Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo cha uzalishaji wa madume bora ya ng’ombe Wilayani Bahi ili kuleta tija kwa wafugaji?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Katika Wilaya ya Mpwapwa kuna idadi kubwa sana ya mifugo, lakini changamoto yetu kule ni ukosefu wa mfumo rasmi wa upatikanaji wa madawa kwa ajili ya kutibu mifugo yetu. Wafugaji kule wanategemea sana walanguzi ambao wakati mwingine wamewauzia dawa feki na zimewasababishia hasara. Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu rasmi wa kuhakikisha kwamba wafugaji wetu wanapata dawa za kutibu magonjwa ya mifugo katika maeneo yao?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Malima, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Afya kwenye vitengo vyetu vya Baraza la Veterinary Tanzania na TMDA kwa pamoja tunafanya operations za mara kwa mara za kufuatilia dawa zisizo na viwango. Kwa mwaka jana tulikamata na hatua za kisheria zilichukuliwa na mwaka huu pia vile vile Mkoani Mwanza tayari yuko mzalishaji na msambazaji wa dawa feki ambaye tumemkamata.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wetu sasa kupitia Baraza hili ni kuhakikisha kwamba udhibiti wa dawa hizi unaimarishwa ikiwa ni pamoja na kuzalisha dawa nyingi zaidi zilizobora kupitia viwanda vyetu vya hapa nchini pamoja na kiwanda cha Serikali kilichoko pale Kibaha kwa maana cha TVI ili wafugaji wetu waweze kupata uhakika wa chanjo na dawa zenye kukidhi viwango.