Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Primary Question

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itaelekeza kwa wananchi maamuzi ya Timu ya Mawaziri iliyozunguka kwenye maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na mapori ya hifadhi? (b) Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na wananchi itaweka mipaka kati ya mapori ya hifadhi na vijiji vinavyoyazunguka ili kupunguza migogoro iliyopo na kuwezesha wananchi kufanya shughuli za kiuchumi bila usumbufu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza. Naomba niulize swali moja tu la nyongeza nalo ni hili lifuatalo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa utekelezaji wa maamuzi wa maelekezo na kazi nzuri iliyofanywa na mawaziri hawa nane bado hayajafanyika, na kwa kuwa bado maelekezo yaliyotolewa wakati timu hiyo inaundwa kwamba wananchi waachwe maeneo yao wakiendelea na shughuli za maendeleo bado halijavunjwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa je, ni kwa nini wananchi wa vijiji 11 wanavyozunguka pori la Akiba Mkungunero bado mifugo yao inakamatwa? Na wananchi bado wanapigwa na maaskari hawa wakiwa kwenye maeneo yao hayo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ashantu na kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Kaimu Naibu Waziri wa Maliasili nilitaka nimpe maelezo Mheshimiwa Mbunge kwamba tumepata maelekezo maalum ya Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu, kwamba sasa tuunde timu kwenda kufanya uhakiki wa maeneo hayo kama Mkungunero ambalo anahangaika nalo na mimi nalijua sana. Na ilikuwa lazima Mheshimiwa Rais mwenyewe atoe idhini na maelekezo hayo na ametoa maelekezo ya huruma kabisa kwamba pamoja na maelekezo yale ya awali, lakini nendeni mkafanye uhakiki kabisa ili tuone namna ya kumaliza jambo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka kumhakikishia timu ya watalaam itakuja Mkungunero mwezi wa kumi na maeneo mengine yenye migogoro kama hii kwa sababu inajulikana. Tumeagizwa tufanye kazi hiyo ya uhakiki ili kukomesha kabisa migogoro hii kwa kadri itakavyowezekana. Uamuzi umetolewa na Mheshimiwa Rais. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tutakuja kushirikiana pamoja na wewe na viongozi wengine na viongozi wa mkoa katika kuhakikisha mambo haya yanakwisha.

Mheshimiwa Spika, tunajua yapo mengi huyu ameuliza katika mengi mengine na wewe hata leo uliunda kamati fulani niende kule nimewaambia kidogo, lakini nataka kukuhakikishia kwamba haya maneno Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo maalumu.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itaelekeza kwa wananchi maamuzi ya Timu ya Mawaziri iliyozunguka kwenye maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na mapori ya hifadhi? (b) Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na wananchi itaweka mipaka kati ya mapori ya hifadhi na vijiji vinavyoyazunguka ili kupunguza migogoro iliyopo na kuwezesha wananchi kufanya shughuli za kiuchumi bila usumbufu?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa maelezo haya mazuri, lakini sasa wakati wananchi wanaendelea kusubiri hii kauli ya njema sana ya Mheshimiwa Rais. Nini kauli ya Serikali kwa maafisa hawa wanyamapori ambao wanaendelea kunyanyasa wananchi na kukamata mifugo yao kwa kipindi hiki?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, narudia tena kwamba Mheshimiwa Rais amesema kazi iendelee. Anatambua uamuzi uliotolewa na Awamu ya Tano na yeye amesisitiza kwamba wananchi wote waliopo kwenye maeneo yao wasiondolewe katika vile vijiji 920, uamuzi huo upo vilevile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ametupa kazi ya ziada kwenda kufanya uhakiki wa hali halisi iliopo. Kwa hiyo, ningeomba na wananchi nao wasitumie vibaya uamuzi huu wa Serikali wakafiri kwamba basi wasiondolewe maana yake ni kujipanua wanavyotaka. Tafadhali wakae kama walivyokuwa ili kazi hii ya uhakiki ije iwatendee haki kwa sababu hii pande mbili kuna upande huo wa wananchi, lakini upande wa Serikali.

Mheshimiwa Spika, kuna wananchi wengine tulivyotoka na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kule Katavi, baada ya kutoa tamko lile pale watu waliingia kwenye Msitu wa Mbuga ya Katavi. Kwa hiyo, na wananchi nao wasubiri nia njema ya Rais wa Awamu ya Sita ni kutenda haki. Tufanye uhakiki kama alivyoagiza halafu uamuzi utatolewa.

