Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Vijiji na Kata katika Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo havijapata umeme vitapata umeme?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize mswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, kuna baadhi ya vijiji ambavyo vimeachwa katika huu mkakati ambao sasa unaenda kutekelezeka wa vijiji hivi 29, mathalani Vijiji vya Sagara, Itaja, Kinyamwenda, Mwighanji, Itamka, Endesh, Sefunga, Namrama havijaonekana.

Sasa Serikali inampangao gani kuhakikisha vile vijiji vyote vilivyoachwa vionekane sasa katika ramani ili navyo vinufaike na mradi huu?

Mheshimiwa Spika, katika maeneo ambayo yameshapatiwa umeme, kuna vitongoji vikubwa vyenye hadhi ya kijiji na taasisi za umma kama vile shule na zahanati, lakini umeme umeishia pale tu center, na hapo hapo kuna maeneo ambayo tayari walishafanya na wiring waliagizwa wafanye wiring na umeme haujafika.

Sasa ningependa kujua Serikali ina mpango gani kuhakikisha maeneo yale ambayo ni makubwa yana hadhi ya kijiji nayo yapatiwe umeme? Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abeid, Mbunge wa Singida Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna vijiji ambavyo vilionekana vimebaki katika kuchukuliwa kwa awamu ya tatu mzunguko wa pili wa REA, na amevitaja vijiji sita, vijiji vitatu vya Endesh kinyamwenda na Endesh nyengine viko katika mradi wa backbone ambao unatoka Iringa kwenda kupeleka umeme mpaka Namanga, kwa hiyo ule mradi mkubwa umechukua vijiji vitatu ambavyo tutavipatia umeme. Mkoa wa Singida una vijiji saba ambavyo tumeviweka kwenye ule mradi, vijiji vitatu viko Singida Kaskazini na vitaingia kwenye huo mradi na vitachukuliwa na vitapatiwa umeme kufikia mwishoni mwa mwezi Julai.

Mheshimiwa Spika, vijiji vyengine vitatu vinavyobakia vimechukuliwa katika hivyo 26; kama tulivyosema hapo awali kwamba kuna maeneo ambayo yalikuwa yamebaki na takriban vijiji 680 vyote yameingizwa kwenye REA Awamu ya Tatu mzinguko wa pili, na yote yatafanyiwa kazi kwa pamoja ili inapofika Disemba 2022 vijiji vyote Tanzania Bara viwe vimepata umeme.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili ni kweli kwamba kuna maeneo yetu ya vitongoji bado hayajapata umeme, na kama ambayo tunavyokuwa tukisema maendeleo ni hatua taratibu tunawafikia, tulianza kwenye vijiji na tunamaliza Disemba mwakani, kwenye vitongoji tunaendelea kufika na speed yetu ni nzuri na tunamini kwamba muda kabla haujawa mrefu sana, kila kitongoji kitakuwa kimepatiwa umeme.

