Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha mpaka wa Kirongwe kwa kujenga One Border Post ili kuimarisha na kuongeza mapato ya Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi, lakini nishukuru pia na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Naomba niulize maswali mawili ya nyogeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, ucheleweshaji wa umuhimu wa eneo la mpaka wa Kirongwe si tu ina umuhimu kwa Wilaya na Halmashauri ya Rorya lakini pia ina umuhimu pia kwa Serikali kwa ujumla wake kwa sababu ya sensitivity ya eneo lenyewe lilivyo kati ya mpaka wa Tanzania na Kenya. Lakini mpaka sasa hakuna kifaa chochote vile vifaa tofauti naweza nikasema na counter book na kalamu kwa upande wa Tanzania na Kamba peke yake. Je Serikali haioni kuna umuhimu sasa kipindi ambacho tunakwenda kwenye bajeti ya utekelezaji wa mwaka huu kuweka vifaa vya kisasa ili kuimarisha mpaka ule lakini kudhibiti mapato yanayopotea kwenye eneo lile?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili kwa kuwa ucheleweshaji wa eneo hili linaathiri pia mapato ya halmashauri ndani ya Jimbo letu la Rorya. Je Serikali haioni kuna umuhimu, pamoja na maboresho yanayokwenda ya nyumba za watumishi, kuweka soko kubwa la kimataifa ambalo litakuwa ni sehemu ya fursa kati ya wananchi wa Wilaya yangu ya Rorya pamoja na wananchi wa upande wa pili wa Kenya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jafari Chege Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hoja zake zote mbili ni za msingi sana. Hoja ya kuhakikisha kwamba tunatafuta vifaa vya kutosha ili kuwezesha huduma katika mpaka wa Kirongwe pamoja na ujenzi wa soko ni hija za msingi. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge atupe muda Serikali wakati tunakamilisha, kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, hatua za ujenzi wa nyumba kwa bajeti ya mwaka huu basi na hili la vifaa tulichukue na hili la soko lenyewe Serikali imelipokea itaangalia pale hali itakaporuhusu ili liweze kufanyiwa kazi.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha mpaka wa Kirongwe kwa kujenga One Border Post ili kuimarisha na kuongeza mapato ya Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mwezi wa nane mwaka huu nikiwa na Kamati ya Bajeti tulipata nafasi ya kutembelea border post ya Namanga. Lakini katika jambo ambalo lilitushangaza ni kwamba border post ile haikuwa na Cargo scanner; na katika kuuliza tukaambiwa kuna border post nyingine vilevile hazina cargo scanner, jambo ambalo linahatarisha mapato ya Serikali vilevile kuchelewesha upitishaji wa mizigo.

Mheshimiwa Spika, ningeomba Serikali itueleze ni nini msimamo wa Serikali katika kuhakikisha border post zote kubwa zinapata cargo scanners ili kuweza kuondokana na matatizo yaliyopo? Ahsante, nakushukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abbas Tarimba Mbunge wa Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko katika mpango wa miaka mitano kuanzia mwaka 2020/2021 mpaka mwaka 2024/2025, ambapo mpango huu unalenga pamoja na mambo mengine kuimarisha ama kuboresha utendaji kazi wa vituo vyetu vyote tisa vya one stop border kote nchini; ikiwemo kuweza kuipatia vifaa, watumishi, kuwajengea uwezo watumishi, kuweza kuviimarisha kwa njia mbalimbali. Kwa hiyo mpango huu utakapokuwa umekamilika hii changamoto za scanner na changamoto za vitendea kazi vingine pamoja na mifumo ya TEHAMA kwa ujumla wake, maabara nakadhalika na nyingine ambazo nimezitaja zitakuwa zimepatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, nimwombe avute subra wakati kipindi cha utekelezaji wa mkakati huu utakapokamilika ni imani yangu kwamba tatizo la scanner Namanga na maeneo mengine litakuwa imepatiwa ufumbuzi.