Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Vijiji vya Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida ambao wapo ndani ya Kilometa 12 kutoka katika mtandao wa maji ya Ziwa Victoria?

Supplementary Question 1

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza swali moja la nyongeza, nashukuru kwa majibu mazuri sana ya Serikali na niruhusu vile vile kumpongeza kidhati Mheshimiwa Jumaa Aweso Waziri wa Maji kwa kazi nzuri na kubwa anayoifanya katika kutekeleza miradi ya maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi hizi na shukurani hizi vile vile zimfikie Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini kwenye Wizara hii. Ninaamini wale ambao huwa wanapita pita kutoa zile PhD kama za Dkt. Musukuma punde tu watampa Udaktari wa Miradi ya Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa majibu haya mazuri na kwa ahadi ya Serikali ya kufikia Mwezi Agosti, 2022 miradi hii itakamilika je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuambatana na Mheshimiwa Mnzava kufanya ziara punde tu baada ya Bunge hili?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana kaka yangu Jerry Silaa kwa kazi kubwa ambayo anayoifanya, katika Jimbo lake la Ukonga kwa kweli anafanya kazi kubwa na nzuri sana na yenye kuonekana. Lakini kubwa kuhusu suala la kwenda katika Jimbo la Mkoa wa Shinyanga niko tayari baada ya Bunge hili. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Vijiji vya Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida ambao wapo ndani ya Kilometa 12 kutoka katika mtandao wa maji ya Ziwa Victoria?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa nafasi ambayo amekuwa akinipa kujadili miradi ya Wilaya ya Kyerwa.

Swali langu la nyongeza, tunao mradi wa vijiji 57 na mradi huu Mheshimiwa Waziri tumekubaliana unajengwa kwa awamu. Lakini kuna mradi unaotoka Kyerwa, Nyaruzumbula, Nyakatuntu mpaka Kamuli. Mradi huu umechukua muda mrefu ni lini mradi huu utaanza? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote dhati ya moyo nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Kyerwa kwa kazi kubwa na nzuri, ambayo anaifanya na amekuwa msumbufu sana kuhusu suala zima la Jimbo lake liweze kupatiwa huduma ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimuhakikishie utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha. Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan sisi Wizara yetu anatupatia fedha kila mwezi kupitia Mfuko wa Maji na tumetengewa zaidi ya shilingi bilioni 459.2 kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji vijijini. Nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ahadi ambazo tuliziahidi kama Wizara ya Maji tutakwenda kuzitekeleza kwa sababu ya upatikanaji wa fedha ambazo tunapewa na Mheshimiwa Rais. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Vijiji vya Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida ambao wapo ndani ya Kilometa 12 kutoka katika mtandao wa maji ya Ziwa Victoria?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali langu ni dogo kweli na fupi. Sote tunakumbuka wakati wa bajeti hapa Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba ile Miji 26 ya Miradi ya (India) itatekelezeka ndani ya muda. Lakini leo wakati Mheshimiwa Mwanyika anauliza kutaka kujua status ambapo tuna mradi huo wa kutoka Rorya kwenda Tarime Mjini. Tunataka kujua exactly ni lini utakamilika huu mradi? Sio kwamba mtuambie mnasubiri kibali kutoka Exim Bank ni lini utakamilika? Maana yake wananchi wanategemea kupata huduma hii ya maji. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na najua dhati ya moyo namna gani wananchi wako wanataka huduma ya maji. Utekelezaji wa miradi ya maji lazima tukubali upitie taratibu ama michakato mbalimbali ambayo inahitajika. Michakato ya manunuzi sisi kama Wizara ya Maji tumekwishaikamilisha. Tunakamilisha taratibu za manunuzi lazima tupeleke katika Exim Bank ambao wanatupa kibali cha (no objection). Sisi kama Wizara ya Maji tumeshazungumza na wahusika kuna mambo machache ambayo wanayakamilisha na muda si mrefu tutapata kibali kile kwa ajili ya kwenda kutekeleza miradi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge Subira yavuta kheri na kheri itapatikana juu ya utekelezaji wa miradi ya maji. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Vijiji vya Kata za Imasela, Ilola, Lyamidati, Lyabukande na Nyida ambao wapo ndani ya Kilometa 12 kutoka katika mtandao wa maji ya Ziwa Victoria?

Supplementary Question 4

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, afadhali. Swali langu moja kwa Wizara ya Maji. Kampuni ya (DDCA) au Wakala wa Kuchimba Visima nchini Wilaya ya Songwe kupitia TARURA Songwe tumewalipa Shilingi milioni 158 tarehe 24 Novemba, 2021 kwa ajili ya kuchimba visima ili tuweze kupata fedha kwa ajili ya miradi ya maji. Lakini mpaka leo Kampuni hiyo haijachimba visima na nimekuwa nikiwasiliana na CEO wa DDCA anakosa majibu na gari lipo lakini hawajaja bado kuchimba visima katika Wilaya ya Songwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa namuomba Mheshimiwa Waziri ni lini sasa gari hilo litakuja Wilaya ya Songwe kwa sababu Wilaya ya Songwe ni scattered na mvua zimeshaanza kunyesha na kuna baadhi ya maeneo mwezi huu njia ile itakuwa haipitiki kwa sababu ya mvua?

Lakini je, nilikuwa najaribu kumuomba Mheshimiwa Waziri atafute Kampuni nyingine tuweze kuchukua fedha DDCA tuweze kuchimba visima kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maji Songwe.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa wa Songwe kaka yangu Mulugo kwa kazi kubwa na nzuri ambayo unaifanya katika Jimbo lako. Nataka nimuhakikishie nikiri Waheshimiwa Wabunge kama mnakumbuka katika Bunge la Bajeti, mlitoa changamoto juu ya utendaji katika suala zima la Wakala wetu wa Maji na Uchimbaji Visima na Mabwawa (DDCA). Tulikuwa na changamoto ya kiutendaji tumeshafanya mabadiliko hususani Mkurugenzi yule ambaye anasimamia Taasisi ile na muda mfupi mtaona mabadiliko hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara ya Maji hatupo tayari kuona wananchi wa Songwe wanateseka ili hali fedha zimeshalipwa. Nikuombe Mheshimiwa Mbunge tukutane tufanye alternative ya haraka katika kuhakikisha visima vile vinachimbwa na wananchi wanufaike na kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan. (Makofi)