Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. ERIC J. SHIGONGO Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha Mamlaka kwa Madiwani ya kuzisimamia halmashauri zao pamoja na kuwaazimia Wakurugenzi wa Halmashauri pale linapotokea tatizo kwenye halmashauri husika?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, matatizo ya Wakurugenzi katika halmashauri mbalimbali yanakuwepo na Madiwani wanayaona na saa nyingine wanayaripoti lakini hayafanyiwi kazi mpaka mwenye Mamlaka labda Mheshimiwa Rais apite ndiyo unakuta hatua zinachukuliwa. Mheshimiwa Waziri haoni sasa ni wakati muafaka wa kuhakikisha au kutoa maelekezo kwa wale wenye dhamana wanapoletewa malalamiko kutoka kwa Watumishi au Madiwani wayafanyie kazi na siyo kusubiria mpaka Mheshimiwa Rais apite ndiyo aende kutengua utenguzi wakati matatizo yalikuwa yanaonekana siku nyingi na Mkurugenzi pale ameleta athari kubwa katika ujenzi wa Taifa?Ninakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tunza Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa taratibu za utumishi wa umma, mamlaka za nidhamu za wakurugenzi ziko katika ngazi tofauti, kama nilivyotangulia kusema, ngazi ya Katibu Mkuu Kiongozi, lakini pia Waziri mwenye dhamana. Lakini Waheshimiwa Madiwani wana nafasi na mamlaka ya kutoa taarifa ya changamoto ambazo mkurugenzi anapitia katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, hatua zimekuwa zinachukuliwa kwa wakati, lakini kuchukua hatua ni mchakato kwa sababu, kuna taratibu za uchunguzi, lakini pia kujiridhisha na yale mapungufu yanayoripotiwa kwa mkurugenzi husika, ili kuweza kutenda haki. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba, Serikali itaendelea kufuata taratibu hizo, kufanya uchunguzi kwa wakati, lakini pia, kuchukua hatua ili kutenda haki. Na kuhakikisha kwamba, halmashauri zetu zinakwenda vizuri. Ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. ERIC J. SHIGONGO Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha Mamlaka kwa Madiwani ya kuzisimamia halmashauri zao pamoja na kuwaazimia Wakurugenzi wa Halmashauri pale linapotokea tatizo kwenye halmashauri husika?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi: -

Mheshimiwa Spika, yapata zaidi ya mwaka mmoja sasa mamlaka za Serikali za Mitaa, hususan Madiwani, hawakuweza kupata semina kwa ajili ya kuwajengea uwezo. Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka sasa wa kutoa semina kwa Waheshimiwa Madiwani kote nchini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Serikali kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa mara baada ya Madiwani kuchaguliwa katika mwaka 2020, maelekezo yalitolewa wakurugenzi kuhakikisha Madiwani wanapewa mafunzo kwa taratibu ambazo walijipangia wao katika halmashauri husika. Na mpaka sasa Madiwani wengi wamepata mafunzo, lakini ni kweli kuna baadhi ya halmashauri hazijafanya mafunzo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaendelea kusisitiza kwamba, halmashauri zifanye mipangilio ya ndani ya halmashauri kuhakikisha kwamba, Madiwani wanapata mafunzo hayo, lakini pia, kushirikiana na chuo chetu cha Hombolo cha mafunzo ya Local Government, ili kuhakikisha Madiwani wetu wanajua majukumu yao na mipaka yao ili kuboresha utendaji.

Kwa hiyo, jambo hilo ni endelevu litaendelea kufanyika katika ngazi ya halmashauri, ili kuhakikisha kwamba, utumishi unakwenda vizuri. Ahsante.