Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa Vituo Vya Wazee nchini?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini nilikuwa na maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kutokana na tafiti ambazo zinaendelea inaonyesha kwamba kutakuwa kuna ongezeko kubwa la wazee duniani ikiwemo na Tanzania. Sasa Wizara inajipangaje kuhakikisha inaongeza vituo vya kulelea wazee, aidha kutoka mikoa angalau basi twende hata kwenye Wilaya.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, pamoja na ukarabati ambao unaendelea kwenye hivyo vituo: -

Je, Serikali imejipangaje kuweka vifaa tiba na mahitaji muhimu kwa ajili ya wazee wetu ndani ya hivyo vituo?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bahati kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Bahati na kumpongeza kwa kujali wazee, kwani wazee ni tunu ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake na mwanzo Mheshimiwa Bahati Mbunge, ushauri wake umepokelewa na kuzingatiwa katika mapendekezo ya bajeti katika kipindi cha mwaka 2022/2023. Hata hivyo kila mwaka tunaboresha mahitaji ya wazee kuhakikisha kwamba wanapata mahitaji muhimu kama vile mavazi, chakula, malazi na afya bora. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili ambalo linasema kwamba wazee wapewe msaada wa kisaikolojia. Makazi ya wazee yanaongozwa na kusimamiwa na Maafisa wa Ustawi wa Jamii, wataalam ambao wanatoa msaada wa kisaikolojia kwa wazee wetu. Hata hivyo, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, anawajali sana wazee, anawapenda na kuhakikisha kwamba wanapata haki zao za msingi kila wakati na pale inapohitajika. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa Vituo Vya Wazee nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Wizara hii tayari inaona ina changamoto sana ya kupata fedha kwa ajili ya kundi hili la wazee, lakini bado wazee hawa wana changamoto sana ya uwezo.

Je, Wizara ya ina mkakati gani sasa wa kutumia ile sera ya asilimia 10 kuweza kuwaweka na wazee kupata kama asilimia mbili ili ziwasaidie?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,
WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Issa Mtemvu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Issa tunakuomba kwamba sheria bado zinafanya kazi na zitakapokamilika basi wazee hawa watapewa haki zao na watapewa msaada wa kuongezewa kiasi cha fedha kwa ajili ya mahitaji ya maisha yao. (Makofi)