Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mnara wa mawasiliano ya simu katika Kata ya Mtego wa Noti ili wananchi waweze kupata huduma ya mawasiliano ya simu?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, naomba nishukuru pia kwa Serikali kutoa majibu mazuri lakini bado naomba niulize swali moja la nyongeza.

Katika Vijiji vya Ilalangulu, Chagu, Katumba na Songambele ni maeneo ambayo yanazungukwa na msitu wa Halmashauri na ambao msitu ule wakati mwingine wananchi wanapata shida ya kutekwa na hivyo kukosa mawasiliano.

Naomba Serikali itoe majibu kwamba ni lini hasa hawa wananchi nao wataweza kupata nafuu ya kupata mawasiliano kwenye vijiji vyao?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimesema katika jibu langu la msingi na pia kwa maelekezo ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi Ibara 61(j) ni haki ya msingi kwa kila wananchi wanaoishi ndani ya nchi yetu kupata mawasiliano; hivyo tunaamini kabisa kwamba baada ya kufanya tathmini na kujiridhisha ukubwa wa tatizo tutaenda kuchukua hatua na kuhakikisha kwamba wanafikishiwa mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, lakini vilevile katika maeneo ambayo yako pembezoni na maeneo ambayo ni ya mbuga tunaamini kwamba katika mkataba huu ambao Mheshimiwa Waziri anaenda kuusimamia ili usainiwe maeneo 90 yanaenda kupata utatuzi wa changamoto wa mawasiliano baada ya kukamilika kwa ujenzi wa minara 90. Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira kipindi ambacho Serikali itakuwa tayari basi tutahakikisha kwamba mawasiliano katika eneo hilo itakuwa imetatuliwa ahsante sana.

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mnara wa mawasiliano ya simu katika Kata ya Mtego wa Noti ili wananchi waweze kupata huduma ya mawasiliano ya simu?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, kata yangu ya Karitu ndiyo kata pekee ambayo bado haijapata mnara wa mawasiliano ya simu Jimboni kwangu. Zaidi ya mara mbili kata hii imekuwa kwenye orodha ya kata ambazo zinapaswa zijengewe minara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote lakini mwaka unaisha haujajengwa.

Sasa swali langu ni kwamba je, Wizara ina mpango gani au mkakati gani wa kuhakikisha kwamba kata zote zinazokuwa kwenye mpango wa kujengewa minara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote basi inajengewa kwa mwaka huo husika wa fedha?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kuhusu kata ya Karitu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Mheshimiwa Mbunge alichokisema na hili limekuwa ni tatizo kwa muda mrefu ni kwamba katika zabuni ambazo zimepita tulitangaza ujenzi wa minara katika maeneo 199 lakini watoa huduma walijitokeza katika maeneo 90. Sisi kama Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote tunatoa ruzuku, ruzuku ambayo tunayoitoa mtoa huduma anaenda kujiridhisha katika eneo ambalo anatakiwa kujenga mnara na baada ya kuona kwamba business case inaonesha kabisa kwamba baada ya muda mrefu kabisa hawezi kupata faida yoyote hivyo maeneo hayo wanayakwepa.

Mheshimiwa Spika, lakini sasa Serikali imeanzisha mazungumzo ili tuangalie namna bora ya kuhakikisha kwamba tunapotangaza maeneo haya basi maeneo yote yapate watoa huduma kulingana na market share ya kila mtoa huduma hapa nchini nakushukuru sana.