Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya samaki katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika hususani Kata ya Kala Mpasa, Wampambe, Kizimbi na Naninde ili wavuvi wapate maeneo ya kuuzia samaki badala ya kulazimika kwenda kuuza nchi za jirani za Zambia, Congo na Burundi?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Uchumi wa blue unafanana na mazingira mazuri kabisa sawa sawa na Ziwa Tanganyika. Je, Serikali ina mpango gani kama inavyofanya kwenye mazingira ya Bahari ya Hindi rasilimali zinavyopatikana baharini, vivyo hivyo na rasilimali zinapatikana Ziwa Tanganyika. Ni lini Serikali mnakuja na mkakati maalum swali namba moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali namba mbili dagaa Ziwa Tanganyika ni zao la kipekee ambalo ndio linasababisha uchumi wa Mikoa mitatu Kigoma, Rukwa na Tanganyika. Serikali ina mpango gani na zao hili na pia kwa sababu linavuliwa ndani ya Mikoa mitatu, libadilishwe jina sio dagaa wa Kigoma waitwe dagaa wa Ziwa Tanganyika ili kuweza kutangaza Ziwa Tanganyika? Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua kwanza fursa hii, kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbogo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza naomba kwa namna ya kipekee nimpongeze yeye na Wabunge wote wa Mkoa wa Kigoma, Katavi na Rukwa kwa kuona umuhimu wa Ziwa Tanganyika na mazao yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan, moja ya mkakati ni hili la uchumi wa blue na ni kipaumbele kama Taifa letu na ndio maana katika bajeti ya mwaka huu, Serikali ya Awamu ya Sita imeweka jumla ya kiasi cha shilingi milioni 800. Kwa kusudio la kwanza ni kuhakikisha kwamba tunafanya stock assessment. Ziwa Tanganyika halijawahi kufanyiwa stock assessment kwa mara ya kwanza sasa tunakwenda kufanya stock assessment, ya kujua ni kiasi gani cha Samaki migebuka na dagaa tulionao katika eneo lile. Hii itatusaidia sana kwenye mkakati wa uchumi wa blue, ili kuweza kuvutia uwekezaji na watu kuweza kujua kwamba akiweka fedha yake itakwenda kumlipa kwa kiasi gani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini hili la pili la ushauri la kwa nini dagaa hawa wasiitwe dagaa wa Ziwa Tanganyika? Nataka nimhakikishie yeye na Waheshimiwa Wabunge wote tumeuchukua ushauri huu. Isipokuwa kibiashara wewe unafahamu ya kwamba katika marketing strategy dagaa hili limetambulika kwa miaka mingi sana kama dagaa la Kigoma.

Kwa hiyo, ikiwapendeza sisi tutakaa nao tutashauriana nao badala ya kuwa dagaa la Kigoma, tutasema kwamba liitwe dagaa la Tanganyika. Kwa dhumuni jema lile la kwamba wanavuliwa kwenye Mikoa yote mitatu, Rukwa, Katavi na Kigoma kwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na dagaa hizi ni mali sana hazijawahi kushuka bei hivi sasa inauzwa mpaka shilingi 30,000 kwa kilo na haijawahi kushuka chini ya shilingi 20,000. Ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya samaki katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika hususani Kata ya Kala Mpasa, Wampambe, Kizimbi na Naninde ili wavuvi wapate maeneo ya kuuzia samaki badala ya kulazimika kwenda kuuza nchi za jirani za Zambia, Congo na Burundi?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Ziwa Tanganyika linatumika zaidi ya nchi moja kwa maana ya Tanzania kuna Congo, Burundi na nchi nyingine. Lakini dagaa wengi wanapatikana Ziwa Tanganyika upande wa Tanzania na sheria ambazo mlizitunga pamoja na Kanuni, zinawa-guide wavuvi wa Tanzania wavue usiku wakati dagaa wengi wanapatikana mchana. Kwa hiyo, ni muda muafaka sasa wa Wizara ya Uvuvi hawaoni kwamba, kuendelea kutumia hizo sheria ambazo zinawakandamiza wavuvi wa Tanzania na kuwapa faida nchi nyingine waachane nazo? (Makofi)

SPIKA: Kwa hiyo, kule Congo na wapi wanavua mchana?

