Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza mradi wa maji wa Mji Mdogo wa Chala ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni za mwaka 2020?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuweza kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Nkasi ina kadiriwa na changamoto kubwa sana ya maji, ni lini Seikali itatoa maji Ziwa Tanganyika ambacho ndiko chanzo kikuu cha uhakika kuweza kutatua changamoto Wilayani Nkasi?

Swali la pili; Wilaya ya Nkasi katika Tarafa ya Nkate upo mradi wa maji ambao umekaa muda mrefu sana Tarafa ya Nkate ambao unahudumia vijiji vya Ntuchi, Ntemba, Siriofu na Ifundwa, mradi huu Mkandarasi hajalipwa ili aweze kumaliza mradi huu na ipo kesi ambayo anatuhumiwa mahakamani, naomba Wizara hii iweze kushughulikia kesi ya Mheshimiwa Felix Mkandarasi atoke ili aweze kumalizia mradi huu umekaa muda mrefu wananchi wanahangaika na maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbogo Mbunge wa Nkasi Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, lini Serikali itatumia maji ya Ziwa Tanganyika kwa ajili ya kulisha katika Mji wa Nkasi wote. Serikali ya Awamu ya Sita katika vipaumbele vyake cha kwanza ni kuhakikisha kumtua ndoo kichwani mwanamama, kwa hivyo nataka nimhakikishie kazi kubwa imefanyika katika maji eneo la Ziwa Victoria kuyatoa na kuyapeleka Mikoa mbalimbali ikiwemo Tabora na kwingineko, kwa sasa kwenye bajeti hii ya 2021/2022 Serikali inaendelea kutafuta fursa ya kuona namna ya kuweza kusaidia na kwa hivyo hili la Ziwa Victoria naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge linaweza kuwa ni moja ya sababu ya kuweza kulifanyia kazi ili kuondosha hii adha inayowapata wananchi wa Nkasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili juu ya mradi uliokwama wa Kata ya Nkate jambo hili naomba nilichukue na mara baada ya kikao hiki kuisha tuje tulizungumze tulielewe tatizo lake ni nini na baadaye tuweze kulitatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)