Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Kanda ya Magharibi kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa jibu zuri la Serikali, lakini kutokana na umuhimu wa hospitali hii ya Kanda ambayo inajumuisha mikoa mitatu; Kigoma, Katavi na Tabora; nataka majibu ambayo yataweza kutuonesha Wana-Kanda ya Magharibi ni lini hasa hospitali hii itaanza kujengwa kutokana na kwamba eneo lilishatengwa kama ambavyo amesema na katika Kata ya Magili kwa hekari 200? Hii itasaidia wananchi wasianze kufanya shughuli za maendeleo kwa kuzingatia ni muda mrefu mchakato huu walishasema utafanyika lakini bado haujafanyika.

Je, Serikali inaweza kutueleza ni lini hasa kazi hii inaweza ikafanyika? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ambavyo nimeshaeleza kwenye swali la msingi kuhusu tathmini; kwanza fedha za kwanza ambazo makadirio ya kuanza, kwa sababu ni fedha ambazo hazitamaliza, lakini zimeshatengwa shilingi bilioni 10 za kuanza, lakini kazi inayofanyika ni kuangalia kwenye mikoa hiyo kuhusu umbali, kwa sababu hatuangalii tu Hospitali ya Kanda kwamba tunaweka Magharibi au wapi, tunaangalia ni mikoa ipi na ni mkoa upi upo mbali na facilities kama hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, ukiangalia kutoka Tabora kuja Benjamin Mkapa ni Kilomita ngapi? Tabora kuja hospitali nyingine ya Kanda ni Kilomita ngapi? Hii itasaidia tuweze kuamua eneo sahihi ambalo huduma itawasogelea wananchi walio wengi na tuangalie eneo ambalo vile vile huduma nyingine ziko mbali na wananchi ambazo wengine wako karibu nazo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, upembuzi bado unafanyika ili kutambua eneo ambalo hospitali itaenda kuwekwa kwa kutumia busara kusogezea huduma wananchi walio wengi zaidi. Ahsante.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Kanda ya Magharibi kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa. Shida ya kujengewa hospitali katika Kanda ya Magharibi inafanana kabisa na shida tuliyonayo Wilaya ya Moshi.

Je, ni lini Serikali itatujengea Hospitali ya Wilaya ya Moshi kwa sababu tayari tumeshapata eneo la ekari 38? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge. Mimi mwenyewe nimetembelea eneo hilo ambalo anasema limetengwa, nimeliona. Kikubwa ni kwamba tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ili kwenye bajeti ya mwaka huu tuweze kuona ni namna gani utekelezaji wa hilo hitaji lao litafanyika. (Makofi)

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Kanda ya Magharibi kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwetu kule Mkoa wa Mbeya Wilaya ya Rungwe kuna hospitali kubwa sana ambayo ilikuwa ikiwatibu watu wenye ugonjwa wa ukoma na watu kutoka nchi mbalimbali walikuwa wakitibiwa ikiwa ni pamoja na Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda na Malawi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali ile, ukoma ulifungwa rasmi mwaka 2002. Majengo yale ni hospitali kubwa ambayo ina wodi ya wanaume, wanawake na watoto, ina mochwari, bwalo, jiko kubwa, mpaka machine ya kuchomea takataka na Makanisa yapo pale, pia heka zaidi ya 100 ziko pale, lakini yamekaa bila kufanyiwa kazi yoyote: -

Je, Serikali ina mpango gani na majengo yale? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kujibu swali zuri la Mheshimiwa Mbunge, ameeleza kwamba kuna hospitali yenye facilities hizo. Sasa niweke tu vizuri kwamba suala la ukoma, bado tunaenda kuongeza nguvu kwa sababu tunataka mwaka 2030 ukoma uwe umeisha kabisa Tanzania. Ila wazo lake hilo ambalo anasema kuna facility hiyo ambayo inaweza kutumika kwa namna nyingine; baada ya Bunge tarehe 24, nitakuwepo Njombe, nitapitia Songwe kuangalia Hospitali ya Mkoa wa Songwe halafu tutaenda pamoja kutembelea hilo eneo na watalaam ili tuweze kuamua kwa kuangalia mazingira halisi na kuleta majibu ambayo yatakuwa sahihi kulingana na hali halisi ya kule. (Makofi)