Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Katumbasongwe hadi Ileje kilometa 90.7 itaanza kujengwa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ni barabara muhimu sana kwa ulinzi wa nchi yetu hasa kwa upande wa Tanzania na Malawi, pamoja na hayo kuna barabara muhimu sana ambayo kwa uchumi wa Kyela inafaa ijengwe mara moja.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini barabara ya Ibanda – Itungi – Poti itaanza kujengwa rasmi?

Swali la pili, wakati wa ujenzi wa barabara ya Kikusya – Matema kuna madaraja ya chuma yaliyokuwepo kwenye Mto Lufilyo Nambaka yalitolewa. Je, Mheshimiwa Waziri, kwa sababu ya uhaba wa madaraja na watu wanaotembea kilometa nyingi kufuata daraja lilipo, Serikali haioni kwamba ni muhimu sasa madaraja yale yarudishwe Kyela ili yapelekwe sehemu zenye uhitaji za Ilondo, Ipande na sehemu za pale Ngorwa? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Anyigulile Mlaghila, Mbunge wa Kyela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Ibanda – Itungi – Poti imetengewa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami na naamimi tayari maandalizi yako ili iweze kutangazwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Kyela waiamini Serikali na hata akienda kwenye vitabu vyetu vya bajeti tumeonesha fedha ambayo imetengwa kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili haya madaraja ambayo anayasema. Madaraja haya ya chuma ni madaraja ambayo yanatumika kwa ajili ya kutumika pale panapotokea dharura. Kwa hiyo, madaraja anayoyasema ni kweli yalikuwepo lakini yalishapelekwa Katavi kwa ajili ya koa changamoto ambayo ilitokea. Kwa hiyo, kupitia Bunge lako Tukufu nimuagize Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mbeya aende akafanye tathmini halafu tuone kama tutapata madaraja sehemu nyingine tuweze kurejesha mawasiliano ili kuwapunguzia adha wananchi ambao wanakwenda mbali kwa ajili ya kupata huduma ya usafiri. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Katumbasongwe hadi Ileje kilometa 90.7 itaanza kujengwa?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tofauti kubwa kati ya miradi ya upembuzi yakinifu wa barabara zetu ukilinganisha na ujenzi, kwa sababu zipo barabara ambazo zimefanyiwa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2012 na bado hazijajengwa.

Je, Serikali haioni kwamba ipunguze miradi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili barabara ambazo zimeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwanza zijengwe, kwa sababu haiwezekani mwaka 2012 ifanyiwe upembuzi halafu uje kuijenga 2025 useme kwamba utaijengwa kwa data zile zile, ni lazima itabidi ujenge kwa data zingine.

Je, huoni kama Serikali inapoteza fedha nyingi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana nae kwamba tukifanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa muda inakuwa ni gharama kwa sababu itabidi tuje turudie, lakini azma ya Serikali wakati tunafanya upembuzi na usanifu wa kina inakuwa ni kuijenga barabara kwa kipindi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyosema kinachosumbua wakati mwingine ni upatikanaji wa fedha kwa kipindi hicho lakini ni muhimu tukafanya usanifu ili mara tunapopata fedha basi barabara hizo ziendelee kujengwa. Kwa hiyo, tutaendelea kufanya usanifu na kutafuta fedha. Ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka Katumbasongwe hadi Ileje kilometa 90.7 itaanza kujengwa?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Kwa kuwa tatizo lililopo Kyela ni sawasawa na tatizo lililopo katika Wilaya ya Halmashauri ya Msalala. Je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara inayotoka Busisi – Ngoma, Ngoma – Nyang’hwale, Nyang’hwale – Chela, Chela – Busangi – Kahama? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara anayoisema ya kutoka Busisi – Nyang’hwale na kupita kwenye Jimbo lake ni barabara ambayo tayari imeshafanyiwa usanifu na kinachosubiri ni upatikanaji wa fedha ili barabara hiyo iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi kwa kipindi cha miaka mitano nina uhakika zitajengwa kwa kiwango cha lami kadri fedha itakavyoendelea kupatikana. Ahsante.