Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU (K.n.y MHE. LUCY SIMON MAGERELI) aliuliza:- Machimbo ya Madini ya ujenzi yaliyoko Kigamboni yanatoa malighafi muhimu sana inayosaidia ujenzi katika jiji la Dar es Salaam; machimbo haya yanatoa ajira kwa zaidi ya wakazi 6,000 na ndiyo machimbo yenye mwamba laini kwa Mkoa wa Dar es Salaam ukilinganishwa na madini yanayotoka Goba:- (a) Je Serikali haioni kuwa utaratibu wa kuratibu zoezi la kufunga machimbo haya utakosesha ajira kwa watu zaidi ya 6,000? (b) Je, kwa kufunga machimbo hayo, Serikali haioni kuwa inawanyima fursa wananchi wa Dar es Salaam na Pwani kupata madini ya bei nzuri na kuwapunguzia gharama za ujenzi?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na ninashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Swali la kwanza, maeneo haya ambayo yanachimbwa madini yako mbali na makazi ya watu mfano Kimbiji na Chamazi, lakini Serikali imezuia. Je, umbali upi unaotakiwa kiasi kwamba mkafikia kufunga yale machimbo ya maeneo yale?
Swali la pili, madini haya sasa hivi yanatoka katika Mkoa wa Pwani hasa Wilaya ya Mkuranga. Je, kuna tathmini gani mmefanya kwamba machimbo haya sasa hivi hayataleta athari katika maeneo mliyoyapeleka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa maeneo ya Kigamboni kwa sasa yana madini aina ya ujenzi na hasa ya changarawe pamoja na kokoto. Maeneo yanayochimbwa kwa Kigamboni hasa hasa ni maeneo ya Mjimwema pamoja na Kijisu. Hata hivyo, eneo alilotaja la Kimbiji pamoja na Chamazi ni kweli kabisa kuna wachimbaji wadogo wadogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba siyo kweli kwamba tumesimamisha au tumefunga eneo la Kigamboni. Tulipofunga ni eneo la Kunduchi ambapo sasa wachimbaji tena ambao walikuwa kidogo ni haramu wanachimba kuelekea upande wa barabara. Kwa hiyo, pale Kunduchi tulisimamisha tena miaka minne iliyopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimtahadharishe tu Mheshimiwa Mbunge kama nilivyosema, lakini namshukuru kwa kuwaulizia wananchi wa Kigamboni. Taratibu za Sheria ya Madini zinataka uache umbali wa mita 200 kutoka makazi, lakini kadhalika zinataka uache umbali wa mita 100 kutoka vyanzo vya ziwa au bahari kama ferry ya Kigamboni ilivyo na inataka uache umbali wa mita 100 kutoka umbali ambako sasa kiwanja cha ndege kitajengwa au city itajengwa. Sasa kwa Kigamboni kuna eneo kubwa ambalo limeainishwa kwa ajili ya satellite city. Eneo lile tumezingatia Sheria ya Madini kuacha umbali wa mita 100 usiopungua 100 hadi 200.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu sasa kule kigamboni tunatenga eneo rasmi la Mjimwema pamoja na maeneo ya Mkuranga aliyosema ya Visiwasiwa, pamoja na maeneo mengine ya kule Kibaha kwa Mathias na kwa Mfipa. Maeneo hayo tunayatenga kwa ajili ya wananchi wa Dar es Salaam ili wapate maeneo rasmi sasa ya kuchimba madini ya mchanga kwa ajili ya shughuli za ujenzi.
Kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Mbunge, tutakaa pamoja na utendaji wako ili tubainishe maeneo ambayo tutachimba kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Kigamboni.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU (K.n.y MHE. LUCY SIMON MAGERELI) aliuliza:- Machimbo ya Madini ya ujenzi yaliyoko Kigamboni yanatoa malighafi muhimu sana inayosaidia ujenzi katika jiji la Dar es Salaam; machimbo haya yanatoa ajira kwa zaidi ya wakazi 6,000 na ndiyo machimbo yenye mwamba laini kwa Mkoa wa Dar es Salaam ukilinganishwa na madini yanayotoka Goba:- (a) Je Serikali haioni kuwa utaratibu wa kuratibu zoezi la kufunga machimbo haya utakosesha ajira kwa watu zaidi ya 6,000? (b) Je, kwa kufunga machimbo hayo, Serikali haioni kuwa inawanyima fursa wananchi wa Dar es Salaam na Pwani kupata madini ya bei nzuri na kuwapunguzia gharama za ujenzi?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri, kwa sababu Wakala wa Madini (TMAA) wanafanya kazi nzuri sana. Mwaka 2010 na mpaka mwaka 2015 waliweza kukamata madini yenye thamani ya Dola bilioni mbili, lakini pia kwa upande wa shilingi, jumla ya shilingi bilioni 64 zilikamatwa. Je, kwa utaratibu huo huo Serikali ina mpango gani wa kuzuia wachimbaji katika migodi hasa katika usafirishaji wa ule mchanga kwenda kupimwa nje?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kabisa sasa hivi mchanga wote wa concentrate, yaani copper concentrate na hasa unaotoka kwenye mgodi mkubwa wa Bulyanhulu unasafirishwa kwenda ama China ama Japani. Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kwa sababu hapa viwanda vya kuchenjua dhahabu na kuachanisha madini, havijajengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia namwambie Mheshimiwa Ndassa, ni kweli kabisa uwekezaji huu unahitaji mitaji mikubwa; na siyo chini ya Dola 1,000 kuanzisha mradi wa kuchenjua madini hapa nchini. Hata hivyo, kama Serikali, tunatambua sana mchango wa TMAA mamlaka yetu. Kweli kabisa kwa kutumia TMAA imedhibiti asilimia kubwa sana ya upotevu wa madini ambao ulikuwa unatokea hapo nyuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimkumbushe tu Mheshimiwa Ndassa kwamba ni kweli, mwaka 2015, migodi mikubwa kama GGM ililipa shilingi milioni 117 kama dola kwa ajili ya royalty. Hii kutokana na kazi ya TMAA. Pia local levy iliyolipwa ni dola bilioni 4.7 za Marekani, hiyo ni kutokana na udhibiti wa TMAA.
Kwa hiyo, Serikali tunaendelea sasa kuangalia uwezekano wa kuhamasisha wawekezaji wakubwa kuanza sasa kujenga viwanda vya kuchenjua dhahabu hapa nchini. Hata hivyo, itachukua muda, bado Serikali tunalifanyia kazi. Hii ni kwa sababu inahitaji mitaji mikubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Ndassa tumelichukua, tutalifanyia kazi kama ambavyo Mheshimiwa Ndassa tunashirikiana, tunakushukuru sana.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU (K.n.y MHE. LUCY SIMON MAGERELI) aliuliza:- Machimbo ya Madini ya ujenzi yaliyoko Kigamboni yanatoa malighafi muhimu sana inayosaidia ujenzi katika jiji la Dar es Salaam; machimbo haya yanatoa ajira kwa zaidi ya wakazi 6,000 na ndiyo machimbo yenye mwamba laini kwa Mkoa wa Dar es Salaam ukilinganishwa na madini yanayotoka Goba:- (a) Je Serikali haioni kuwa utaratibu wa kuratibu zoezi la kufunga machimbo haya utakosesha ajira kwa watu zaidi ya 6,000? (b) Je, kwa kufunga machimbo hayo, Serikali haioni kuwa inawanyima fursa wananchi wa Dar es Salaam na Pwani kupata madini ya bei nzuri na kuwapunguzia gharama za ujenzi?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Nataka kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mgodi mkuu uliokuwepo katika Mji wa Nzega wa Resolute ulishafungwa na kwenye ripoti ya TMAA inaonyesha Mwekezaji huyu aliondoka na fedha za Halmashauri ya Mji wa Nzega, ten billion shillings ambazo zilikuwa ni service levy: Je, kama Wizara, imefikia wapi kulifuatalia suala hili kuhakikisha haki hii ya wananchi wa Mji wa Nzega inarudi? ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Bashe nakushukuru sana. Kama unatukumbusha kwamba kampuni iliondoka na ten billion sasa umetupa taarifa, tutalifanyia kazi. Mimi na wewe pamoja na wataalamu na vyombo vingine tutashirikiana pamoja, tutalifanyia kazi ili pesa ziweze kurejea. Kwa hiyo, nakushukuru Mheshimiwa Bashe. Ahsante sana.