Mheshimiwa Spika, kwenye vitongoji TANESCO ni jukumu lao la kila siku wanaendelea kupeleke kwenye maeneo yetu, na REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unapoingia kijijini utafika pia kwenye vitongoji na pia miradi yetu mingine ikiwemo densification ambayo tunatarajia ianze mwezi wa 10 itachukua walau sehemu ya vitongoji ili zoezi
hilo la kupeleka umeme kwenye vitongoji liweze kukamilika na wananchi waweze kupata umeme, ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Vijiji na Kata katika Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo havijapata umeme vitapata umeme?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa dhamira ya Serikali ni kupeleka umeme katika vijiji vyote katika nchi ya Tanzania nzima ikiwemo na vitongoji, lakini kuna changamoto katika Wilaya ya Manyoni feeder ya Manyoni kutoka Singida ambayo inahusisha Wilaya ya Ikungi, Wilaya ya Manyoni na Halmashauri ya Itigi, umeme wake una katikakatika mara kwa mara, na ipo dhamira njema ya Serikali ya kujenga vituo vya kupozea umeme katika Mkoa wa Singida vipo vitatu ikiwepo Manyoni, Mitundu katika Jimbo langu na Iramba; je, ni lini ujenzi wa vituo hivi unaanza?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mgunge wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba yapo baadhi ya maeneo ambayo umeme wake unakuwa haufiki vizuri kwa sababu ya laini kuwa ni ndefu, lakini Mkoa wetu wa Singida ni mkoa mmojawapo wenye kituo kikubwa sana cha kupoza umeme pale mjini, na umeme unatokea pale kuelekea maeneo ya jirani, na tunao umeme wa kutosha kuweza kuhudumia maeneo yote. Ni kweli tunatarajia kuweka vituo vyengine vya kupoza umeme katika maeneo yetu ya Singida, mchakato wa kutafuta wazabuni na maeneo sahihi ya kuweka unaendelea, kabla ya mwaka huu haujaisha Waheshimiwa Wabunge wataona maendeleo katika maeneo yao na ikiwemo kwenye Jimbo lake ambapo tunatarajia kuweka kituo cha kupoza umeme kwa ajili ya kuweza kusambaza umeme kwa karibu zaidi katika maeneo yake.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Vijiji na Kata katika Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo havijapata umeme vitapata umeme?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na changamoto kubwa katika Mkoa wa Manyara ya upandishwaji wa gharama za umeme kutoka kwa wananchi kutoka unit zero mpaka kupelekwa unit one. Changamoto hiyo imetokea wananchi walikuwa wanalipa umeme wa shilingi 5,000 wanapata unit 41, na kwa sasa hivi wananchi wakinunua umeme shilingi 5,000 wanapata umeme unit 14; na Wilaya zilizoathirika ni Wilaya za Hanang, Mbulu, Babati, Simanjiro kwa ujumla wake mkoa mzima wa Manyara.

Nini kauli ya Serikali juu ya kuwapa umeme kwa bei ya kawaida wananchi wa Manyara ili waweze kujiinua kiuchumi na wasilale giza? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Taifa Vijana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba gharama za umeme ziko juu hata hizo zinazosemwa ni ndogo sisi bado tunaziona ziko juu. Nia ya Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha umeme unakuwa wa gharama nafuu na kila mmoja anaweza kuupata kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi pia na ya kijamii.

Mheshimiwa Spika, tariff tunazozitumia sasa zilitengenezwa mwaka 2016 na EWURA ndiyo msimamizi wa gharama za utoaji wa umeme kwa watu mbalimbali. Sasa naomba nieleze kinachotokea; zile tariff, ile kanuni ya gharama inasema mtu anayetumia unit sifuri mpaka unit 75 atakuwa-charged shilingi 100 kwa unit moja, yule anayetumia zaidi ya unit 75 na kuendelea gharama zake ni shilingi 200 hadi 350 kulingana na yuko kwenye tariff I, tariff II au tariff III.

Sasa kuna kifungu kwenye kanuni ile kiliwekwa kwamba wananchi wote wanaotumia umeme wakiwa maeneo ya vijijini wapate gharama hiyo ya unit moja shilingi moja na wanaozidi 75 waendelee kwingine. Wale ambao sio wa maeneo ya vijijini hawapati nafuu ya punguzo hilo la gharama.

Mheshimiwa Spika, lakini baada ya kuona kwamba kanuni hizo zilitengenezwa kipindi ambacho kulikuwa na shida sana ya upatikanaji wa umeme wa gharama nafuu kwa maana ya kutumia mafuta mazito na mitambo mingine, lakini sasa tuanzalisha umeme kutoka kwenye maji ambako ni nafuu, tunayo gesi yetu ya kutosha kabisa kwa ajili ya kuzalisha umeme.

Mheshimiwa Spika, tumekubaliana na wenzetu wa TANESCO, wakae chini, wa-review hizo gharama za kuuza umeme ili tuweze kupata umeme mwingi zaidi na tukauuza kwa gharama ndogo.

Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Asia pamoja na Waheshimiwa wengine watuvumilie kidogo, tuko katika mapitio mazuri kabisa ya kushusha gharama za kuuza umeme na kila mmoja atapata gharama hiyo ya umeme nzuri kabisa kwa ajili ya maendeleo kwenye maeneo yetu ya mijini na maeneo ya vijijini ili ile nia ya uwekezaji ambayo Mheshimiwa Rais anaitaka kwa Watanzania wote iweze kufikiwa kwa kila mmoja. Ahsante. (Makofi)