Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka uwiano sawa wa mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani bila kujali mapato ya halmashauri husika ili kusaidia wanufaika wa mikopo wanaoishi nje ya miji wapate fursa sawa na wanufaika wa mijini?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushkuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza mawali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wakati Mheshimiwa Rais, mama Samia Suluhu Hassan, anahutubia wanawake wiki iliyopita, aliatoa maelekezo kwenye halmshauri zetu, waweze kutoa mikopo mikubwa kwa vikundi ili kuongeza tija ya mikopo hii. Je, lini halmashauri zetu zitaanza kutekeleza maagizo haya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wanawake wa Mkoa wa Arusha wamenituma, pmoja na makundi mengine tajwa ya vijana na walemavu, kumekuwa na urasimu mkubwa sana kupata mikopo ya halmashauri. Wanufaika hawa wanatembea umbali mrefu, kufatilia mikopo hii Halmashauri bila ya mafanikio, naomba kusikia kauli ya Serikali juu ya jambo hili, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa viti maalim kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, ni jambo la msingi sana, Mheshimiwa Rais wetu, mama Samia Suluhu Hassan, ameelekeza na ameweka msisitizo kuhakikisha kwamba, mamlaka za Serikali za Mitaa zinatoa mikopo yenye tija kwenye vikundi vya wajasirimali, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Ni kweli kwamba mikopo hii ambayo imekuwa inatolewa, imekuwa inatolewa kwa kiwango kidogo, ambacho hakiwakwamui wajasiriamali kutoka hatua moja kwend hatua nyengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais TAMISEMI, tumekwishatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa mamlaka ya Serikali za Mitaa, kuhakikisha wanatoa mikopo hiyo yenye tija, ya kuwawezesha sajasiriamali hao kujikwamua. Kwa hiyo naomba nimuhakikishie Mheshimiwa mbunge kwamba Serikali tayari inatekeleza maelekezo hayo ya Mheshimiwa Rais, na tumeshatoa maelekezo kwa Wakurugenzi na kazi hiyo inaendelea kuhakikisha mikopo ile inatolewa kwa kiwango kinachokubalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kweli kwamba kwa jografia ya halmashauri zetu nyingi, kuna umbali mkubwa kati ya maeneo ambayo wajasiriamali wanafanya shughuli zao, na Makao Makuu ambapo wanahitaji kupata huduma hizi za mikopo.

Mheshimiwa mwenyekiti, tumendelea kuboresha pia maafisa mikopo katika Halmashauri, maafisa wa maendeleo ya jamii kuwafikia wajasiriamali katika maeneo yao, kuwawezesha na kuwarahisishia uwezekano wa kupata mikopo hii. Na Serikali itaendelea kuboresha mbinu hizi ili kuendelea kurahisisha upatikanaji wa mikopo.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka uwiano sawa wa mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani bila kujali mapato ya halmashauri husika ili kusaidia wanufaika wa mikopo wanaoishi nje ya miji wapate fursa sawa na wanufaika wa mijini?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushkuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa pamekuwa na tatizo la matumizi ya hizi fedha za mikopo kwa maeneo mengi, na hasa maeneo mengine zimekuwa zikipelekwa kutumika kwenye maeneo yasiyo kusudiwa baada ya kukopwa.

Je, Serikali haioni wakati umefika sasa badala ya kutoa fedha, tutoe vifaa vinanyoendana na biashara husika au shughuli husika ambao inakopewa. Kwa sababu hivi vifaa tunahakika vitakwenda kufanya shughuli iliyokusudiwa, mfano, matrekta au vifaa vya uzalishaji badala ya kutoa fedha kama fedha. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Nape Moses Nnauye Mbunge wa Mtama kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, Serikali inatambua kuna mikopo ambayo inatolewa kwa maada ya fedha taslim kwenye vikundi, pia kuna mikopo ambayo sasa tumeboresha utaratibu wa kutoa vifaa vitakavyowawezesha wajasiriamali kutekeleza shughuli zao; Kwa hivyo wazo lake ni zuri sana. Na sisi kama Serikali tumelichukua tumeanza kulifanyia kazi, kuna vikundi ambavyo kimsingi vinahitaji vifaa, na kuna vikundi ambayo vitahitaji fedha kwa ajili ya aina ya shughuli zake, na hili nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kulitekeleza. Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti.