo. Kwa hiyo, itategemea na fedha zitakapopatikana, kwa sababu taratibu zote za awali zimeshakamilika ili barabara hii ambayo inaunganisha Mkoa wa Songwe, Mkoa wa Rukwa hadi Katavi iweze kujengwa. Ahsante. (Makofi)