Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji katika Mji wa Vwawa?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri na jitihada za Serikali ambazo imefanya. Nashukuru kwa mpango wa muda mrefu, lakini mpango wa muda mrefu utachukua muda mrefu, sasa kwa mpango wa muda mfupi pale kwenye Mto Mantengu pale Vwawa; iwapo mnaweza kufunga pump mbili zenye uwezo wa kusukuma maji tunaweza tukapunguza upungufu wa maji katika Mji wa Vwawa kwa kiwango kikubwa.

Sasa je, ni lini Serikali itakuwa na mpango wa kufunga pump mbili kubwa za kuweza kusukuma maji katika katika Mto Mantengu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Rais wa Awamu ya Tano alipotembelea Mji wa Vwawa mwaka 2019 alitoa shilingi milioni 100 na ndio zikaenda kuchimba visima vitatu katika eneo la Ilolo, Old Vwawa na Naihanda. Lakini visima hivyo vilitelekezwa mpaka leo bado havijafunga miundombinu.

Sasa je, Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari kuambatana na mimi baada ya kipindi hiki cha Bunge ili twende tukaangalie hali halisi na tutatue changamoto ya muda mrefu ya wananchi wa Mji wa Vwawa? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ukimuona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Sasa nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge maji hayana mbadala na kwa kuwa tukiweka ama tukifunga pump mbili wananchi wako wanakwenda kupata maji toshelevu, nikuombe baada ya saa Saba tukutane tutoe fedha kuhakikisha kwamba pump zile zinapatikana na wananchi wako wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, nipo tayari kuongozana na wewe Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha kwamba tunakwenda kukulindia jimbo lako la Vwawa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji katika Mji wa Vwawa?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Wilaya ya Rungwe katika Kijiji cha Masukulu kumekuwa na shida sana ya maji japokuwa Serikali ilipeleka fedha. Je, hamuoni kuna haja ya kutuongezea fedha ili maji yaweze kuenea katika vijiji vinavyozunguka Kata ya Masukulu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, lakini kubwa ambalo nataka nimuhakikishie, Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan, dhamira yake kumtoa mwana mama ndoo kichwani, kwa hiyo sisi tupo tayari kutoa fedha kuhakikisha wananchi wako wa Masukulu wanapata huduma ya maji sasa.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji katika Mji wa Vwawa?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika ahsante kwa kunipa nafasi, Wilaya ya Wanging’ombe kuna Mradi wa Maji wa Igando - Kijombe wa shilingi bilioni 12 ulitakiwa uwe ushakamilika tangu mwaka 2019 lakini hadi sasa hakuna kitu kinachoendelea. Nilitaka kujua lini Serikali itakamilisha mradi huu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, sawa na nataka niseme tu unatosha mpaka chenji inabaki, lakini kubwa ambacho ninachotaka kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha, sasa sisi tumeshapatiwa fedha kuhakikisha kwamba tunakamilisha miradi mbali mbali, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaupa nguvu mradi wake, kuhakikisha tunapeleka fedha kwa wakati, ili mradi ukamilike na wananchi waweze kupata huduma maji safi na salama.