Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Kahama?

Supplementary Question 1

MHE. ALEXANDER P. MNYETI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Barabara hii tunayoizungumzia hapa ni barabara ambayo imekuwa kwenye Ilani ya Uchaguzi kwa mihula mitatu mfululizo, 2010, 2015 mpaka 2020; na Mheshimiwa Rais alipokuja Misungwi aliahidi barabara hii ianze kutengenezwa kwa kiwango cha lami haraka iwezekanavyo na Mheshimiwa Waziri tulikuwa naye pale, maelekezo ya Rais yalitoka hadharani kuwa barabara hii itengenezwe. Sasa anaposema kwamba anatafuta fedha sijajua yeye ni TRA ama ni nini, kwa sababu mwenye TRA ambaye ni Mheshimiwa Rais amesema barabara ianze kutengenezwa haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, swali langu la nyongeza ni kwamba, ni lini Wizara itaanza kujenga barabara hii? Kwa sababu imekuwa ikikarabati vipande vidogo vidogo ambavyo havina tija yoyote kwenye barabara hii. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pastory Mnyeti, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tayari jitihada za Serikali zimeonekana, tumeshafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Pia ili kuhakikisha kwamba barabara hii inatumika tumeshaanza kujenga madaraja ambayo mara nyingi yanafanya barabara hii isipitike.

Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine wa barabara hii tayari tumeshaanza kujenga kilometa tano upande wa Kahama, ambayo ni barabara hiyo hiyo. Kwa hiyo Serikali ina nia njema na mara fedha itakapopatikana yote barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami kama ahadi za viongozi wa kitaifa walivyoahidi. Ahsante. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Kahama?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Kwa kuwa ni ahadi ya muda mrefu ya viongozi kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Mbalizi - Shigamba. Je, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara imeahidiwa na viongozi mbalimbali wametoa ahadi.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara hii ipo kwenye mipango ya kuanza kufanyiwa usanifu wa kina kama maandalizi ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Kahama?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nikushuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Mkutano wa Tatu wa Bunge lako hili niliulizia kuhusiana na Barabara ya kutoka Kiranjeranje, Nanjilinji mpaka Ruangwa kujengwa kwa kiwango cha lami na majibu ya Serikali ilikuwa kwamba itajengwa mara tu fedha zitakapopatikana.

Mheshimiwa Spika, sasa je, Serikali iko tayari kwa mwaka ujao wa 2022/2023 kutenga fedha kwa ajili ya kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami, ambayo iko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kiranjeranje hadi Ruangwa ambayo Mheshimiwa Mbunge ameisema, ni kweli ipo kwenye Ilani. Hata hivyo, kama nilivyosema, ni kipindi hiki tunachoendelea na bajeti, barabara hii pengine mwaka huu itakuwepo kwenye mpango kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kufanya usanifu wa kina. Ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mwanangwa – Misasi – Kahama?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Changamoto ambayo inawakumba watumiaji wa Bandari ya Kabwe ni barabara inayotoka Lyazumbi kwenda Kabwe na ni agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu. Napenda kujua, ni lini agizo hilo litatekelezeka kwa kuanza kujenga hiyo barabara ili tufikie malengo ya bandari yetu waliyowekeza fedha nyingi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara aliyoisema ya Lyazumbi hadi Kabwe inakwenda kwenye bandari ambayo Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa sana kwa ajili ya biashara kati ya Tanzania na DRC Congo. Naomba nimhakikishie Mbunge kwamba ziko jitihada zinafanyika za kuijenga kwa kiwango cha lami, lakini mpango uliopo sasa hivi ni kipanua ile barabara na kujenga madaraja makubwa na kuiweka kwa kiwango cha changarawe ili magari makubwa yaweze kupita wakati Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya mpango wa kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Ahsante.