Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza ujenzi wa nyumba za kambi ya Polisi Mabatini zilizoanza kujengwa tangu mwaka 2012 na sasa zinazidi kuwa magofu ili zisaidie hizo familia chache zipatazo 13?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza; namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri yaliyonyooka, ningependa sana kujua swali langu la kwanza kwamba, pamoja na fedha zilizotengwa, ni kiasi gani cha fedha hasa kilichotengwa kwa sababu hiyo ingetusaidia kuwa uhakika na hii bajeti kwamba fedha hizi zilizotengwa zitakwenda kukamilisha majengo haya, ili kuwafanya Askari hawa waliosubiri takribani miaka minne sasa walau hizi familia ishirini zipate makazi bora na salama ya kukaa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa sababu tunafahamu Nyamagana ndiyo kitovu cha Mkoa wa Mwanza, nyumba hizi zinazotarajiwa kukamilika zinaweza kukidhi mahitaji ya familia zisizozidi ishirini na tano. Ukweli ni kwamba Askari ni wengi na umuhimu wa kambi hii ni mkubwa sana kwenye Mkoa wa Mwanza. Sasa ningependa tu kujua mpango wa Serikali, kuongeza nyumba zingine kwa muda na wakati ili Askari hawa wanaoishi kwenye kambi hiyo ya Mabatini na familia zao ambao sasa ina mwingiliano mkubwa na wananchi wa kawaida waweze kupata makazi mengine bora zaidi ili waweze kuwa kwenye mazingira salama nakushukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mabula kwa jitihada zake za kushughulikia changamoto za Jimbo lake. Tulikuwa pamoja kwenye ziara wakati nilipokwenda kutembelea Nyamagana na alitupa ushirikiano mkubwa sana. Kuhusiana na kiwango ambacho kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo ni takribani shilingi milioni 565 kwa kuwa nyumba zenyewe zimefika katika hatua ya mwisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili alitaka kujua kwamba kwa kuwa hizo ni familia chache ambazo zitakidhi kukaa katika nyumba hizo, kuna mpango gani mwingine nilitaka nimjulishe tu kwamba, tuna mpango wa kujenga nyumba takribani 300 kupitia ile programu ambayo iko katika hatua nzuri za utekelezaji wa ujenzi wa nyumba 4,136 nchi nzima.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza ujenzi wa nyumba za kambi ya Polisi Mabatini zilizoanza kujengwa tangu mwaka 2012 na sasa zinazidi kuwa magofu ili zisaidie hizo familia chache zipatazo 13?

Supplementary Question 2

MHE. KANGI A. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.
Kwa kuwa, Jimbo la Mwibara ambalo kwa muda mrefu kulingana na jiografia yake matukio kwenye visiwa ya ujambazi tulishaomba kuwa na Wilaya ya kipolisi. Je, Serikali mpaka sasa ina mpango gani wa kujenga kituo cha Polisi na kutupa hadhi ya Wilaya ya kipolisi. Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, upo mpango wa kujenga vituo vya Polisi nchi nzima, ambapo kimsingi tuna upungufu mkubwa wa vituo vya Polisi vinavyokadiriwa kuwa zaidi ya 4,500 nchi nzima ikiwemo eneo ambalo Mbunge amelizungumza. Kwa hiyo, nichukue fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tunatambua changamoto ya upungufu wa vituo vya Polisi ikiwemo katika Jimbo lake na tupo katika harakati za kuhakikisha kwamba tunapunguza tatizo hilo katika Jimbo hilo na maeneo mengine ya nchi nzima.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza ujenzi wa nyumba za kambi ya Polisi Mabatini zilizoanza kujengwa tangu mwaka 2012 na sasa zinazidi kuwa magofu ili zisaidie hizo familia chache zipatazo 13?

Supplementary Question 3

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa, humu ndani maswali yote huwa yanaelekeza nyumba za Polisi. Je, Waziri anasema nini kuhusu nyumba za Askari Magereza hapa nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pia tuna tatizo la upungufu wa nyumba katika Jeshi la Magereza. Kama ambavyo ipo katika Jeshi la Polisi, pia iko programu ya ujenzi wa nyumba ambazo zinakwenda sambamba na hizi za Polisi, kwenye Polisi tuna nyumba 4,136 na Magereza tuna nyumba takribani 9,500 kama nitakuwa sijakosewa sawasawa takwimu zake. Kwa hiyo, tunatambua hiyo changamoto na zipo katika hatua nzuri tu za utekelezaji naamini kabisa katika kipindi cha miaka mitano hii, tutaanza kuona miradi mbalimbali ya ujenzi wa nyumba hizi pindi mipango ya upatikanaji wa fedha na taratibu za kifedha kupitia Hazina itakapokamilika basi nyumba za Polisi na Magereza kwa pamoja zitakwenda sambamba.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza ujenzi wa nyumba za kambi ya Polisi Mabatini zilizoanza kujengwa tangu mwaka 2012 na sasa zinazidi kuwa magofu ili zisaidie hizo familia chache zipatazo 13?

Supplementary Question 4

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii.
Kwa kuwa, tatizo la Nyamagana la nyumba za makazi ya Polisi linafanana sana na tatizo la makazi kwa Polisi wa Kisiwa cha Mafia. Je, Mheshimiwa Naibu waziri anaweza kulitolea maelezo gani tatizo la makazi kwa Polisi wa Kisiwa cha Mafia? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli lipo tatizo la makazi ya Polisi pia katika Jimbo la Mafia. Nataka tu nimpe taarifa Mheshimiwa Dau kwamba katika ujenzi wa hizi nyumba ambazo tunataka kujenga, kwa upande wa Pwani tunatarajia kujenga nyumba 150. Mpaka sasa hivi, bado mchanganuo wa ujenzi kwa kila Wilaya ama kila Jimbo haujakamilika. Kwa kuwa, Mheshimiwa Mbunge amelizungumza hilo tatizo la Mafia basi tutalichukua tuone katika ujenzi wa hizo nyumba 150 kwa upande wa Pwani tuone uwezekano wa kuweza kuhakikisha kwamba naamini kabisa Mafia itakuwa imo katika mpango huu, lakini siwezi kuzungumza ni nyumba ngapi kwa upande wa Mafia, hilo tunaweza tukafanya kazi kwa kushirikiana mimi na yeye baadaye.