Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italifuta shamba la Mwakinyumbi Estate lililotelekezwa kwa muda mrefu na kuwapa wananchi wa Hale na maeneo jirani ili waweze kufanya shughuli za kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru pamoja na majibu mazuri sana kutoka kwa Mheshimiwa Waziri naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza. Jambo la kwanza jambo hili limekuwa ni la muda mrefu sana na Mheshimiwa Waziri atakuwa shahidi wa jambo hilo pamoja na ahadi hii nzuri ulioitoa Mheshimiwa Waziri ningependa kujua uko tayari baada ya Bunge hili uongozane na mimi kwenda kuzungumza na wananchi wa Hale uwape matumaini ya kuharakisha jambo hili ili wapate ardhi kwa ajili ya kufanya shughuli zao za kilimo?

Mheshimiwa Spika, Swali la pili Wilaya ya Korogwe sehemu kubwa ya ardhi yake ni mashamba makubwa ya wawekezaji wa chai na wawekezaji wa mkonge na maendelezo yake hayaridhishi sana na jambo hili limefanya wananchi wetu kukosa maeneo ya kufanya shughuli za kilimo hasa vijana wamekosa maeneo ya kujiajiri. Je, Serikali iko tayari kukaa pamoja na wawekezaji hawa pamoja na umuhimu wa uwekezaji wao kwenye maeneo haya lakini tufanye mazungumzo ya kuona namna gani ya kumega maeneo kwa ajili ya kuwapa vijiji ili wananchi wapate sehemu ya kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo suala la kilimo? (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Mnzava Mbunge kijana machachari wa Korogwe kama ifuatavyo: -

Kuhusu swali la kwanza, kwenda anauzoefu anajua akiniita naenda tulishaenda na nitakuja na huko na nitafanya yale ambayo tulifanya sehemu nyingine ambazo ulinipeleka. Kwa hiyo, wananchi wasiwe na wasiwasi Mheshimiwa Mnzava akinihitaji kwangu mimi ni agizo nakwenda tu na Waheshimiwa Wabunge wote kama kuna matatizo kama haya mkiniambia ndiyo inanisaidia kupata kazi maana mkinituma ndiyo napata uhalali wa kuja. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mnzava nakuja. (Makofi)

Swali lake la pili; ni kweli una mashamba mengi na ni kweli kwamba kwenye mashamba mengi najua wakati ule wenye mashamba wanapomiliki hasa Kanda hii ya Kaskazini wananchi walikuwa wachache sasa wananchi wameongezeka sana. Kwa hiyo nataka ukitoka hapa muulize Mheshimiwa Mbunge wa Same hapa Mama Kilango akufundishe namna alivyofanya na mpaka na mimi nikaenda kule na moja ya shamba wananchi wakarudishiwa ekari 300. Kwa hiyo uwezekano huo upo kwa sababu mifano tunayo tutakaa na wenye mashamba wanajua kabisa wanataka kuishi vizuri na majirani wao, hawakatai.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge aniorodheshee hao wenye mashamba ni watu gani halafu tupange ratiba tuzungumze nao wanajua hali halisi na wenyewe wanataka kuishi vizuri na wananchi wanaowazunguka kwa hiyo hilo tutafanya, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italifuta shamba la Mwakinyumbi Estate lililotelekezwa kwa muda mrefu na kuwapa wananchi wa Hale na maeneo jirani ili waweze kufanya shughuli za kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nilipenda kujua tu kwamba Waziri anayezungumza hapa ndiyo mwenye mamlaka ya kugawa mipaka ilivyo kati ya wananchi na wanyamapori. Sasa nimuombe Mheshimiwa Lukuvi mpaka wa vijiji kama 11 hivi vya Jimbo la Bunda ukianzia mipaka ile ya Honyali, Maliwanda ukienda Mgeta mpaka Tingirima mpaka wao ni Mto Rubana ndiyo mto asili unaotumiwa na wananchi wa maeneo yale lakini mpaka uko katikati ya Mto Rubana. Ni lini Waziri ataenda pale kutenganisha mita 500 za wanyamapori na mita 500 za wananchi?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Getere kwanza nitamuona hapa hapa anipe ufafanuzi vizuri zaidi lakini pia ninao uwezo wa kwenda Mkoa wa Mara kwenda kuzungumza nae na viongozi wengine ili tujue hilo kwa sababu hata vijiji huwa vinaanzishwa kwa mfumo ule ule unaofanywa na Wilaya na Mikoa.

Mapendekezo ya kuanzisha vijiji huwa yanaanzia Wilayani yanakuja mkoani mwishoni Ofisi ya Rais, TAMISEMI ndiyo inaidhinisha ambayo iko chini ya Ofisi ya Rais na kutoa GN maandishi yanayoainisha kila Kijiji na mipaka yake iko namna gani. Jukumu langu mimi siyo kuanzisha mipaka ya vijiji vipya Wizara ya Ardhi hatuanzishi mipaka, tunasuluhisha lakini kwa kutafsiri ardhini GN za mipaka zilizoainishwa na mamlaka inayohusika.

Kwa sababu hiyo, nitakwenda huko kwenda kuwasaidia wananchi wa vijiji hivyo kuainisha mipaka iliyopendekezwa au iliyoamuliwa kuaanzisha vijiji hivyo kwa mujibu wa mapendekezo ya mamlaka. Lakini pia hiyo migogoro kati ya buffer zone na ardhi za vijiji nitapenda kumsikia lakini tutakwenda huko hivi karibuni tulikwenda Serengeti nako kulikuwa na migogoro ya buffer zone vijiji vilivyoanzishwa hifadhi ya Serikali ilichukua mita 500 za ardhi ya vijiji ikafanya buffer zone.

Rais wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameagiza ili kuondoa taharuki, ardhi ile ambayo Serengeti walichukua kuanzia Mkoa wa Mara kule Tarime mpaka Serengeti mita 500 kwenye ardhi za vijiji zirudishwe kwenye vijiji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumetekeleza maelekezo hayo mita 500, 500 zilizokuwa kwenye buffer zone ya Hifadhi ya Serengeti zimerudishwa kwenye vijiji na hivyo Serengeti sasa kama wanahitaji buffer zone watarudi ndani ya hifadhi yao. Lakini zile za vijiji zimerudishwa tayari, kwa hiyo hili nalo tutakwenda kujifunza nature ya mgogoro huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Rais wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameagiza, ili kuondoa taharuki, ardhi ile ambayo Serengeti walichukua kuanzia Mkoa wa Mara kule Tarime mpaka Serengeti, mita 500, kwenye ardhi za vijiji zirudishwe kwenye vijiji.

Mheshimiwa Spika, tumetekeleza maelekezo hayo, mita mia tano mia tano zilizokuwa kwenye buffer zone ya Hifadhi ya Serengeti zimerudishwa kwenye vijiji na hivyo, Serengeti sasa kama wanahitaji buffer zone watarudi ndani ya hifadhi yao, lakini zile za vijiji zimerudishwa tayari. Kwa hiyo, hili nalo tutakwenda kujifunza nature ya mgogoro huu.