Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM D. MZUZURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za viongozi waandamizi wa Serikali kama Makatibu Wakuu na Mawaziri katika Mji wa Dodoma kwa ajili ya makazi ya viongozi hao?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Spika, niseme wazi tu sijaridhika na majibu ya Serikali kwenye swali hili ambalo ni la mkakati na lina umuhimu sana na niseme tu mimi kama Mbunge mwenyeji nimeshafuatwa sana na Naibu Mawaziri huku kuwatafutia nyumba za kuishi na kwa kweli wanatusababishia mtaani watu wengi kukosa.

Mheshimiwa Spika, iliwezekana Dar es Salaam kule Masaki, kule Mikocheni kujengwa nyumba kwa ajili ya viongozi. Kwa nini ishindikane mbona mji wa Serikali tumeujenga? Kwa hiyo naomba kwa kweli nitakuja kulirudia hili swali na lije na majibu yanayoeleweka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini tumeona jitihada za Serikali katika ujenzi wa makao makuu katika kuendeleza miundombinu yetu.

Maswali mawili ya nyongeza; la kwanza naomba kuuliza je wamefikia hatua gani katika ujenzi wa airport ya kule Msalato? Lakini la pili katika ujenzi wa barabara ya mzunguko kwenye Jiji letu la Dodoma? Nnashukuru.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu maswali ya nyongeza mawili ya Mheshimiwa Mariam Ditopile kama ifuatavyo:-

Kwanza ni kweli kwamba Waheshimiwa Wabunge wameleta maombi mbalimbali ya nyumba pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali. Lakini tumeshatoa maagizo kwa Meneja Mtendaji Mkuu wa TBA na kuna viongozi wengine ambao walishastaafu yaani walikuwa Wabunge siyo Wabunge tena hapa Dodoma. Wengine walikuwa ni viongozi wa Serikali siyo viongozi wa Serikali walikuwa wanatumia hizo nyumba mpaka tunavyozungumza hapa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo wameshapewa notice nadhani ndani ya wiki mbili zijazo utapata taarifa halisi na baadhi ya Wabunge watapata nafasi ya nyumba hizi.

Mheshimiwa Spika, lakini maswali yake mawili kama ifuatavyo; la kwanza ni kweli kwamba Kamati ya kwako ya Kudumu ya Miundombinu, mwezi huu unaoishia walitembelea eneo la uwanja wa ndege wa Msalato, lakini pia na barabara za mzunguko hapa Dodoma naomba niseme tu kwamba fedha zipo za kulipa fidia. Pale Msalato kuna baadhi ya wananchi ambao hawakuwepo wakati wa fidia, fedha zipo zoezi linafanyika ndani ya muda mfupi sana zoezi litakamilika.

Mheshimiwa Spika, kujenga uwanja wa ndege wa Msalato pamoja na ring roads ni ahadi ya Serikali na Mheshimiwa Rais Mama Samia ameshatoa maagizo na maelekezo tutasimamia na itatekelezwa, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, lakini tumeona jitihada za Serikali katika ujenzi wa makao makuu katika kuendeleza miundombinu yetu.

Maswali mawili ya nyongeza; la kwanza naomba kuuliza je wamefikia hatua gani katika ujenzi wa airport ya kule Msalato? Lakini la pili katika ujenzi wa barabara ya mzunguko kwenye Jiji letu la Dodoma? Nashukuru.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. MARIAM D. MZUZURI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za viongozi waandamizi wa Serikali kama Makatibu Wakuu na Mawaziri katika Mji wa Dodoma kwa ajili ya makazi ya viongozi hao?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; kwa nini Serikali isijenge nyumba ambazo watakuwa wanaweka mkataba kwa Wabunge kila baada ya miaka mitano ambao wanaendelea wataendelea kukaa kwenye nyumba hizo, lakini ambao watakuwa hawaendelei basi nyumba hizo Wabunge wapya wanaokuja wakaweza kukaa. Kwa nini Serikali isiwe na mpango wa kujenga nyumba namna hiyo?(Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kama nilivyosema kwenye maelezo yangu ya awali hizi nyumba zimekuwa na matumizi ambayo ni mabaya na tumekuja kugundua kuna baadhi ya watu wana nyumba zao hapa kwa sababu hizi za Serikali gharama ni chini kidogo wanapangisha za kwao hizi wanakaa nazo.

Mheshimiwa Spika, tumeshatoa maelekezo TBA kwamba wapitie na kimsingi ni nchi nzima ikiwepo ni madeni ambayo ni makubwa yapo watu wanadaiwa hawajalipa fedha ya Serikali na kupelekea wanashindwa hata kukarabati nyumba hizo.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili kwamba kama kuna mtu alikuwa ni Mbunge hapa Dodoma, ameshamaliza kipindi chake ile nyumba inapaswa irejeshwe au alikuwa ni mtumishi wa Serikali hizi nyumba zinapaswa kutumiwa na viongozi waliopo kwa wakati huu katika nafasi zao. Wazo lako ni jema Mheshimiwa Mbunge tulipokee tutalifanyia kazi ahsante sana. (Makofi)