Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - (a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)? (b) Je, Serikali haioni kwa kuifuta TFDA itashindwa kudhibiti ubora wa vyakula ipasavyo?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kutokana na kuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukizwa yanayosababishwa na ulaji wa vyakula, kwa mfano cancer na viriba tumbo: Je, Serikali haioni kwamba TBS imeshindwa kudhibiti ubora wa vyakula?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kwa kuwa TBS inadhibiti ubora wa vitu vingi ikiwemo petroli, magari, matairi, chemicals na vitu vingine: Je, Serikali haioni kwa unyeti wa chakula ikaweza kutenganishwa na vitu hivi vingine? Ahsnate. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Neema Mgaya kwa sababu tu ushauri wake hauishii kwenye kutushauri kupitia maswali, lakini amekuwa ni mdau mzuri sana wa Wizara ya Afya katika kutoa ushauri hasa kwenye kuboresha afya za Watanzania. Swali lake la kwanza anadhani sisi hatuoni kwamba kutokana na matatizo ya cancer pamoja na viriba tumbo, inawezekana ikawa ni vigumu kusimamia eneo hilo kama haya mambo yataendelea kubaki TBS. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza moja, hili ni suala la kisheria. Lilikuja Bungeni na ikaonekana sababu za kuweza kuhamisha hizi shughuli ziweze kupelekwa TBS badala ya kubaki Wizara ya Afya. Sasa, wazo lake ni zuri kwa sababu kweli kama ambavyo hata wiki iliyopita na inaonekana masuala ya cancer yamekuwa yakisumbua watu, lakini kuna umuhimu wa masuala ya chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakwenda kujadiliana na Wizara ya Afya na tuko tayari kupokea maelezo na kujadiliana na Wizara ya Viwanda, ambayo ni Wizara husika. Tukiona kuna umuhimu wa kuhamisha, basi tutarudi Bungeni kwa ajili ya kufanya hilo ambalo amelisema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kwamba anadhani vile vile kule TBS wanafanya mambo mengi mengine hayahusiani kabisa na afya. Hata hivyo, nimwambie tu, hata petroli yenyewe ina-impact vile vile kwenye afya. Kwa hiyo, usipoangalia vizuri unaweza ukahamisha kila kitu ukaleta afya. Kwa sababu, petroli ukienda kwa maana ya mazingira na mambo mengine bado yanarudi pale pale kumuumiza binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachoweza kusema, wazo lake ni zuri, lakini ni suala la kisheria na Bunge lilikaa likapitisha, tutaendelea kukusanya maoni ya wadau, tutashirikiana na Wizara ambayo inahusika na masuala hayo. Kukionekana kuna uhitaji wa kurudi Bungeni kubadilisha sheria na mambo hayo yaje Wizara ya Afya, tuko tayari kufanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli input ya Mheshimiwa Mbunge ni muhimu kwa sababu tuna changamoto kubwa sana sasa hivi kwenye masuala mazima ya afya. Mimi nalichukua kama wazo, tunakwenda kuanza kufanyia kazi. Nafikiri na mimi kuna umuhimu wa kuanza kutafakari kama anavyofikiri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - (a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)? (b) Je, Serikali haioni kwa kuifuta TFDA itashindwa kudhibiti ubora wa vyakula ipasavyo?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi. Kwanza nakiri kwamba nimekuwa mtumishi wa TFDA kwa miaka kumi. Niseme, kuhamisha bidhaa za chakula na vipodozi kumekinzana na dhana nzima duniani ya udhibiti wa bidhaa hizo. Ukiangalia nchi zote duniani; uende Marekani bidhaa za chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba, zote zinadhibitiwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, duniani pote ndivyo ilivyo, lakini TFDA imekuwa ni kioo katika East Africa. Wamefundisha Rwanda, wamefundisha hadi Tanzania Visiwani leo tuna ZFDA. Kwa hiyo, kuhamisha kwenda kwenye Bureau of Standards ni jambo ambalo kidunia wanatushangaa. Je, ni lini sasa Serikali italeta sheria hapa ibadilishwe ili hizi bidhaa zidhibitiwe kulingana na matakwa ya kikanda na kimataifa? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri. Kwanza amesema ni practice ya kidunia na pia amesema kwamba TFDA ni mfano kwa East Africa. Nataka kumwambia, ni ya kwanza kwa Afrika nzima. Ndiyo sasa hivi inaongoza kwa Afrika nzima kwa zile standards za kidunia. Kwa hiyo, kwa Afrika ni ya mfano, hata nchi zilizoendelea kuliko sisi tumewapita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi mimi kama ambavyo nimejibu swali la msingi, naona kuna element hapo, lakini kwa sababu walioamua kubadilisha ilikuwa ni suala la kisheria na Bunge likaleta hapa Sheria Na. 8 ya Fedha ilivyobadilishwa ndiyo uamuzi ukafanyika, kwa hiyo, kabla ya kusema tutafanya nini, naomba mtupe muda wa kufanya uchambuzi wa kina kwa kushirikiana na Wizara husika ili tulete maamuzi hapa tusije tukaingilia mambo ambayo yanaweza yasitekelezeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunaelewa concern yenu Wabunge, tunaelewa concern ya swali la msingi. Tutaendelea kulichungulia vizuri na kushirikiana na wadau husika ili tuweze kuona tuendeje. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - (a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)? (b) Je, Serikali haioni kwa kuifuta TFDA itashindwa kudhibiti ubora wa vyakula ipasavyo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nataka niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, majukumu ya TFDA ikiwa ni pamoja na Baraza la Wafamasia ni udhibiti wa dawa. Sasa hivi kumekuwa na tatizo kubwa sana la uuzaji wa dawa holela ikiwa ni pamoja na hizi dawa zinaitwa P2. Nini mkakati wa Serikali wa kudhibiti uuzaji holela wa dawa katika maduka bila kuzingatia misingi na matumizi ya dawa hizo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ameeleza kwamba kuna uuzaji wa dawa kwa namna holela. Kikubwa wala hilo halihitaji kusema tunajipangaje. Hilo liko wazi, zipo hizo taasisi, yupo Mfamasia wa Serikali, ipo Pharmacy Council, wapo TMDA ambao ndiyo wanahusika kufanya hiyo kazi. Straight forward ni kwamba hatutaki kuliona hilo. Waanze kusimamia miongozo na sheria na taratibu za kusimamia masuala mazima ya dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kimsingi ni agizo tu linatoka hapa kwamba inatakiwa hili analolisema Mbunge lisiweze kuonekana tena likitokea kama lipo. Tutakwenda kulifuatilia kama lipo, wanaofanya hivyo watawajibika na vile vile tutaenda kusimamia sheria kama ambavyo ilishapitishwa na Bunge. (Makofi)