Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta teknolojia mbadala ili kunusuru afya za wananchi wanaotumia zebaki kwa matumizi mbalimbali?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimwulize maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kwenye jibu la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri amezingatia eneo moja tu la uchimbaji wa dhahabu: Je, Serikali ina mpango gani wa kubadili matumizi ya zebaki inayotumika katika vifaa vya afya ikiwemo katika ujazaji wa jino?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Je, zebaki inayotumika katika huduma za afya kama vile kipima joto kwa maana ya thermometer ama wakati wa kujaza jino kwa maana ya amalgam, ina athari gani zinapotumiwa na binadamu; na je, athari hizo zinapatikana baada ya muda gani? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili mazuri ya Mheshimiwa Mbunge mwenzangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, matumizi ya vitu vyenye mercury kwenye kutibu meno; moja, kwa mercury ipo dozi maalum ambayo kuna mahali inapofikia ndiyo inaweza kuleta athari. Hata hivyo ni kweli kwamba kuna baadhi ya watu wakizibwa meno kwa kutumia amalgam hiyo yenye mercury, wengine wanapata allergy.

Kwa hiyo, wakati mwingine watu wanaweza wakafikiri ni madhara ya mercury, lakini ni allergy kwa sababu kuna watu wenye allergy na baadhi ya mambo. Mpaka sasa, kwa kutibu meno, inatumika na haijaonesha madhara ambayo unadhani yanatokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna options mbalimbali za kutumia na utafiti unaendelea kuona namna ya kupata kitu chenye strength ile ile ambayo amalgam ilikuwa inafanya ili waweze kuitoa, lakini kwa kweli mpaka sasa kitiba haina shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, amezungumzia thermometer na vifaa vingine vya tiba ambavyo vina mercury, tunafanyaje? Kikubwa ambacho mpaka sasa hata kwenye madini kinafanyika, kwenye vifaa vyote vya tiba na hata dawa, suala kubwa hapa, ni kwa namna gani unafanya disposing na control mechanism zinavyohaibika na zile thermometer unazi-dispose kwa namna gani? Ndiyo maana kuna utaratibu maalum wa namna ya ku-dispose vifaa tiba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutaendelea na utaratibu wa kuhakikisha thermometer na vifaa vingine vyote vinavyotumia mercury vinakuwa under control na vikiharibika ile disposing mechanism inafuatwa ili kutunza mazingira na kutunza afya ya binadamu. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta teknolojia mbadala ili kunusuru afya za wananchi wanaotumia zebaki kwa matumizi mbalimbali?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matumizi ya zebaki, hasa Kanda ya Ziwa, sehemu ambazo wanachimba madini imekuwa ikisababisha ongezeko la wagonjwa wa Kansa ya Shingo ya Uzazi: Je, Serikali imeshafanya utafiti kuthibitisha kwamba zebaki ndiyo chanzo cha ongezeko la magonjwa ya kansa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba hata ukienda Ocean Road imeonekana kwamba wagonjwa wengi wenye matatizo ya kansa wanatokea Kanda ya Ziwa. Hayati Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Magufuli aliwahi kuagiza ufanyike utafiti ambao bado majibu yake hayajaja ili kuthibitisha nini hasa chanzo cha tatizo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachofanyika kwa sasa ni kwamba kwanza kuna sababu nyingi ambazo zinasababisha kansa ya kizazi. Kwa hiyo, hatuwezi kusema specifically ni hilo. Kikubwa, tunashirikina na Wizara ya Madini kupitia taasisi yake kuhakikisha sasa wanapochenjua madini, wale wachimbaji wadogo na wakubwa kunakuwepo na control ya kutosha kuhakikisha kwamba haiendi kwenye mazingira na vilevile haiendi kufika maeneo ambayo binadamu wanatumia maji na vitu vingine. Hilo ndiyo tunaendelea nalo kwa sasa.