Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU (K. n. y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA) aliuliza:- Njia pekee ya kuinua uchumi wa Taifa linalotegemea kilimo kwa sehemu kubwa ni pamoja na kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo na mifugo; (a) Serikali ina Mkakati gani wa kujenga viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo na mifugo kwenye Mikoa yote ya kilimo na yenye mifugo mingi nchini; (b) Wafanyabiashara wa mazao ya kilimo na mifugo wanafanya udanganyifu mkubwa wa kujaza magunia lumbesa, kutanua madebe, pia kupima mifugo kwa macho na kwa kupapasa hali inayowaumiza na kuwapa hasara kubwa wakulima. Je, kwa nini Serikali inashindwa kuweka matumizi ya mizani rasmi kwa mazao hapa nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Waziri wa Wiwanda, ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miaka ya karibuni viwanda vingi vilibinafsishwa na kuuzwa, vikiwemo viwanda vya mazao ya kilimo na mifugo na kubadilishwa matumizi yake.
Je, Serikali iko tayari kuhakikisha madhumuni ya awali yanatekelezwa kama ilivyoainishwa uko mwanzo?
Swali la pili, kwa vile suala la vipimo vya kienyeji, kama rumbesa na ndoo, maarufu kama Msumbiji limekuwa likilalamikiwa kwa muda mrefu; Je, Serikali haioni kuna haja ya kutoa tamko ni lini hasa wakala wa vipimo na mamlaka za Serikali za Mitaa zitaanzisha hivyo vituo? Ahsante.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, dhana ya kujenga uchumi wa viwanda, inaendana na utaratibu wa kuhakikisha viwanda vyote vile vilivyobinaifishwa vinarudi kufanya kazi. Wale ambao walipewa viwanda hawakuuziwa walipewa, kwa sababu walilipa kishika uchumba tu, hawakulipa fedha kamili ya kununua kiwanda, ni kwamba wanapaswa wavirudishe. Na napenda nitoe taarifa kwa Bunge lako Tukufu kwamba wanaitikia vizuri na wote watakuja kuendesha viwanda kwa misingi ambayo walikusudia. Atakayeshindwa atanyang‟anywa na atapewa Mtanzania mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mkapa, alikuwa na dhamira safi ya kuwapa Watanzania ili kusudi watoke, wajijenge kiuchumi lakini dhamira yake watu wakaitumia vibaya ndiyo hayo wakaenda kutumia viwanda ambavyo havikukusudiwa.
Mhesheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, vipimo aina ya rumbesa, Msumbiji, na wengine wanaita badimanyaira. Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI, wameshatoa maelekezo na mtakuta hata njiani, mimi napokea simu nyingi, watu wengi wanakamatwa. Uuzaji wa mazao unakuwa na vituo maalum na Maafisa Ugavi na Watendaji wa Kata, ni moja ya jukumu lao kufika maeneo yale na mnunuzi yeyote hakikisha unapima kilo zisizidi 100. Nitafanya jitihada zaidi kuhakikisha kwamba tunawapelekea mizani kadri tutakapopata uwezo wa kuweza kununua mizani hiyo ili kusudi wananchi pamoja na kupima usawa wa gunia lakini wawe na uhakika kwamba ni kilo 100 tu, wasiwanyonye wauzaji.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU (K. n. y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA) aliuliza:- Njia pekee ya kuinua uchumi wa Taifa linalotegemea kilimo kwa sehemu kubwa ni pamoja na kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo na mifugo; (a) Serikali ina Mkakati gani wa kujenga viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo na mifugo kwenye Mikoa yote ya kilimo na yenye mifugo mingi nchini; (b) Wafanyabiashara wa mazao ya kilimo na mifugo wanafanya udanganyifu mkubwa wa kujaza magunia lumbesa, kutanua madebe, pia kupima mifugo kwa macho na kwa kupapasa hali inayowaumiza na kuwapa hasara kubwa wakulima. Je, kwa nini Serikali inashindwa kuweka matumizi ya mizani rasmi kwa mazao hapa nchini?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa Mkoa wa Dodoma una mifugo mingi na kunahitajika kiwanda cha kuchakata mazao ya mifugo; Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kiwanda hicho katika Mkoa wa Dodoma?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fatma Toufiq. Mpango wa Serikali ni kujenga viwanda vya kuchakata nyama, huu ni mkakati pamoja na faida ya zao hili la nyama, tunalenga kutumia njia hii kuwashawishi wafugaji waweze kutoa mifugo yao kwenye sehemu za hifadhi. Kwa hiyo Sekta binafsi inahamasishwa na tuna machinjio hapa, tunategemea kutengeneza Kongwa, Ruvu, na tunaimani kwamba kwa kuwa na Kongwa na machinjio ya Dodoma kiwanda kitaweza kutangamka. Lakini nichukue fursa hii kukuomba Mheshimiwa Mbunge, ukimuona Mwekezaji yeyote mwambie aje awekeze Dodoma, mimi ninazo ekari 200, kama anataka kuwekeza aje tushirikiane nitampa eneo, ajenge sehemu ya kuchakatia, machinjio tunayo ni sehemu ya kuchakatika nyama tu.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU (K. n. y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA) aliuliza:- Njia pekee ya kuinua uchumi wa Taifa linalotegemea kilimo kwa sehemu kubwa ni pamoja na kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo na mifugo; (a) Serikali ina Mkakati gani wa kujenga viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo na mifugo kwenye Mikoa yote ya kilimo na yenye mifugo mingi nchini; (b) Wafanyabiashara wa mazao ya kilimo na mifugo wanafanya udanganyifu mkubwa wa kujaza magunia lumbesa, kutanua madebe, pia kupima mifugo kwa macho na kwa kupapasa hali inayowaumiza na kuwapa hasara kubwa wakulima. Je, kwa nini Serikali inashindwa kuweka matumizi ya mizani rasmi kwa mazao hapa nchini?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii.