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo, jambo hilo litatekelezwa, lakini wakati huo huo kazi iendelee maana yake uamuzi ule, ule uliotolewa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Sita amerudia maagizo yale yale kwamba nataka wananchi wote waliopo kwenye vile vijiji 920 wasiondolewe. Kwa hiyo, nadhani hakuna mtu wa Serikali anayewaondoa watu katika maeneo yale. (Makofi)

SPIKA: Kwa muda mrefu Wabunge walikuwa wakisubiri taarifa ile ya mawaziri nane, tunajua ni taarifa ya Serikali sijui kama imefikia kiwango cha Wabunge kuweza kujua angalau kilichomo au bado ni...Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana leo asubuhi uliunda kamati mbili twende tukawasilishe ile taarifa, lakini nimewaomba rasmi kwamba jambo hilo ndilo ambalo Mheshimiwa Rais ametupa maelekezo mwezi huu uliopita. Kwa hiyo, nikawaomba radhi kwamba kwa sasa hatuna jipya watusubiri kidogo kazi hii ya kwenda kufanya uhakiki wa kina wa leo kwa sababu maamuzi haya yametolewa miaka mitatu, lakini hali ya leo ni tofauti na yeye ni Rais wa Awamu wa Sita amemetutuma mwezi uliopita.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimewaomba radhi kwamba kwa leo hatutatoa hiyo taarifa, lakini itakapokamilika huu uhakiki wa uandani ambao kwa vyovyote vile tukipita mikoani tutawakuta na Waheshimiwa Wabunge huko baada ya kukamilika hiyo kazi na Mheshimiwa Rais akitolea maamuzi tutakuja kuileta taarifa hiyo.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itaelekeza kwa wananchi maamuzi ya Timu ya Mawaziri iliyozunguka kwenye maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na mapori ya hifadhi? (b) Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na wananchi itaweka mipaka kati ya mapori ya hifadhi na vijiji vinavyoyazunguka ili kupunguza migogoro iliyopo na kuwezesha wananchi kufanya shughuli za kiuchumi bila usumbufu?

Supplementary Question 3

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nataka kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa miaka mitatu, minne iliyopita mawaziri nane hawa walipewa kazi ya kupita huko wilayani na vijijini kwa ajili ya kuhakiki mipaka na matatizo mengine kama hayo. Lakini baadhi ya wilaya kama Wilaya ya Songwe ilikuwa bado wakati huo ni wilaya mpya hatukufikiwa na timu ile na wale watalaamu na sasa hivi ukimuambia Mheshimiwa Waziri anasema kwamba tena wameambiwa waende wakahakiki, lakini najua tunaweza tukasahaulika tena na anasema watapita huko na wataona na Wabunge, lakini Wabunge wanaweza wasiwepo wakati huo.

Mheshimiwa Spika, kwa nini siku nne ambazo zimebaki hapa tusipewe kazi Wabunge tuorodheshe vile vijiji ambavyo vina matatizo ya mipaka na mambo mengine ili angalau tumpe Waziri atakapokuwa anakwenda huko awe tayari na feedback ya Wabunge? Ahsante.

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mulugo.

Mheshimiwa Spika, utakumbuka tulipoanza Bunge hili, nilileta maombi kwa Katibu wa Bunge kuuliza swali hili kwa Mheshimiwa Mbunge yeyote ambaye anakero yake atuandikie, walioandika, wameandika. Nakupa ruksa Mheshimiwa Mulugo kama unayo nikabidhi tu, sisi tunapenda kuwa na hiyo directory ya migogoro hii ili itusaidie.

Mheshimiwa Spika, lakini hata utaratibu utakaokwenda tukienda mikoani tutakutana na viongozi wote kwa ujumla ili watuambie haya kwa sababu siyo kweli kwamba kamati hii ya watu nane ilipita kila mahali hapana. Tulienda maeneo machache, lakini tuli-take stop taarifa mbalimbali ya kamati mbalimbali ikiwemo Kamati ya Bunge mbalimbali zilizoundwa humu. Zilikuwa na taarifa nyingi sana ndiyo tumetumia zile taarifa kuchambua juu ya migogoro mbalimbali iliyopo, siyo kwamba sisi ndiyo tumegundua migogoro ilikuwepo katika nyaraka na tume mbalimbali za Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge wote ambao wanafikiri wanazo taarifa za ziada, ambazo wanafikiri tungependa kuzijua, ruksa tupo hapa tupatieni tu sisi tutaweka kwenye rekodi yetu siyo lazima iwe sisi kuna taarifa nyingine kama hizo za mipaka ya vijiji na vijiji siyo lazima sisi. Mamlaka zipo kule tutawaelekeza watafanya tu. Kwa hiyo, ni fursa kwa Waheshimiwa Wabunge wakati wowote kutupa hiyo kazi. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itaelekeza kwa wananchi maamuzi ya Timu ya Mawaziri iliyozunguka kwenye maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na mapori ya hifadhi? (b) Je, ni lini Serikali kwa kushirikiana na wananchi itaweka mipaka kati ya mapori ya hifadhi na vijiji vinavyoyazunguka ili kupunguza migogoro iliyopo na kuwezesha wananchi kufanya shughuli za kiuchumi bila usumbufu?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la mwisho.

