Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha mashindano ya michezo mbalimbali kwa kila mwaka wakati wa sherehe za Muungano ili kudumisha hamasa za Muungano kwa vijana?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mbali na majibu mazuri yaliyojibiwa na Mheshimiwa Waziri, lakini bado nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kama ni hivyo ndivyo, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba katika hayo mashindano ambayo mnaenda kuyaandaa yanaenda kuwaunganisha vijana wa kike na wa kiume moja moja kwa moja au asilimia 50 ya wanawake na asilimia 50 ya wanaume katika hayo mashindano? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kama hivyo ndivyo, Mheshimiwa Waziri ni lini mashindano hayo yataanzishwa kwa sababu tayari tulishaona katika mpango kazi mmetuambia kwamba hayo mashindano yataanza. Nahitaji commitment ya Serikali, ni mwaka gani hayo mashindano yataanza? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri wangu kwa majibu mazuri, lakini nimpongeze dada yangu Latifa kwa sababu miongoni mwa vijana ambao wamewakilisha Tanzania mwaka huu katika mjadala wa siku ya Muungano, Latifa alikuwa mmojawapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hilo, suala zima la kuhakikisha wanawake na wanaume wanashiriki kwa uzuri zaidi, tutalifanyia kazi. Na bahati nzuri kama unavyofahamu Serikali ya Awamu ya Sita imejielekeza huko kuhakikisha mchanganyiko wa jinsia zote mbili zinashiriki vizuri. Wasiwasi wangu ni kwa wanaume tusijetukajikuta kwamba idadi ya wanaume ikawa ndogo kuliko idadi ya wanawake katika michezo hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika upande wa commitment jambo hili kwa sababu suala zima la uratibu na Wizara ya Michezo kule Zanzibar na Wizara ya Michezo hapa Bara tutalifanya, baadae tutatoa taarifa rasmi katika suala zima la mchakato wa michezo hiyo, ahsante sana. (Makofi)