Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya mradi mkubwa wa maji toka Ziwa Tanganyika kwenda Mpanda Mjini ili kutatua tatizo la maji?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru sana kupata nafasi ya kuuliza swali, lakini niishukuru sana Wizara ya Maji kupitia kwa Waziri mwenye dhamana wamefanya kazi kubwa sana ya kupeleka huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shida kubwa ya Mkoa wa Katavi tunahitaji kupata chanzo cha uhakika cha maji na chanzo hicho kipo Ziwa Tanganyika ambalo linaweza likatatua tatizo la maji kwa kupeleka huduma kwa Wilaya zote tatu kwa maana ya Wilaya Tanganyika, Wilaya ya Mlele na Wilaya ya Mpanda.

Ni lini Serikali itakuja kutatua tatizo la kupeleka huduma ya maji kuliko kutumia fedha nyingi wanazozitumia kuandaa miradi midogo midogo ambayo haina tija?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyoendelea kufuatilia suala la matumizi ya vyanzo vya uhakika kama Ziwa Tanzanyika. Wizara tumejipanga kuona kwamba maziwa yote tunakwenda kuyatumia tukiamini tunakwenda kutatua tatizo hili la maji na tutamtua ndoo mwanamama kichwani kama ambavyo Mheshimiwa Rais anatutaka na tumshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kutupa fedha Wizara ya Maji. Hivyo, kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi tuko katika kufanya usanifu ili kuona mwaka 2022/2023 matumizi ya maji makuu kama vyanzo vya maji vya uhakika yaweze kufanyika.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya mradi mkubwa wa maji toka Ziwa Tanganyika kwenda Mpanda Mjini ili kutatua tatizo la maji?

Supplementary Question 2

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto hii ya maji inayokuba mji wa Mpanda inafanana sana na changamoto ya maji katika jimbo langu Nanyumbu. Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitumia takribani shilingi bilioni moja kujenga bwawa katika kata ya Maratani ili vijiji vya Lipupu, Maratani. Mchangani A na Malema viweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu haukufanikiwa na Waziri mwenye dhamana alifika katika jimbo langu na kuahidi kutoa kuchimba visima viwili katika kila kijiji hivi nilivyovitaja.

Je, ni lini ahadi hii ya Mheshimiwa Waziri itatekelezwa ili wananchi katika jimbo hili waweze kunufaika na hii ahadi ya Mheshimiwa Waziri? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahya Mhata, Mbunge wa Nanyumbu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ni deni na kwa sababu ameahidi Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Mbunge ninakuhakikishia mgao ujao visima vitakuja kuanza kuchimbwa fedha italetwa.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya mradi mkubwa wa maji toka Ziwa Tanganyika kwenda Mpanda Mjini ili kutatua tatizo la maji?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Katika Mji wa Karatu tuna bodi mbili za maji, Bodi ya KARUWASA inauza maji kwa shilingi 1,700 kwa unit, Bodi ya KAFIWASU inauza maji kwa kwa unit 3500. Sasa ni lini Serikali itaweza kuweka bei ya uwiano katika Jimbo la Karatu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Karatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi gharama za kulipia maji zimekuwa zikifanyiwa marekebisho kila inapobidi kwa kuzingatia uendeshaji wa mradi wa maji wa eneo husika. Hivyo, kwa Jimbo la Karatu nao mchakato unaendelea na tunaamini kabla ya mwaka huu wa fedha kukamilika basi bei hizi zitakuwa rafiki na itakuwa kwa manufaa zaidi ya wananchi.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya mradi mkubwa wa maji toka Ziwa Tanganyika kwenda Mpanda Mjini ili kutatua tatizo la maji?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza nianze kumpongeza Waziri wa Wizara ya Maji pamoja na Naibu kwa kuendelea kutukamilishaia mradi wetu ambao ulikuwa unaitwa ni mradi kichefuchefu wa Wilaya ya Nyang’hwale kutoka Nyamtukuza kwenda Bukwimba kwamba sasa hivi maji hayo tayari tumeanza kuyatumia, lakini kuna tatizo moja maji yale si safi na salama, hawajajenga chujio la maji.

Je, Serikali inatuahidi nini kwenda kujenga hilo chujio la maji ili tuweze kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amar kutoka Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan huu mradi ulikuwa kichefuchefu lakini kwa sasa hivi kama alivyokiri mwenyewe Mheshimiwa Mbunge kwa jitihada zake za ufuatiliaji pamoja na mashirikiano mazuri sasa hivi maji yanatoka. Kuhusiana na chujio ni hatua inayofuata na yenyewe pia tutakuja kukamilisha. Ahsante.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya mradi mkubwa wa maji toka Ziwa Tanganyika kwenda Mpanda Mjini ili kutatua tatizo la maji?

Supplementary Question 5

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutupatia fedha za mradi wa maji katika cha Ibatu.

Swali, kwa kuwa mkandarasi aliyopewa mradi huu kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Kijiji cha Ibatu mpaka sasa ameingia mitini, hakuna shughuli zinazoendelea. Nini mpango wa Serikali na kwa nini Serikali isiweke mkandarasi mwingi au ikafanya kazi wizara yenyewe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga kuhusiana na mradi wa Ibatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tumefuatilia huyu mkandarasi Farbank Company na tayari tumewaagiza mameneja ambao wako pale Njombe wanafanyia kazi. Kwa sasa hivi mkandarasi amerejea kazini siku hizi mbili, lakini tumempa muda wa maangalizo kwa wiki mbili na baada ya hapo basi sheria itafuata mkondo wake.