Kwa kuwa, ndizi ni kati ya zao ambalo linatumika sana nchini lakini kipimo chake kimekuwa na tatizo na wakulima wa ndizi wanapunjika sana zikiwemo ndizi kama mishale, minyenyele, mlelembo, toke, kitarasa na mtwishe. Mheshimiwa Waziri anatueleza nini kuhusu soko la bidhaa kama hiyo?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ndizi zimenilea, lakini msema kweli ni mpenzi wa Mungu, sijui international standard za kupima ndizi, nitakwenda kuwa task watu wa TBS na watu wa vipimo kusudi tuweze ku-establish kipimo standard cha ndizi. Lakini kitakachoamua bei nzuri kwa mkulima ni soko la ndizi, watu wa (TAHA) Tanzania Horticulture, chini ya ndugu Jacquline wanatafuta soko la ndizi nje ya nchi, na tumeshapata soko ambalo tunahitaji kuuza nje ya nchi tani 50 kwa wiki. Kwa hiyo tunawasiliana na mama Raymond kusudi tuweze kumuunganisha na Jacquline tuone kama Kilimanjaro mnaweza kulima kusudi kupeleka nje ya nchi.

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU (K. n. y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA) aliuliza:- Njia pekee ya kuinua uchumi wa Taifa linalotegemea kilimo kwa sehemu kubwa ni pamoja na kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo na mifugo; (a) Serikali ina Mkakati gani wa kujenga viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo na mifugo kwenye Mikoa yote ya kilimo na yenye mifugo mingi nchini; (b) Wafanyabiashara wa mazao ya kilimo na mifugo wanafanya udanganyifu mkubwa wa kujaza magunia lumbesa, kutanua madebe, pia kupima mifugo kwa macho na kwa kupapasa hali inayowaumiza na kuwapa hasara kubwa wakulima. Je, kwa nini Serikali inashindwa kuweka matumizi ya mizani rasmi kwa mazao hapa nchini?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru pia kwa juhudi nzuri za Mheshimiwa Waziri anazozifanya katika kuhakikisha kwamba Mikoa ambayo inalima mazao mbalimbali, inakuwa na uwezekana wa kupata viwanda vya ku-process hayo mazao. Mkoa wetu wa Tabora una zao la tumbaku, na juhudi ambazo anazifanya Mheshimiwa Waziri tunaziona;
Je, Mheshimiwa Waziri anatuelezaje kuhusu uwezekano wa kupata mwekezaji wa kuja kuweka kiwanda katika cha kuchakata kuchakata zao la tumbaku katika Mkoa wetu wa Tabora?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambayo ninayahangaikia sana ni kuweza kupata viwanda Tabora. Kwa sababu ameniuliza kuhusu tumbaku nitajibu tumbaku lakini siku nyingine nitakueleza na viwanda vingine ambayo viko kwenye pipe line. Tumehangaika, tumewapata Wachina tunawashawishi wakatengeneze kiwanda cha ku-process tumbaku pale, lakini panapo majaliwa ya Mwenyenzi Mungu, huenda mwisho wa mwezi huu au mwezi ujao nikaenda Vietnam, nakwenda mahsusi kutafuta kiwanda cha tumbaku na kukipeleka Tabora, kwa hiyo nahangaika jambo la muhimu watu wa Tabora muiombee Serikali hii ili kusudi tuchape kazi.