Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Mji wa Mombo ni mji unaokua kwa kasi kubwa na kuna mradi mkubwa wa maji unaotoka Vuga – Bumbuli kwenda Mombo katika Kitongoji cha Mlembule na mradi huo utagharimu shilingi 900,000,000. (a) Je, ni lini mradi huo utakamilika? (b) Kwa kuwa mradi huo unapita katikati ya Mji wa Mombo, je, Mji wa Mombo utafaidikaje na mradi huo?

Supplementary Question 1

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Namshuruku Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yenye matumaini kwa wananchi wa Mombo lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi huu sasa hivi una muda mrefu na tatizo la maji la Mombo ni la muda mrefu na wananchi wameanza kukata tamaa; na kwa kuwa halmashauri mbili zilishakubaliana, ya Bumbuli na Korogwe kwamba maji yale yapitie katika vile vijiji vinavyolinda chanzo cha maji, ni wakati gani wananchi wale wa Korogwe Vijijini na Bumbuli wataanza kupata maji?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa sasa hivi Serikali imetutengea shilingi bilioni 1.9 kwa ajili ya mradi wa maji wa Korogwe Vijijini; kuna mradi wa maji wa Bungu, mradi huu hatukuwa tunatumia hela za Serikali, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yalitumia hela zao kukamilisha mradi huu ambao ulikuwa ni kwa ajili ya vijiji saba. Kati ya vijiji hivyo saba vijiji vinne tu ndivyo vimepata maji. Serikali iliombwa shilingi milioni 410 ili mradi huu ukamilike lakini mpaka sasa hivi hela hiyo haijapatikana. Vijiji ambavyo vimekosa ni Mlungui, Kwemshai na Ngulwi. Naomba sasa Serikali mtenge hela za dharura ili tukakamilishe mradi huo ambao haukutumia hela za Serikali, ni mashirika binafsi yaliamua kujenga mradi huo. Ahsante sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Nganyani kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza linaonesha Mheshimiwa Mbunge unawapenda wananchi wako na unataka hatua za haraka kuhakikisha kwamba wanapata maji. Wizara ya Maji na Umwagiliaji, wewe mwenyewe Mheshimiwa Mbunge na halmashauri yako naomba tushirikiane, tukutane ili tuone tunafanyaje kuhakikisha kwamba tunachukua hatua za haraka ikiwa ni pamoja na fedha ambazo umetengewa katika bajeti inayoanza Ijumaa tarehe 1 Julai, kuhakikisha wananchi watapata maji kwa haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali namba mbili, kuhusu Mradi wa Maji wa Bungu ambao umefadhiliwa na marafiki zetu lakini hawakuukamilisha. Katika vijiji vilivyotarajiwa ni vijiji vinne tu ambavyo vimepata maji vingine bado, tufanyeje?
Naomba pia hili tushirikiane, Mkurugenzi wa Halmashauri atuletee taarifa. Tumeahidi katika bajeti inayokuja, miradi yote iliyokuwa inaendelea, ili mradi tu ililenga kuwapatia wananchi maji, hata kama ilikuwa inafanywa na wewe mwenyewe na umefikia ukomo tupe taarifa Serikali itatoa hela ili tuweze kukamilisha miradi hiyo wananchi wapate maji.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Mji wa Mombo ni mji unaokua kwa kasi kubwa na kuna mradi mkubwa wa maji unaotoka Vuga – Bumbuli kwenda Mombo katika Kitongoji cha Mlembule na mradi huo utagharimu shilingi 900,000,000. (a) Je, ni lini mradi huo utakamilika? (b) Kwa kuwa mradi huo unapita katikati ya Mji wa Mombo, je, Mji wa Mombo utafaidikaje na mradi huo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Matatizo ya maji kwenye maeneo ya Shinyanga na Korogwe ni sawa na matatizo kwenye maeneo yetu. Naomba Serikali ituambie na iwape matumaini wananchi wa Tarafa za Sikonge, Kiwele, Inyonga mpaka Kwilunde ambako yeye Mheshimiwa Kamwelwe anawakilisha; ni lini sasa shida za maji za wananchi hao zitapungua au zitaisha kabisa? Ahsate sana.

