Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ya malengo ya Mtaala wa Elimu ya Msingi na Sekondari nchini ili kuendana na uhitaji wa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la msingi lilikuwa linalenga kwenye malengo ya mtaala; na malengo ya mtaala kwa mujibu wa sera ni kumwandaa mwanafunzi ili aweze kuendelea na ngazi zinazofuata za masomo. Hii imesababisha wimbi kubwa la wanafunzi wanaoshindwa kupata hiyo nafasi ya kuendelea kuachwa na mfumo wa elimu.

Je, Wizara sasa ina mpango gani wa kuboresha mtaala kwa kuongeza malengo ya kumwandaa mwanafunzi kujiajiri kwenye mazingira yake? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ni lini sasa au ni kwa namna gani Serikali inakwenda kutoa elimu ya lazima hadi Kidato cha Nne. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama nilivyoeleza katika jibu langu la msingi kwamba tunakwenda kuwa na mjadala mpana ambao utakwenda kuhakikisha kwamba taaluma yetu na nchi yetu wapi tunapotaka kuelekea. Katika mjadala huo mpana tunaamini hayo malengo Mheshimiwa Mbunge anayoyazungumza, tutaweza kuyadadavua, kuyafafanua na kuyaweka kwa namna tunavyotaka yawe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyozungumza awali, kwamba mitaala yetu hii imekuwa ikifanyiwa maboresho na maboresho haya mara nyingi sana huwa yanalenga katika maeneo ambayo yamekuwa na changamoto. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mjadala wetu mpana huu, malengo haya ambayo anayazungumza yatakwenda kuzingatiwa na vilevile maboresho ya mitaala yetu ili sasa vijana wetu wanapohitimu waweze kujiajiri nayo vilevile yanaweza kuzingatiwa. Ahsante.