Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vtuo vya kutolea huduma za afya Wilayani Ulanga?

Supplementary Question 1

MHE. SALIM A. HASHAM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Waziri yupo tayari kutembelea baadhi ya zahanati, vituo vya afya pamoja hospitali ya wilaya ili kujionea changamoto hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, kwa kuwa upungufu wa watumishi katika jimbo langu umefikia asilimia 67, je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza watumishi wa afya katika Jimbo la Ulanga? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya Mheshimiwa Salim Alaudin Hasham, Mbunge wa Jimbo la Ulanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni kama ombi, je, tupo tayari kutembelea jimbo lake na kujionea changamoto hizo zinazolikabili. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge tupo tayari mimi na mwenzangu Naibu Waziri wa TAMISEMI anayeshughulikia masuala ya afya Mheshimiwa Dkt. Dugange na tutafika katika eneo lake na kushuhudia haya ambayo ameyazungumza na tutachukua hatua za kimsingi kuwasaidia wananchi wa jimbo lake.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, ameuliza kama tupo tayari kuongeza watumishi. Niseme tu kwa kadri tutakapokuwa tunaendelea kupata kibali cha kuajiri kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi tutaendelea kuajiri na kuongeza watumishi. Kwa hiyo, katika nafasi chache tunazozipata kama ambazo tunakwenda kuziajiri nafikiri kabla ya mwisho wa mwezi huu tutakuwa na watumishi kwenye kada ya afya karibu 2,700. Kwa hiyo, miongoni mwa watumishi hao wengine tutawaleta katika jimbo lako ili waweze kusaidia kuongeza ile ikama ya watumishi wa kada ya afya. Ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vtuo vya kutolea huduma za afya Wilayani Ulanga?

Supplementary Question 2

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tatizo walilonalo Ulanga ni sawasawa na tatizo tulilonalo katika Wilaya Bunda hasa katika Jimbo la Mwibara. Je, ni lini Serikali itatusaidia kuondoa tatizo la madawa na vifaatiba katika zahanati zetu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA ((MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kajege, Mbunge wa Mwibara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, anachouliza Mheshimiwa Mbunge ni lini Serikali sasa tutasaidia kuondoa tatizo la vifaatiba na dawa katika jimbo lake. Ukiangalia katika bajeti za Serikali kila mwaka tumeendelea kuongeza fedha ili kuhahakisha tunasogeza huduma hizi kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mzuri, sisi wote ni mashuhuda bajeti ya vifaatiba na dawa kwa mfano katika mwaka 2015/2016 nchini ilikuwa ni shilingi bilioni 31, lakini katika mwaka 2021/2022 tunazungumzia bajeti ya dawa na vifaatiba nchi nzima ni shilingi shilingi bilioni 270. Kwa hiyo, niseme tu, tumeongeza bajeti tutaendelea kuongeza na kuboresha ili kuhakikisha tunaliondoa kabisa tatizo hili la huduma ya afya katika maeneo yetu yote nchini. Ahsante.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vtuo vya kutolea huduma za afya Wilayani Ulanga?

Supplementary Question 3

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukosefu wa dawa na vifaatiba imekuwa ni changamoto karibia nchi nzima. Je, ni kwa nini Serikali basi isihamasishe uwekezaji mdogo na mkubwa wa viwanda vya dawa na vifaa tiba ikiwa ni pamoja na kuondoa Kodi ya Forodha pamoja na masharti mengine ili basi viwepo viwanda vingi ambapo mwisho wa siku dawa hizi zitakwenda kuwasaidia Watanzania na hususani walio wengi huko vijijini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Agnesta Lambert ameleta pendekezo kwamba ni kwa nini sasa Serikali isione haja ya kuongeza uwekezaji kwenye viwanda vya kuzalisha dawa na vifaa tiba nchini ili kupunguza hii adha? Jambo hili ni jema, ndiyo maana sasa hivi sera ya Serikali ni kuhimiza watu wote wanaotaka kuwekeza nchini waje, ikiwemo kwenye sekta hii ya dawa na vifaa tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sisi tunawaruhusu watu wote na katika kipindi sahihi kabisa cha kuwekeza ni
sasa, kwa sababu Serikali imeboresha mazingira bora ya kufanya biashara nchini ambayo yanaruhusu wawekezaji wote kuwekeza ndani ya nchi. Ninaamini hao watakaokuja kuwekeza kwenye maeneo ya dawa na vifaa tiba wanapewa kipaumbele zaidi. Kwa hiyo, mazingira ya Serikali yako sahihi na tunawaruhusu na Serikali itaendelea kuwekeza zaidi. Ahsante.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vtuo vya kutolea huduma za afya Wilayani Ulanga?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa bajeti ya dawa ya Serikali imeongezeka kama ambavyo taarifa zinaonyesha kutoka shilingi bilioni 31 mpaka shilingi bilioni 270 na kwenye makabrasha ya Serikali inaonekana upatikanaji wa dawa umeongezeka kwa kiwango kikubwa lakini uhalisia kwenye Vituo vya Afya na Zahanati siyo sawa na hizi taarifa kwa sababu bado kwenye Jimbo la Sumve katika Vituo vya Afya na Zahanati tatizo la upatikanaji wa dawa bado ni kubwa sana: - (Makofi)

Je, Wizara haioni sasa umefika wakati muafaka wa kutengeneza utaratibu mahususi ambao utaisaidia Serikali kwenda kutatua tatizo hili kwa uhalisia kwa kupata taarifa halisi kutoka kwenye vituo na siyo makabrasha ambayo yanapatikana kwa wataalam? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Kasalali Mageni ame-suggest jambo jema ambapo ukiangalia katika hotuba ya Wizara ya Afya wakati wanaisoma hapa pamoja na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwenye Idara ya Afya ambayo sisi tunasimamia, katika moja ya changamoto ambayo imekuwa ikitukumba ni kwamba Serikali imekuwa ikipeleka dawa lakini haziwafikii walengwa kama ambavyo imekusudiwa. Sababu kubwa ilikuwa ni baadhi ya watumishi, sio wote, kutokuwa waaminifu; aidha kwa kuuza zile dawa ama wengine kutokuzitumia mpaka zina-expire, matokea yake wale wagonjwa wanaotakiwa wapatiwe zile huduma za kimsingi wanashindwa kuzipata.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sasa hizi Serikali tuko katika hatua za mwisho za kuandaa mfumo ambao sasa hivi utakuwa unajua dawa inayoingia na dawa inayotoka kiteknolojia. Kwa hiyo, naamini hiyo ndio itakuwa mojawapo ya suluhisho la kuondoa hii changamoto iliyopo sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)