Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza upembuzi yakinifu wa ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya Manyoni East – Heka – Isseke - Sanza hadi Dodoma?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kutokana na majibu ya Naibu Waziri ni kwamba tangu mwaka 2018 tayari upembuzi yakinifu ulishafanyika.

Swali la kwanza, ni lini sasa Serikali itamalizia kuwalipa fidia wale wananchi wa vijiji vya Ikasi, Sanza na Chicheho ambao wanadai takribani shilingi milioni 60 ili kupisha ujenzi wa lile daraja? (Makofi)

Swali la pili ni kwamba, barabara hii ya kutoka Manyoni - Heka - Sanza mpaka Dodoma inaunganisha Halmashauri Nne; Halmashauri ya Itigi, Halmashauri ya Manyoni, Halmashauri ya Bahi na Halmashauri ya Dodoma Mjini. Kwa mantiki hiyo, hii ni barabara muhimu sana kwa sababu inaleta watu kwenye Makao Makuu ya nchi: Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka kuhakikisha kwamba tunatafuta vyanzo vya fedha ili kufungua hii barabara kukuza Mji wa Dodoma? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY G. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Daraja la Sanza ambalo litakuwa na urefu wa barabara kilomita 14.5 pande zote mbili limeshafanyiwa usanifu na tunavyoongea hivi, kama Wizara tayari tulishapeleka maombi ya fedha Wizara ya Fedha ili tuweze kuwafidia wananchi wote ambao watapisha ujenzi wa barabara. Baada ya hapo, kama Mheshimiwa Mbunge alivyouliza, tayari tumeshatenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa daraja hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ni muhimu kama alivyosema, lakini haitapitika kama daraja lile halitajengwa. Kwa hiyo, Serikali iliona ni busara kwanza tujenge hilo daraja ili kuwe na mawasiliano ya moja kwa moja mwaka mzima. Ndiyo maana kama nilivyosema, kwa umuhimu huo ambao unaunganisha Halmashauri nne alizozitaja, tunaamini baada ya kukamilika daraja usafiri utakuwa na uhakika na baadaye tutaanza kutafuta fedha kujenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza upembuzi yakinifu wa ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya Manyoni East – Heka – Isseke - Sanza hadi Dodoma?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Changamoto iliyopo Manyoni Mashariki ni sawa na changamoto iliyopo kwenye Jimbo la Ngara ambapo Serikali ilituahidi miaka 15 iliyopita kutujengea barabara ya Murugarama, Rulenge na Rusahunga kilomita 85 kwa kiwango cha lami. Kwa masikitiko makubwa miaka 15 iliyopita hakuna kilichofanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua sasa: Ni lini; kwa maana ya dakika, saa, siku, mwezi na mwaka ambapo Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi itaanza kujenga barabara yetu kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Waziri alikuja mwaka 2021, tukaahidi wananchi kwamba barabara hii inaenda kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami. Naomba niambiwe saa, siku, mwezi na mwaka ambapo barabara hii inaanza kujengwa kwa kiwango cha lami.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY G. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndasaba, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilitembelea Jimbo la Ngara na moja ya eneo ambalo tulilitembelea ni hii barabara. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Ngara, pamoja na wananchi wa Ngara kwamba dhamira ya Serikali bado ni kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba bajeti tunayoendelea kuitekeleza tulitenga fedha. Kwa hiyo, mara fedha itakapopatikana, ujenzi wa barabara hii utaanza kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza upembuzi yakinifu wa ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya Manyoni East – Heka – Isseke - Sanza hadi Dodoma?

Supplementary Question 3

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ninashukuru kwa kupewa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Naomba kuuliza, barabara ya kutoka Makete kwenda Mbeya takribani kilomita 97 ni barabara ambayo ilipata kibali cha Mheshimiwa Rais katika barabara 16 ambazo tulisomewa kwenye bajeti. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais ameongeza kutoka kilomita 25 kwenda kilomita 36.5 za kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi dakika hii ninapozungumza ni kwamba bado tumebaki kwenye mchakato wa tendering toka mwezi wa Tisa.

Je, ni lini mchakato wa tenda utakuwa umeisha na barabara hii iweze kuanza kujengwa kwa sababu hili ndilo geti la uchumi kwa Wilaya ya Makete lakini pia kwa Mkoa wa Mbeya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY G. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru kwa kuipongeza Serikali na kwamba barabara yake ni kati ya barabara zilizopata vibali. Hata hivyo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Sanga Mbunge wa Makete, kwa kuwa barabara ilishapata kibali cha Mheshimiwa Rais kwamba iendelee kujengwa, taratibu za manunuzi haziwezi zikakiukwa. Kwa hiyo, kama kuna changamoto ambayo ipo, labda Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa naomba tukutane tuone kuna tatizo gani? Ila ni kweli kwamba ikishapata kibali inatakiwa ujenzi uanze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba baada ya kikao hiki tuone kama kuna changamoto yoyote tofauti na taratibu za kawaida ili kama Wizara tuweze kuzitatua. Ahsante. (Makofi)

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza upembuzi yakinifu wa ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya Manyoni East – Heka – Isseke - Sanza hadi Dodoma?

Supplementary Question 4

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya Morogoro – Njombe – Boda, umuhimu wake inaunganisha Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na ni barabara inayotoa alternative, yaani ni barabara mbadala kwa Mikoa ya Mbeya - Iringa - Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu dogo la nyongeza ni kwamba, barabara hii ina urefu wa kilomita takribani 222 na kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha zimetengwa fedha ili ujenzi uanze walau kilomita 50; na taarifa nilizonazo, imeshapata kibali: Ni lini sasa Wizara itaanza utekelezaji wa barabara hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY G. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema, taratibu za manunuzi zinaendelea na mara zitakapopatikana, basi kilomita hizo zitaanza kujengwa. Siwezi nikasema ni lini na tarehe gani, kwa sababu taratibu za manunuzi zina utaratibu wake, zinaweza zikachukua wiki au mwezi. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii itaanza kujengwa katika kipindi hiki cha bajeti. Ahsante. (Makofi)