Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la maji safi katika maeneo ya Ngara Mjini pamoja na maeneo ya jirani ya Murukulazo, Nyamiaga, Muruguanza na Buhororo yanayohudumiwa na Mamlaka ya Maji Safi Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa utekelezaji wa miradi ya maji umekuwa ukitumia wakandarasi; na kwa kuwa wakandarasi hawa wanachukua muda mrefu sana kukamilisha miradi hii ya maji; na kwa kuwa yuko mkandarasi alipewa mradi aumalize ndani ya mwaka mmoja na sasa ni mwaka wa sita unakwenda wa saba hajakamilisha mradi huo; na kwa kuwa mimi nia yangu ni kuhakikisha miradi yote ya maji niliyoshiriki kupitisha fedha Bungeni hapa inakamilika ndani ya kipindi cha miaka mitano. Je, Serikali inaweza kuturuhusu kutumia force account kutekeleza Mradi huu wa Maji wa Ngara Mjini na miradi mingine ili miradi hii ikamilike kwa wakati, tena ndani ya kipindi cha miaka mitano? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Ndaisaba Ruhoro, amekuwa ni mfuatiliaji na yeye mwenyewe amekuwa akienda mbele zaidi katika shughuli hizi za miradi ya maji. Hata nilipomtembelea pale jimboni, alionesha jitihada kubwa sana ya kuona kwamba miradi inakamilika.

Mheshimiwa Spika, kutumia force account ni moja ya namna ambavyo tunatekeleza miradi yetu sisi Wizara ya Maji. Hivyo, katika miradi hii ambayo imechukua muda mrefu, tayari miradi zaidi ya 100 tumeweza kuruhusu force account na imekamilika. Hivyo na huu nao tunaupokea, tutahakikisha wenzetu waliopo pale Ngara na wao wanafanya jitihada ya kuona mradi unakamilika. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la maji safi katika maeneo ya Ngara Mjini pamoja na maeneo ya jirani ya Murukulazo, Nyamiaga, Muruguanza na Buhororo yanayohudumiwa na Mamlaka ya Maji Safi Ngara?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nipongeze Wizara ya Maji kwa juhudi zinazoendelea za kuwapatia wananchi wa Jimbo la Kyerwa maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kyerwa tunao Mradi wa Vijiji 57, lakini mradi huu tumekubaliana utajengwa kwa awamu. Hata hivyo, zipo Kata kama Businde, Songa Mbele, Kikukuru, Kitochenkula; kata hizi haziko kwenye awamu hii ya kwanza. Je, Serikali iko tayari angalau hata kuchimba visima ili hawa wananchi ambao wanapata wakati mgumu waweze kupatiwa maji safi na salama wakati wanasubiria mradi mkubwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna mradi mzuri sana pale kwenye Jimbo la Kyerwa na Mheshimiwa Innocent amekuwa bega kwa bega na Wizara. Tumekuwa tukishirikiana naye sana Mheshimiwa Mbunge. Kwa visima kuchimbwa kwa dharura wakati miradi mikubwa ikiendelea na utekelezaji, hii ni moja ya jitihada za Wizara na tumetenga zaidi ya visima 500 kuona kwamba tunavichimba katika maeneo ambayo miradi yake inachukua muda mrefu. Hivyo, kwa kata hizi ambazo ziko pembezoni kwenye Jimbo la Kyerwa nalo tutalifikiria kuona visima vinachimbwa.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la maji safi katika maeneo ya Ngara Mjini pamoja na maeneo ya jirani ya Murukulazo, Nyamiaga, Muruguanza na Buhororo yanayohudumiwa na Mamlaka ya Maji Safi Ngara?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Jimbo la Momba lina vijiji 72 na vitongoji 302. Katika vijiji hivyo, vijiji ambavyo vinapata majisafi na salama ambayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu haviwezi kuzidi 20; isipokuwa tunatumia mbadala wa maji ambayo yametuama kwenye madimbwi na kwenye mito midogo midogo ambapo tunakunywa pamoja na ng’ombe, punda, mbuzi na wanyama wote: -

Je, ni lini Serikali itaona katika vijiji vilivyobaki, watusaidie kutuchimbia visima vya dharura wakati tunaendelea kusubiri miradi mikubwa ya maji ili tuendelee kupata maji safi na salama kama ambavyo binadamu wengine wanapata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester, Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Jimbo la Momba bado lina changamoto ya maji na ni moja ya maeneo ambayo yapo kimkakati katika Wizara na tumetupia jicho la kipekee kabisa pale. Visima ni moja ya miradi ambayo tunakuja kuitekeleza ndani ya Jimbo la Momba. Hivyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, tutakuja kutekeleza wajibu wetu, kwa sababu wananchi wale pia wapo Tanzania. Mheshimiwa Rais mama Samia Suluhu Hassan, amesema wanawake wote lazima tuwatue ndoo kichwani. Mantahofu, tunakuja kufanya kazi Momba. (Makofi)