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Sikonge, niseme kwamba tulikuwa tumetoa nafasi kwamba kila halmashauri ilete vipaumbele ya vijiji ambavyo wataanza navyo katika kutekeleza programu ya maji. Kwa hiyo, hayo maeneo anayoyasema Mheshimiwa Mbunge naamini kabisa halmashauri yake imeweka ndivyo vipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunasema katika miaka mitano tunataka tupeleke miradi ya maji, kwa maana ya upatikanaji wa maji na ule mtawanyiko utakuwa kwa asilimia 85 ikifika mwaka 2020. Katika kutekeleza miradi hii ndiyo wao watachagua ni ipi tuanze na maeneo yale ambayo hayana maji kabisa wangeweka ndiyo kipaumbele ili kusudi tufikie asilimia hii tunayotaka kuifikia tukifika mwaka 2020. Kwa hiyo, yeye ndiye anajua vizuri zaidi majina ya vijiji na zile kata na wao ndiyo wanatakaoweka vipaumbele, Serikali tutaviwekea bajeti ili tuweze kufikia lengo na wananchi wetu waweze kupata maji.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Mji wa Mombo ni mji unaokua kwa kasi kubwa na kuna mradi mkubwa wa maji unaotoka Vuga – Bumbuli kwenda Mombo katika Kitongoji cha Mlembule na mradi huo utagharimu shilingi 900,000,000. (a) Je, ni lini mradi huo utakamilika? (b) Kwa kuwa mradi huo unapita katikati ya Mji wa Mombo, je, Mji wa Mombo utafaidikaje na mradi huo?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru na mimi kupata nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kijiji cha Ikelu kinafanana kabisa na swali la Korogwe; kuna mradi wa kutoka Tove kuja Mtwango mpaka Ilunda, bomba la maji limepita lakini kijiji cha Ikelu ni kilometa mbili tu hakina maji. Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wananchi hawa hasa ikizingatiwa kuwa wako kilometa mbili tu toka bomba lilipo?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna mradi wa Tove-Mtwango ambao unapita karibu na kijiji hicho anachokisema. Awamu ya kwanza hatukuwa tumefikiria kijiji hicho kupata maji lakini sasa kwa jinsi tunavyotanua mtandao wananchi wale walioko umbali wa kilometa mbili toka bomba lilipopita tutaweza kuwaunganishia ili wapate maji.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:- Mji wa Mombo ni mji unaokua kwa kasi kubwa na kuna mradi mkubwa wa maji unaotoka Vuga – Bumbuli kwenda Mombo katika Kitongoji cha Mlembule na mradi huo utagharimu shilingi 900,000,000. (a) Je, ni lini mradi huo utakamilika? (b) Kwa kuwa mradi huo unapita katikati ya Mji wa Mombo, je, Mji wa Mombo utafaidikaje na mradi huo?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa hali iliyoko katika Mji wa Mombo inafanana kabisa na hali katika Mji wa Mafinga ambao unakua kwa kasi na kwa kuwa Mamlaka yetu ya Maji ya Mji wa Mafinga ni ile ambayo ni ya class C, kwa hiyo haijaweza kuwa na uwezo wa kuhudumia maeneo makubwa ya mji. Je, Serikali iko tayari kutusaidia watu wa Mafinga hasa katika Kata za Bumilayinga, Isalavanu na Lungemba japo kuchimbiwa visima?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Chumi, Mbunge wa Mafinga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikupongeze Mheshimiwa Chumi kwa sababu mara nyingi umekuwa unawasiliana na Ofisi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kuhusu kuwapatia maji wananchi wa Mji wa Mafinga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba category ya Mamlaka ya Maji ya Mafinga ni C ambayo inahitaji kupewa msaada na Wizara. Nikiri kabisa kwamba tayari kuna deni la shilingi milioni 150 kwa ajili ya kulipia TANESCO ili umeme uendelee ku-pump maji kupeleka kwa wananchi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Chumi kwamba Wizara ya Fedha kwa sasa imeweka utaratibu, itakuwa inalipa madeni hayo ya maji moja kwa moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu hoja ya pili ya kuchimba visima tuko tayari, Mheshimiwa Mbunge tushirikiane. Kuna hela tuliyokutengea kama itakuwa haitoshi basi ulete taarifa ili tuweze kutenga hela nyingine tuhakikishe hivyo vijiji ambavyo havijapata visima viweze kupata visima.