Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, ni lini tatizo la upungufu wa mabehewa ya abiria na mizigo litatatuliwa katika Kituo cha Mpanda?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nashukuru pia, majibu mazuri yenye kutia matumaini kutoka Serikalini. Hata hivyo, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; nafahamu tulikuwa na behewa la daraja la pili, lakini kwa bahati mbaya behewa hili lilipata ajali ya moto. Ni lini Serikali itaturejeshea huduma hiyo ya behewa la daraja za pili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Kituo cha Mpanda kwa bahati mbaya sana wakati wananchi wakisubiri huduma ya usafiri, jengo lao la kusubiria huduma hiyo halipo. Ni lini Serikali pia, itatusaidia huduma hii muhimu ya jengo la kusubiria abiria? Nakushukuru.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kapufi, kwa faida ya wananchi wa Mpanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua kama tutarejesha daraja la pili katika eneo hili. Naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge maombi haya yamepokelewa. Tutazingatia maombi haya hasa katika mabehewa mapya ambayo yanaendelea kununuliwa angalau huduma hiyo iweze kupatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, tumepokea pia hoja ya pili ya jengo la kusubiri abiria. Hili ni eneo muhimu kwa sababu kama kunakuwa na jua abiria wanahitaji kivuli, lakini pia kama ni wakati wa mvua inapaswa kujikinga. Namwelekeza Mtendaji Mkuu wa TRC atembelee eneo hili ufanywe mpango wa haraka kujenga jengo la kusubiria abiria ili wananchi waweze kupata huduma muhimu. Ahsante.