Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Chuo cha VETA katika Wilaya ya Handeni?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kwenye swali langu la msingi. Kwa kuwa Serikali imewaelekeza wananchi wa Handeni kuendelea kutumia Chuo cha Wananchi cha Maendeleo kilichopo Handeni wakati tukingoja ujenzi wa Chuo cha VETA katika Wilaya yetu: Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa vya kufundishia kwenye chuo hiki cha FDC kwa maana ya vitabu, mitambo na mashine? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukiendeleza chuo hiki cha FDC kilichopo ili kifikie kuwa katika hadhi ya Chuo cha VETA? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjii kama ifuaavyo: -

Mheshimiwa Spika, tarehe 10/10/2021 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliubainishia Umma kwamba tumepata fedha zile ambazo zinatokana na namna gani tunaweza kuondoa changamoto ya Uviko 19.

Katika fedha hizo, jumla ya shilingi bilioni 6.8 zimetengwa kwa ajili ya kupeleka vifaa pamoja na mitambo ikiwemo na vitabu katika vyuo 34 vya FDC. Miongoni mwa vyuo hivyo 34, kimojawapo ni hiki chuo cha Handeni.

Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi kwanza Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imejipanga vizuri, tunakwenda kupeleka vifaa pale ili kuhakikisha tunaboresha mazingira ya ufundishaji pamoja na vifaa ili vijana wetu waweze kupata taaluma yao katika eneo lile. (Makofi)

Katika eneo la pili anazungumzia namna gani tunaweza kuboresha chuo kile labda kiweze kuwa na hadhi ya VETA. Vyuo hivi vya FDC vilianzishwa kwa mkakati maalum wa kuhakikisha tunapeleka maendeleo katika maeneo yale. Hatuna sababu ya kuvibadilisha vyuo hivi kwenda kuwa VETA, ingawa bado vinatoa mafunzo haya ya VETA.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa vile Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba tunakwenda kujenga VETA katika kila Wilaya katika mipango yetu ya baadaye, chuo hiki tutaendelea kukiimarisha ili kiweze kutoa mafunzo na tija katika eneo hili ambalo limekusudiwa na Serikali wakati Serikali inajipanga kutafuta Chuo cha VETA katika eneo hilo. Ahsante sana. (Makofi)