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, ndio wanavua mchana.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tumepokea malalamiko na tumepokea mapendekezo ya wavuvi wote wa Ziwa Tanganyika na hivi sasa, Wizara inafanyia kazi mapendekezo haya yote yaliyotolewa na wavuvi. Lakini naomba kwa ruhusa yako kwa sekunde moja. Dagaa ni aina tofauti katika miongoni mwa aina za samaki tulizonazo, mle katika Ziwa Tanganyika tunao dagaa, tunao migebuka. Lakini Ziwa Tanganyika ni maarufu zaidi kwa samaki wa marembo wanaouzwa duniani kote na tunapata mapato makubwa sana kama Taifa.

Mheshimiwa Spika, kwa nini usiku? Tunaweka sayansi inayoelekeza tunapovua usiku dagaa tunaweka light attraction, ni dagaa pekeyake ndiye anayeweza kuvutwa na mwanga wa taa. Migebuka havutwi, samaki wa marembo havutwi, sangara havutwi anayevutwa ni dagaa peke yake.

Sasa, tunafanya vile kuwavuta dagaa ambao wanakuja katika mtindo wa makundi kwa maana sculling, ili kuwaepusha kuchukua samaki wa aina nyingine. Sasa hawa wanaovua mchana, nina hakika siwezi kuzungumzia nchi zingine, lakini hapo nimezungumza from scientific point of view.

Mheshimiwa Spika, ni kwa nini msingi wa kwa nini tunasema usiku na dagaa asivuliwe mchana, ukimvua mchana utavua na migebuka, utavua na samaki wengine wasiohitajika. Kwa sababu, kila leseni anayopewa mvuvi anapewa kwa kusudio maalum. Lakini hiyo tumeichukua hoja hii na sisi kama wataalam tupo katika harakati za kuangalia, ili tuweze kuendana na mahitaji ya wavuvi wetu waweze kunufaika na rasilimali hii. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya samaki katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika hususani Kata ya Kala Mpasa, Wampambe, Kizimbi na Naninde ili wavuvi wapate maeneo ya kuuzia samaki badala ya kulazimika kwenda kuuza nchi za jirani za Zambia, Congo na Burundi?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Awali ya yote naomba niipongeze Serikali na Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kutupatia vifaa boti katika Jimbo letu la Mchinga. Sambamba na kutupatia mashine katika Jimbo letu la Mchinga na sasa hivi wako kwenye mchakato wa kutupatia hiyo boti. Halikadhalika wako kwenye mchakato mwingine wa kutujengea eneo ambalo wavuvi hawa wadogo wadogo hasa katika Jimbo langu la Mchinga, watajenga mwalo ili wavuvi wote wawe na sehemu ya uhakika ya kuuzia bidhaa zao kutoka kwenye Bahari yetu ya Hindi. Swali langu ni hili lifuatalo: - (Makofi)

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huu wa mwalo katika Jimbo langu la Mchinga na hasa Kata ya Mchinga? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mama yangu Salma Rashid Kikwete, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana ni ukweli kwamba Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan imepeleka mashine za kutosha. Lakini vile vile na Kamba ambazo zilikuwa ni maombi ya kwake yeye mwenyewe Mbunge wa Jimbo la Mchinga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na katika hilo pia vile vile Serikali ya Awamu ya Sita imetenga jumla ya shilingi milioni 800, kwa ajili ya kujenga Mwalo na sasa hivi tupo katika hatua tayari kwa pamoja kwa kushirikiana na wananchi wa Mchinga, tumeshachagua eneo litakalokwenda kujengwa ule mwalo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini sasa tupo katika michoro na baadaye kupata BOQ ambapo jumla ya kiasi cha fedha kisichopungua Shilingi milioni 800 zimetengwa kufanya kazi hiyo. Ninaamini kazi hiyo itakapokamilika ndani ya mwaka huu wa fedha itawanufaisha wavuvi wa eneo hili la Mchinga na wengine katika Pwani ya Bahari ya Hindi. Ahsante sana. (Makofi)