Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini tatizo la maji litakwisha katika Mji Mdogo wa Mikumi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, naamini kuwa Wizara ya Maji inafanya kazi sana kwa jitihada zao, licha ya jitihada hizo, lakini bado watu wanataka maji. Kata ya Ruaha ambayo iko kwenye Jimbo hilohilo la Mikumi, Wilaya ya Kilosa waliahidiwa na Mheshimiwa Rais Awamu ya Tano kupatiwa maji. Kwa hiyo, nauliza ni lini watapatiwa maji? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kata ya Lukobe ambayo iko Manispaa ya Morogoro tulitembelea kamati yangu na wananchi wakaahidiwa kuwa watapariwa maji kuanzia mwezi wa nane hilo tanki la mguru wa ndege, lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea tanki hilo halijawahi kupata maji na sasa ni mwezi wa 11 na ahadi ilikuwa mwezi wa nane, wananchi wanakunywa maji ya visima ambayo ni maji yasiyo Safi na salama. Na wamenituma wanauliza ni lini watapatiwa hayo maji kupitia kwenye tanki hilo la Mguu wa Ndege? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kipekee nipende kumshukuru Mheshimiwa Mama yangu Dkt.Christine Ishengoma kwa namna ambavyo anaendelea kufuatilia suala hili la maji katika maeneo ya Mkoa wa Morogoro na nikushukuru sana Mheshimiwa Christine Ishengoma kwa ushirikiano ambao umeendelea kutupa sisi Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Spika, kwa swali la kwanza Kata ya Ruaha; tayari RUWASA wameshafanya taratibu zote na sasa hivi wametangaza ili tuweze kumpata mkandarasi. Na tunaamini kwa kasi ambayo tunaenda nayo watu wa Ruaha nao watakwenda kunufaika muda si mrefu.

Mheshimiwa Spika, kwa eneo hili la mguru wa ndege wakati wa ziara na mimi nilikuwepo. Mheshimiwa Dkt. Christine kama ambavyo tumekuwa tukiwasiliana kwenye suala hili, lile tanki hata ukipita pale barabarani unaliona kubwa, zuri, lenye ubora kabisa limeshakamilika na sasa hivi tunaingia kwenye awamu sasa ya usambazaji na tayari Wizara tunapeleka fedha kwenye mgawo huu unaokuja kwa lengo la kuona sasa maji yanakwenda kuwafikia wananchi wote wa eneo la Lukobe. Ahsante.