Mheshimiwa Spika, miaka mitatu iliyopita ni kweli iliundwa timu ya mawaziri wanane na walizunguka kwenye wilaya baadhi ya wilaya na wilaya nyingi. Lakini, ombi langu kwa Mheshimiwa Waziri ziara ile ya mawaziri imekuwa kama ni ya kificho ficho, yaani tunawasikia tu, walipita, walipita, yaani sehemu hata ambazo hazina umuhimu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa na sisi ndiyo tunaolalamikiwa kila siku tunakuja kuuliza haya maswali. Kwa nini Serikali au Waziri asiweke mpango mzuri, timu inapoenda kwa mfano Wilaya ya Geita tujulishwe Wabunge na sisi tushiriki kwenye kuonyesha ile mipaka ili kuondoa ile sintofahamu. Ni hayo tu. (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Musukuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, timu yetu ilikuwa na hadidu za rejea, haikuwa kutembea tu, na kuchunguza kila kitu, tulikuwa tumepewa hadidu za rejea na mambo fulani za kushughulikia, ilikuwa ni migogoro maalumu yenye mwiingiliano kati ya hifadhi na wananchi na vijiji, kulikuwa na migogoro hiyo maalumu.

Mheshimiwa Spika, lakini katika kufanya kazi hii nimesema hatukupita kila mahali kwa sababu tulikuwa tayari tuna taarifa, moja ya taarifa kubwa tuliyokuwa nayo ilikuwa migogoro ya wafugaji na wakulima ambayo ilikuwa ni Tume ya Bunge iliundwa hapa na Bunge lako Tukufu nayo tulitumia na tume nyingi nyingi na taarifa mbalimbali. Lakini tukawa tunataka kujiridhisha juu ya yale yaliyoandikwa kwa hiyo tulienda sehemu chache sana.

Mheshimiwa Spika, tunajua nchi hii kuna migogoro ya mipaka kati ya vijiji na vijiji ambayo si ngumu sana kusuluhisha. Tumeagiza sana viongozi wa mikoa na wilaya kwa sababu mwenye mamlaka ya kuunda maeneo ya utawala ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hakuna kijiji kilichoanzishwa wala wilaya wala mkoa ambayo mipaka yake haikuandikwa kwenye GN ni suala la kwenda kusoma GN kwenye uwanda na kuamua mpaka upo wapi kwa sababu hawatakiwi kuunda mipaka ya utawala, mipaka ya utawala imeshaandikwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ipo migogoro mingi inayoendelea vijiji na vijiji kata kwa kata, sijui tarafa kwa tarafa ni uzembe tu. Tukishirikiana migogoro hii itaisha kwa sababu ina maandishi yake. Kwa hiyo, Mheshimiwa Musukuma nataka kukuomba kama kuna mgogoro wa mpaka wa wilaya usisubiri ile tume, tuambie hizo ndiyo kazi zetu za kila siku.

Mheshimiwa Spika. kwa hiyo, tutenganishe kati ya ile kazi ya Tume na shughuli zetu za migogoro kila siku, shughuli kama kuna migogoro mingine mliyonayo Waheshimiwa Wabunge tupeni hizo ndiyo kazi zetu, wizara yangu inatatua migogoro kila siku, kama kuna mtu unamgogoro usisubiri Kamati ya Mawaziri msife na hiyo migogoro tupeni tuifanyie kazi hata sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tutatuma wataalamu, tunavyo vifaa vya kutosha na wizara yangu hivi sasa imeanzisha Ofisi za Ardhi kila mkoa, kuna ma-surveyor kuna kila mtu, tutakuja kuainisha mipaka. Na katika kuahinisha mipaka Mheshimiwa Musukuma ndiyo tunavyofanya tunachukua viongozi wa pande mbili zote wanaobishania mipaka tunaamua kwa pamoja hatuendi sisi peke yetu, na ndiyo maana hata hii ya uhakiki wa Maliasili ipo mipaka iliyowekwa kwenye Hifadhi na Maliasili.

Mheshimiwa Spika, lakini tunataka tuunde timu maalumu ambayo wananchi na majirani pale na viongozi watahusika katika kuhakiki mipaka ya hifadhi ili waridhike kwamba mipaka hiyo inafanana kabisa na ile mipaka iliyoandikwa kwenye GN za Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kazi hiyo tupeni tuifanye msisubiri kamati ya watu wa nane ni kazi yetu ya kila siku.