Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Kilosa hadi Mikumi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nashukuru kwa ujenzi unaofanyika. Licha hivyo nina maswali mawili mafupi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, tukiwa tunasubiri upatikanaji wa fedha na kwa kuwa upembuzi yakinifu umefanyika kwa muda mrefu, je, kuna mkakati gani wa Serikali wa muda mfupi wa ukarabati na kutambua sehemu korofi za barabara hii ya Mikumi – Kilosa ambao unaweza ukafanyika kwa upande wa lami nyepesi kwenye sehemu korofi?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa barabara hii inaendelea mpaka Magore, Tuliani, Mziha, Handeni kule Tanga; na sehemu ya Tuliani mpaka Mziha bado haijajengwa kwa kiwango lami. Ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami ili barabara hii ikamilike? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara kipande cha kuanzia Kilosa mpaka Mikumi fedha ya matengenezo ipo.

Kwa kuwa mvua ilikuwa inanyesha baada ya mvua tu kukatika wakandarasi watakwenda kazini kuhakikisha kwamba maeneo yote yale ambayo yalikuwa yana tatizo yanarekebishwa.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu kuweka lami nyepesi itakuwa ni gharama kwa sababu barabara hiyo iko kwenye mpango wa matangenezo na fedha inapopatikana tunaendelea kuijenga. Tutakachofanya tu ni kuikarabati kwa kiwango cha changarawe ili iendelee kupitika lakini tutakapopata fedha tutajenga barabara zote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu barabara ya kuanzia Mziha – Turiani, katika bajeti ya mwaka huu fedha imetengwa kwa ajili ya kuendelea kuanzia Turiani na kuendelea upande wa kwenda Tanga. Kwa hiyo, kama ataangalia bajeti iliyopitishwa fedha imetengwa kwa barabara zote hizo mbili kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)