Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro uliopo mpakani mwa Wilaya ya Kishapu Kata ya Mwamalasa Kijiji cha Magalata na Wilaya ya Iramba?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, mimi naomba nishukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza siyo peke yake mgogoro huu umekuwepo nyakati za kiangazi mgogoro huu umekuwepo nyakati zote masika na kiangazi na sasa hivi tunapozungumza habari za shughuli za kilimo maana yake zinapoenda kutekelezwa na wananchi wa maeneo haya kipindi hiki pia mgogoro huu unaweza ukaibuka. Kwa hiyo siyo sahihi kwamba ni nyakati za kiangazi peke yake na hata masika kwa sababu shughuli za kibinadamu zinafanyika nyakati zote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mgogoro huu umekuwa ukichangia sehemu kubwa sana uvunjifu wa amani wa wananchi wetu nataka nipate commitment ya kutosha ya Serikali kwamba ni lini sasa watakwenda kutatua mgogoro huu ikiwa ni pamoja na kuijumlisha Wizara ya Ardhi kuhakikisha wanaenda kuainisha na kuweka beacon ili mipaka ya maeneo ya kiutawala yaweze kuainishwa sawasawa. (Makofi)

Swali la pili Wizara ya Ardhi mwaka 2019 walifika katika eneo hili la mgogoro na kwa bahati mbaya kwa sababu walifika nyakati za masika maji yalikuwa yametapakaa katika maeneo hayo ya mipaka na kwa hali hiyo walishindwa kufanya suala zima la kuainisha lakini pia na kuweka beacon na waliahidi wangeweza kutekeleza na kuumaliza mgogoro huu uliokuwepo katika maeneo haya ya Iramba na Kishapu.

Je, ni lini Wizara ya Ardhi watafika na kuhakikisha wanaweka beacon kuainisha maeneo ya kiutawala lakini na kuweka beacon ili mgogoro huu sasa usiendelee na wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo. (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI naomba nichangie kidogo nyongeza ya swali hili, nafikiri nilikutana na huyu Mheshimiwa Mbunge nalijua hili tatizo lakini mimi sijawahi kushiriki vizuri, lakini niliwaahidi kwamba tungeweza tukakutana na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI tukazungumza kwanza kiutawala kati ya Wakuu wa Mikoa hawa wawili lakini mimi Wizara yangu kazi ya kutafsiri mipaka ndiyo kazi yake kwa GN zilizoandikwa.

Mheshimiwa Spika, hivyo nataka kumuahidi Mheshimiwa Mbunge nitalisimamia mwenyewe hilo la kuweka mipaka ili wananchi wa Wilaya hizi waweze kujua mipaka yao iliyoainishwa na mwenye mamlaka kwa sababu mamlaka ya kugawa mipaka ya utawala ni ya Mheshimiwa Rais, sasa wakati mwingine huwa inatokea wananchi wanasema nilikuwa hapa nilikuwa hapa nawakumbusha tu mwenye mamlaka ya kugawa mipaka ya utawala ni Mheshimiwa Rais na mipaka hii huwa inaandikwa kwenye Kanuni zinaitwa GN na GN tunazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mbunge wananchi waambie Wizara yangu itakuja kutafsiri ardhini mipaka iliyoainishwa kama nia ya Mheshimiwa Rais ya kupanga na kuunda hizo Wilaya mipaka ya ardhini itakuja kuainishwa na kutafsiriwa na Wizara yangu na jambo hili litafanyika mara moja. (Makofi)