Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Mradi mkubwa wa maji katika Mji wa Tunduma ili kutatua changamoto wanayoipata wakazi wa mji huo?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza mradi wa kutoka Ileje Mto Songwe kuja Tunduma ulifanyiwa upembuzi yakinifu kutoka mwaka elfu 2013 na kampuni ya networkers kutoka Marekani. Mradi huu ulikuwa unagharimu kiasi cha Shilingi bilioni tatu. Sasa nataka kujua;

Je, ni lini mradi huu utakamilika ili wananchi wa Tunduma waweze kunufaika na maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa wananchi wa Kata ya Mpemba na Kata ya Katete wamekuwa wakitegemea mradi wa maji kutoka katika Wilaya ya Mbozi maeneo ya Ukwile, lakini mradi huu umekuwa ukisumbua sana kutokana na miundombinu kuwa mibovu, miundombinu iliyopo ilitengenezwa kutoka mwaka 1971 sasa nataka kujua;

Je, ni lini Serikali itaweza kuboresha miundombinu hii ili wananchi wa Kata ya Katete na Kata ya Mpemba waweze kupata maji kwa ukamilifu kabisa? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Fiyao kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu wa maji kutoka Ileje kwenye Mto Bupigu ni mradi mkubwa. Kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi mwaka ujao wa fedha 2021/2022 mhandisi anatarajiwa kuja kwa ajili ya usanifu wa kina, na tunaratajia mwaka ujao wa fedha usanifu wa kina utakamilika. Kwa hiyo, kadri tutakavyokuwa tukipata fedha mradi huu utatekelezwa kwa haraka sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni kutokana na maeneo ya Mpemba na Katete kupata maji kwa kusumbua sumbua. Binafsi nimeshafika pale kwenye mradi ule, nilikwenda nikiwa na Mbunge wa Jimbo na tulifanya kazi vizuri sana na niliacha maagizo ya kujitosheleza. Na yule meneja ambaye alikuwa pale ambaye kidogo alisuasua tulimbadilishia kazi, tulimwondoa pale na sasa hivi anakuja meneja mwingine mwenye maagizo kamili ili miradi hii yote iweze kutekelezwa kwa kina.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Mradi mkubwa wa maji katika Mji wa Tunduma ili kutatua changamoto wanayoipata wakazi wa mji huo?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Licha ya kutengwa bajeti katika maeneo mbalimbali katika Wilaya ya Kyerwa katika Kata ya Kikukuru haikutengwa hata Shilingi moja; kata hiyo ina vijiji vitatu ambavyo hakuna hata kijiji kimoja chenye maji na wananchi wanatembea umbali wa muda mrefu kutafuta maji.

Sasa nataka kujua ni mpango gani mahususi wa kusaidia hiyo kata ili waweze kujikwamua na wao kupata maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata hizi alizozitaja katika Jimbo la Kerwa nazo pia zimepewa jicho la kipekee kabisa. Unaweza ukaona kwenye bajeti yetu huku haikupangiwa, lakini kipekee nipende kumshukuru Mheshimiwa Rais ambaye ameweka mkazo katika kuona miradi yote ya maji nchini itafanyiwa kazi. Kama mlivyomsikia, mama yetu ametuahidi kutuongezea fedha zaidi ili miradi yote iweze kutekelezwa. Hivyo nikutoe hofu Mheshimiwa Mbunge, mradi huu pia tutakuja kuutekeleza.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Mradi mkubwa wa maji katika Mji wa Tunduma ili kutatua changamoto wanayoipata wakazi wa mji huo?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi.

Naomba kufahamu, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji wa Ziwa Basutwa ambao utasambaza maji kwa vijiji tisa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hhayuma Mbunge wa Hanan’g kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi yote ambayo inapatikana kupitia maziwa makuu, mito na vyanzo vikubwa vya maji vyote vimepewa kipaumbele na Wizara. Na kama tulivyowahi kumsikia hapa ndani Mheshimiwa Waziri yeye mwenyewe ameshaji-commite kwa Serikali, kwamba lazima tutajitahidi kutatafuta fedha ili tuweze kuona maziwa makuu na vyanzo vikubwa vya maji vyote tunakwenda kuvitumia kadri fedha tutakakuwa tunazipata.