Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Kwa muda mrefu Jimbo la Arusha Mjini limekuwa likisumbuliwa na changamoto ya mafuriko kwenye Kata ya Sembetini, Levolosi, Osunyai, Sekei, Unga Ltd, Sakina, Baraa na Olerian yanayosababishwa na miundombinu mibovu ya barabara ya Sakina – Tengeru na Airport – Soko la Kilombero?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba Mheshimiwa Waziri hafahamu kwamba hii ni changamoto kubwa sana kwa Jiji la Arusha na inaathiri karibuni Kata 15 Kata ya Ulolieni, Kata ya Balaha, Kata ya Sekei, Kata ya Kimandolu, Sakina, Kaloleni, Revolosi, Sombetini Osunyai, Unga Limited, Yalelai, Daraja Mbili, Mulieti, Sokonwali na Sinoni. Unaona zaidi ya nusu ya kata zote zina changamoto hii.

Mheshimiwa Spika, kwanza nilikuwa naomba kufahamu ni wadau gani walioshirikishwa ikiwa Ofisi ya Mbunge haijashirikishwa, nimeongea na watu wa TARURA hawajashirikishwa, lakini na madiwani pia wa kata zinazohusika pia awajashirikishwa; kwanza ningependa kufahamu ni wadau gani ambao wameshirikishwa kwenye hii study na kwenye solution ya hili jambo?

Mheshimiwa Spika, lakini ya pili nilikuwa naomba kwa uongozi wako kwa sababu jambo hili linahusisha Wizara mbili; Wizara ya Uchukuzi pamoja na wizara ya TAMISEMI; je, Waziri haoni haja kwamba wizara hizi mbili tukafanya kikao pale Jijini Arusha, kwa kushirikisha Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkuu wa Wilaya ili mwisho wa siku tutafute solution ya kudumu kwa wananchi wetu wa Jimbo la Arusha Mjini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi ni kwamba baada ya kupata hii changamoto ambayo mafuriko yanasababishwa na maji kutoka mlimani na Mheshimiwa Mbunge amekuwa analifuatilia sana, Serikali imeamua kufanya study kuona namna ya kuondosha hili tatizo.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye study hii baada ya kukamilika, itakapokuwa taarifa imepatikana hatutaanza kutekeleza mradi hapo ndipo tutakaposhirikisha wadau kulingana na taarifa za study zitakavyokuwa zimeonyesha kwamba sasa tunategemea kufanya hiki na hiki.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya tafiti hiyo kukamilika wadau hawa watashirikishwa kabla ya kuanza kutekeleza huo mpango ambao utakuwa sasa umebainika kutokana na study hiyo, lakini nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi tulipojenga barabara hii ya TANROADS barabara nyingi zinazoathirika na wananchi wanaoathirika ni wa Wizara sana wanaoshughulikiwa na TARURA na TAMISEMI.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Serikali tunafanya kazi kama timu tutaongea na TAMISEMI na si TAMISEMI tu tu pengine hata ofisi za mazingira na hata watu wa kilimo ambao pengine huko wanasababisha miundombinu yetu kuharibika. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mbunge kwamba kama Serikali tunafanya pamoja kuhakikisha changamoto hii tunaiondoa, ahsante.