Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Je, lini Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe itakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi wa Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri ambayo yanatoa matumaini kwamba hospitali hii sasa itaanza kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, ili hospitali iweze kuanza kufanyakazi inahitaji matayarisho ya kuwa na vifaa tiba vya kutosha ikiwemo ultrasound, x-ray na vinginevyo vyote.

Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba inapofika Julai vifaa tiba vitakuwa vimeshapatikana ili wananchi wa mkoa huu waweze kupata huduma?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa ujenzi wa majengo haya mawili ambayo ameyasema umechukua muda mrefu sana kutokana na mfumo uliokuwa unatumika wa force account ambao haukuleta tija sana kwa sababu ya usimamizi hafifu.

Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba majengo yaliyobaki sasa wanatumia mkandarasi badala ya force account ili yakamilike kwa viwango vinavyokubalika?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA AFYA MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Japhet Hasunga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu upatikanaji wa vifaa tiba hivi ikiwemo x-ray, ultrasound na vingine vyote kwa ajili ya kuhakikisha kwamba huduma zinaanza Julai napenda kumhakikishia kwamba tayari tulishapewa fedha MSD inaendelea na manunuzi na ufuatiliaji unafanyika na x-ray itakayokuja na ultrasound tumelenga kuelekeza kwenye hizi hospitali kubwa ambazo tayari zimeshakamilika kwa ajili ya kuanza huduma.

Mheshimiwa Spika, aidha kwa sababu swali lingine la pili la nyongeza ni kuhusu mfumo huu wa force account kuchukua muda mrefu ni kwa sababu gani tusihamie kwenye utaratibu wa mkandarasi. Naomba kulichukua hili nikaangalie na kabla ya Bunge hili kwisha nitafika pale mimi mwenyewe nikaone uhalisia wa kasi jinsi unavyoendelea sasa hivi kwa ajili ya kufanya maamuzi hayo ambayo ameyapendekeza, ahsante.