Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha makongamano ya Kimataifa ili kukuza utalii wa Mlima Kilimanjaro?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Wizara lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, Wizara ina mkakati gani kuongeza watalii kwa sababu kutokana na UVIKO-19, idadi ya watalii wanaopanda Mlima Kilimanjaro imepungua sana kutoka 50,000 mpaka 12,000 kwa mwaka 2020. Je, Serikali sasa ina mkakati gani wa kuweza kuongeza watalii na kusaidia ajira kwa vijana wanaotegemea mlima huo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; akinamama wajasiriamali wa Kilimanjaro wanaojishughulisha na shughuli za utalii tunaomba na wao waweze kupatiwa mikopo ili waweze kutangaza zaidi mlima wetu, mbuga zetu na utalii kwa ujumla. Ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum Kilimanjaro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Esther kwa juhudi nzuri anazozifanya za kuendelea kutangaza vivutio vya utalii ukiwemo Mlima Kilimanjaro. Nampongeza sana kwa sababu amekuwa ni balozi mzuri wa kuhakikisha eneo hili linaendelea kuvutia watalii wengi.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo ameuliza kwamba tuna mkakati gani wa kuendelea kuongeza watalii na kuongeza ajira kwa vijana. Eneo hili Wizara imekuwa ikibuni mbinu mbalimbali zikiwemo kuanzisha marathons mbalimbali katika maeneo mbalimbali ya hifadhi, lakini lengo ni kuhakikisha kwamba watalii wengi wanakwenda kuviona vivutio lakini pia kuwa mabalozi wa kuendelea kuvitangaza.

Mheshimiwa Spika, hili ni shahidi hata Watanzania wa leo wamekuwa wazalendo na kila mtu sasa hivi anamhabarisha mwenzake kuhakikisha kwamba wanafika kwenye vile vivutio, lakini siyo kufika tu, kuisemea Tanzania ndani ya nchi na maeneo mengine ya nje ya nchi na lengo ni kukuza utalii na kuongeza pato la Taifa. Ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha makongamano ya Kimataifa ili kukuza utalii wa Mlima Kilimanjaro?

Supplementary Question 2

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na kuutangaza Mlima Kilimanjaro ningependa kufahamu, je, Serikali ina mkakati gani wa kutangaza vivutio vidogovidogo ambavyo vipo katika mikoa hasa Mkoa wa Ruvuma, Wilaya ya Mbinga, yenye vivutio vidogo vingi vya kihistoria vyenye kuvutia ili kupata watalii na kuongeza mapato ya ndani?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kapinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na vivutio vidogovidogo ambavyo kwa nia moja au nyingine Serikali ilichelewa kuviibua, lakini Wizara ina mkakati wa kuhakikisha inaibua na kuvitangaza vivutio hivi katika kila mkoa, wilaya na kata.

Mheshimiwa Spika, vivutio vingi vidogovidogo havina GN, hivyo tumeendelea kuelimisha wananchi, kuelimisha Serikali za Vijiji, kata na halmashauri kuhakikisha kwamba yale maeneo ambayo yanasimamiwa na halmashauri ama vijiji wayaibue na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii itatoa wataalam wa kuweza kushauri na kutoa usaidizi wa kuhakikisha kwamba haya maeneo yanapata GN na kuyatangaza na wale watalii waweze kufika katika maeneo hayo. Ahsante.