Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Bandari Kavu ya Isaka?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri kwenye Serikali yetu. Je, ni lini bandari hii itaanza kufanya kazi? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo ameanza kufuatilia tangu nilipoteuliwa tu, alikuja ofisini kwangu kufuatilia suala la Bandari hii ya Isaka iliyopo Mkoani Shinyanga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, anauliza ni lini itaanza hasa. Changamoto kubwa ilikuwa ni kwamba bandari hii ilikuwa haina vitendea kazi. Ilikuwa haina mabehewa, hatuna injini na sasa tumekwishanunua. Nimefanya mkutano jana na Watendaji Wakuu wa Mamlaka ya Bandari pamoja na TRC na nimewaagiza ya kwamba ndani ya wiki hii wanipe ripoti, wafanyabiashara wote ambao wanatumia Bandari ya Dar es Salaam na wanatoka Nchi za Congo, Rwanda na Burundi wakae nao ili waone umuhimu sasa wa kutumia Bandari hii ya Isaka badala ya kuchukulia mizigo yao Dar es Salaam kama ilivyokuwa zamani. (Makofi)

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Bandari Kavu ya Isaka?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kumekuwa na mashindano makubwa sana katika bandari za majirani zetu hasa Mombasa, Kenya na Beira, Msumbiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sijui Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha bandari yetu ya Dar es Salaam ili iweze kuweza kushindana na Bandari hizo za nchi za jirani?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nimpongeze pia Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa Bandari ya Dar es Salaam ni lango la uchumi wa nchi yetu. Sasa anataka kujua je, tuna mikakati gani ya ushindani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika sekta hii ya usafirishaji hususan bandari tuna washindani ambao ni Beira, tuna Durban pamoja na Mombasa. Hivi ninavyosema, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais awali alitoa shilingi bilioni 210 kwa ajili ya kununua vitendea kazi katika ile Bandari ya Dar es Salaam, lakini vifaa vile vilikuwa bado havitoshi na ameongeza shilingi bilioni 290 na kufanya bilioni 500 kwa ajili ya kuongeza ufanisi katika Bandari yetu ya Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo vifaa hivyo kwa kuwa tayari tumeshaagiza na nina hakika kuingia Dar es Salaam tayari, pia tunatengeneza njia za reli kwa ajili ya kwenda kuchukua mzigo na kupeleka katika Bandari hizo ambazo nimezitamka hapo kama Isaka pamoja na nchi jirani za kwenda Zambia. Kwa hiyo tunagemea kwamba ushindani utaimarika zaidi mara tu baada vifaa hivi kuja ili tuwe bora katika nchi zetu za Afrika Mashariki. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Bandari Kavu ya Isaka?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniona. Swali langu litahusu TEMESA na nimeshawasilisha changamoto zake kwa Kamati husika, lakini kwa fursa hii uliyonipa naomba nimuulize Waziri swali moja dogo. Je, kutokana na ucheleweshwaji na gharama kubwa zinazotumiwa na halmashauri zetu wanapopeleka magari na mitambo mingine TEMESA.

Je, Waziri yupo tayari kuiagiza TEMESA kuruhusu halmashauri zenye karakana zake kutengeneza magari yake yenyewe, hasa inapokuwa ni matengenezo madogo madogo?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hili swali la TEMESA ni kwa mujibu wa sheria kwamba magari yote ya Serikali yatengenezwe chini ya TEMESA kwa hiyo, nachukua concern yako kama ambavyo umesema ili nasi tuweze kujadili upande wa Serikali. (Makofi)