Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa Kilomita tano ndani ya Mji wa Bagamoyo itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa barabara hizi ahadi yake ni ya muda mrefu na zimetengewa kiasi kidogo sana cha pesa. Na tuna barabara nyingi sana ambazo katika Mji wa Bagamoyo zinahitaji kupata huduma ya lami, mfano.

Je, ni lini Serikali itachukulia umuhimu Barabara ya Makofia – Mlandizi kwa sababu ni barabara muhimu sana ambayo inapita katika chanzo cha maji ambayo wanakunywa watu wa Dar-es-Salaam pamoja na pwani ambapo panaitwa bomu. Ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami hii njia ili kunusuru magari yanayonasa kupeleka dawa wananchi waweze kunusurika afya zao katika mikoa hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Muharami Shabani Mkenge, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, kama ifuatatvyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa, moja kwamba hizi barabara imekuwa ni ahadi ya muda mrefu na fedha inayotengwa ni ndogo, lakini pili ameanisha Barabara ya Kofia – Mlandizi ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wake wa Jimbo la Bagamoyo kwamba, ni lini sasa Serikali tutatenga fedha:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kama nilivyojibu katika majibu ya awali kwamba, moja ya wajibu wetu sisi ni kupokea mapendekezo yanayoletwa na Wabunge, lakini la pili ni kuhakikisha kwamba, zile ahadi zote ambazo viongozi wetu wakuu walizitoa zinatekelezwa. Na tutaendelea kuzitekeleza kwa kadiri ya upatiakanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndio maana katika jibu langu la msingi nikasema niwaombe Wabunge wote wapitishe Bajeti Kuu ya Serikali ili kile chanzo kilichokuwa kimetengwa zile fedha maana yake zitaongeza kuna kitu tutakwenda kukifanya. Na haya maombi mnayoleta maana yake tutayatekeleza. Hakuna barabara yoyote inaweza kutekelezeka bila kuwa na fedha. Kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge muweze kufanya hivyo, ili tuweze kufanya kazi nzuri ya kuwasaidia wananchi wetu. Kwa hiyo, tunayapokea hayo tutayafanyia tathmini na tutayaweka katika mipango yetu, ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa Kilomita tano ndani ya Mji wa Bagamoyo itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa ahadi ya barabara hizi imetolewa pia kwenye Jimbo la Kibaha Vijijini kwenye Mji wa Mlandizi na tayari kuna barabara ya kilometa moja imeanza kutekelezwa na miezi sita sasa haijalipwa chochote. Je, Serikali haioni ni muda sahihi sasa kumalizia ile fedha ili mkandarasi amalizie ili hata ile kazi ambayo ameshaanza kufanya isiharibike?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara zote ambazo wakandarasi wako site zitaendelea kulipwa fedha ili ziendelee kukamilika, ikiwemo hii barabara ambayo umeitaja hapa.

Kwa hiyo, haitakwama kwa sababu ninaamini kabisa kwamba, sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kupitia TARURA tunapitia zile certificates ambazo wakandarasi wanazileta kwetu na tunazitolea fedha. Kwa hiyo, na hili tumelisikia na nikuhakikishie kwamba, itaisha kwa wakati kama ambavyo iliahidiwa na viongozi wetu wakuu, ahsante.